SERIKALI YAUNDA TUME KUBAINI CHANZO CHA MOTO JNIA
HomeJamii

SERIKALI YAUNDA TUME KUBAINI CHANZO CHA MOTO JNIA

Serikali imesema imeunda Tume ya uchunguzi ya watu 12 ili kuweza kuchunguza na kubaini chanzo cha ajali ya moto iliyotokea jana saa Tano u...

TRA YATWAA TUZO YA UBUNIFU WA MIRADI KWA SEKTA ZA AFRIKA
BENKI YA MWALIMU, (MCB), YATOA SEMINA KWA WASHIRIKI WA KONGAMANO LA KISWAHILI, CHUO CHA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE KIGAMBONI JIJINI DAR ES SALAAM
RAIS DKT MAGUFULI AKUBALI OMBI LA KUJIUZULU WADHIFA WAKE DC WA UYUI MKOANI TABORA
Serikali imesema imeunda Tume ya uchunguzi ya watu 12 ili kuweza kuchunguza na kubaini chanzo cha ajali ya moto iliyotokea jana saa Tano usiku katika chumba kidogo cha kuhifadhia mizigo kilichopo kwenye jengo la Pili la abiria (Terminal II) katika uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam leo, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa amesema kuwa  Tume hiyo iliyoundwa inaongozwa  na Joseph Nyahende ambae anatoka katika ofisi za  Makao Makuu ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini.
“Ninategemea kupata ripoti ya kitaalamu kutoka kwa Tume hii, ili kutusaidia kubaini kiundani juu ya chanzo haswa kilichopelekea moto huu”, amesema Waziri Mbarawa.
Aidha, Waziri Mbarawa amefafanua kuwa huduma katika jengo hilo  zinaendelea kama kawaida ambapo awali zilisitishwa na kuhamishiwa katika Jengo la Kwanza la abiria (Terminal I).
“Mara baada ya moto kutokea, kitu cha kwanza kilichofanyika ni kuudhibiti moto huu ili usiweze kusambaa katika maeneo ambayo hayajaathirika, kisha tukatafuta njia za kurudisha huduma kwa abairia”, amesisitiza Profesa Mbarawa.
Katika hatua nyingine, Profesa Mbarawa ameipa miezi miwili  kampuni ya mizigo ya Swissport kurekebisha huduma zinazolalamikiwa na wateja wake na endapo itashindwa hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Uwanja wa Ndege wa JNIA, Paul Rwegasha ameeleza kuwa tathmini na gharama za mizigo iliyokuwa imehifadhiwa katika chumba hicho bado haijajukana, ambapo ripoti itaeleza gharama hizo pindi itakapokamilisha uchunguzi wake.


Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, 
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: SERIKALI YAUNDA TUME KUBAINI CHANZO CHA MOTO JNIA
SERIKALI YAUNDA TUME KUBAINI CHANZO CHA MOTO JNIA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjFbs7kcP5UFMgb01_uQUbWfzjQCf-c5T-1R38-LWyCXA1Kdo-qyl65I9Pa_2HmFmZW5OGU3_I6z59WjiEN6YSHGedP0hD1UfMrIng9dwjJcs-h13pljtiTvFUW_k4e4ka1p1REpZsOqUR4/s640/unnamed+%252820%2529.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjFbs7kcP5UFMgb01_uQUbWfzjQCf-c5T-1R38-LWyCXA1Kdo-qyl65I9Pa_2HmFmZW5OGU3_I6z59WjiEN6YSHGedP0hD1UfMrIng9dwjJcs-h13pljtiTvFUW_k4e4ka1p1REpZsOqUR4/s72-c/unnamed+%252820%2529.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/01/serikali-yaunda-tume-kubaini-chanzo-cha.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/01/serikali-yaunda-tume-kubaini-chanzo-cha.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy