CCM YAWEKA HADHARANI SIRI YA USHINDI WA CHAGUZI ZAKE ZA MADIWANI TANZANIA BARA NA UBUNGE ZANZIBAR
HomeSiasa

CCM YAWEKA HADHARANI SIRI YA USHINDI WA CHAGUZI ZAKE ZA MADIWANI TANZANIA BARA NA UBUNGE ZANZIBAR

Katibu wa Itikadi na Uenezi, Humphrey Polepole akifafanua mambo mbalimbali mapema leo kwenye Ofisi ndogo za Makao Makuu ya CCM, L...

RAIS MAGUFULI ANAVYOLIRUDISHA AZIMIO LA ARUSHA KWA SPIDI
CUF NGOMA BADO NZITO
KINANA AKUTANA NA BALOZI WA JAMHURI YA KOREA KUSINI HAPA NCHINI


Katibu wa Itikadi na Uenezi, Humphrey Polepole akifafanua mambo mbalimbali mapema leo kwenye Ofisi ndogo za Makao Makuu ya CCM, Lumumba Dar es Salaam, kuhusiana na ushindi wa chama cha Mapinduzi (CCM) katika chaguzi mbalimbali zilizofanyika hivi karibuni za Madiwani na nafasi ya Ubunge huko Zanzibar.

Katika mkutano huo na Waandishi wa Habari, alielezea siri tatu muhimu zilizokiwezesha Chama hicho kupata ushindi, Polepole alizitaja siri ya kwanza ni namna ya mageuzi mapya ya kimuundo na mfumo yaliyolenga kukiwezesha CCM kurudi kwenye mikono ya wananchi kwa serikali yake kujikita zaidi kushughulikia kero zinazowakabili Watanzania na kufanikiwa.

Pole Pole alisema kuwa mabadiliko hayo yamelenga kukirejesha chama wenye misingi uliokifanya kuanzishwa kwake, akabainisha siri ya pili kuwa ushindi huo ni matokeo ya mafanikio ya serikali katika kuweka mikakati ya kubana mianya ya wakwepa kodi pamoja na vita dhidi ya ufisadi.

“Adui yetu mkubwa ni rushwa na vitendo vya ufisadi nchini, Watanzania ni mashahidi kwani muelekeo wa serikali umekuwa thabiti na tumeona watuhumiwa wa vitendo hivyo wakichukuliwa hatua,” alisema.Alisema kuwa siri ya tatu imetokana na kazi nzuri ya utendajikazi wa serikali kwenye utekelezaji wa ahadi zilizotolewa na Chama.
Baadhi ya Wanahabari wakimsikiliza Ndugu Pole Pole alipozungumza nao mapema leo jijini Dar.Picha na Michuzi Jr.

Katika hatua nyingine,Pole Pole alisema kuwa ahadi ya kutoa elimu bure kwa wanafunzi kuanzia elimu ya awali hadi kidato cha nne, imekuwa na uhalisia mkubwa.“Na zaidi ya yote ni huduma za kiuchumi ambazo zimeendelea kutekelezwa ambapo Chama tunaipongeza serikali na kuikumbusha katika maeneo mengine tuliyowaahidi wananchi, ikiwemo kuendelea kutenga asimilia 10 ya mapato ya Halmashauri kwa ajili ya vijana na wanawake.

“Hii itatoa nafasi kwa vijana na wanawake kupata fursa za mitaji na mikopo yenye masharti nafuu, hivyo suala hilo linapaswa kuwekewa msisitizo zaidi,” aliongeza.Alisema serikali inaendelea na mipango ya ujenzi wa viwanda, vinu vya usagaji mkoani Iringa na Mwanza pamoja na kiwanda cha mafuta ya Alizeti, mambo ambayo tayari Chama kimetoa maelekezo kwa serikali.

Akaongeza kuwa , ununuzi wa ndege kwa ajili ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) umesaidia kuwawezesha wananchi kusafiri kwenye maeneo mbalimbali katika kufanya shughuli muhimu za kiuchumi.

Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimeibuka na ushindi mnene katika uchaguzi mdogo wa marudio ya ubunge Jimbo la Diwani na udiwani kwenye kata 20 za Tanzania Bara, Katika uchaguzi huo, kwenye jimbo la Dimani, mgombea wa CCM, Juma Ally Juma, alipata ushindi wa kura 4,860 sawa na asilimia 78.74 dhidi ya mpinzani wake, Abdulrazak Khatib Ramadhan wa CUF, aliyepata kura 1,234.
Ushindi huo umedhihirisha anguko kubwa la CUF, visiwani Zanzibar kwani uchaguzi wa mwaka 2015 licha ya kushika nafasi ya pili, kilipata wastani wa kura 2,300 lakini kwenye uchaguzi wa marudio kura zake zimeshuka kwa zaidi ya asilimia 50.Hivyo ili kujinusuru na hali hiyo, CUF kimetakiwa kumtafuta mchawi aliyepo ndani ya chama hicho visiwani Zanzibar na si kulalamika. 
Aidha CCM imejizolea viti 19 vya udiwani kati ya 20 huku Chadema ikipata kiti kimoja na kufanya Chama kudhihirisha kuwa, bado kinakubalika kwa wananchi.Kufuatia ushindi huo, Chama kimewataka wanachama kurudisha fadhira za ushindi huo kwa wananchi kwa kuwachagulia viongozi wenye mioyo za kizalendo, wachapakazi waliokuwa tayari kuwasikiliza wananchi, katika uchaguzi wa ndani unaofanyika mwaka huu.
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: CCM YAWEKA HADHARANI SIRI YA USHINDI WA CHAGUZI ZAKE ZA MADIWANI TANZANIA BARA NA UBUNGE ZANZIBAR
CCM YAWEKA HADHARANI SIRI YA USHINDI WA CHAGUZI ZAKE ZA MADIWANI TANZANIA BARA NA UBUNGE ZANZIBAR
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjoePmx4e_fBJ8WHMEQXMR-b6QnizCjkahWEES5y5rvpROjzb0oZFmYRAhgolFkpd5xoVep28RtZm0zUrlghfwtRYan0xhDRcEmTAsgKNptcVS-ReBlIIgDZHIFR7cnfXkR4uOXc6asNuo/s640/OTH_9960.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjoePmx4e_fBJ8WHMEQXMR-b6QnizCjkahWEES5y5rvpROjzb0oZFmYRAhgolFkpd5xoVep28RtZm0zUrlghfwtRYan0xhDRcEmTAsgKNptcVS-ReBlIIgDZHIFR7cnfXkR4uOXc6asNuo/s72-c/OTH_9960.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/01/ccm-yaweka-hadharani-siri-ya-ushindi-wa.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/01/ccm-yaweka-hadharani-siri-ya-ushindi-wa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy