JESHI LA POLISI LAMTIA MBARONI MTUHUMIWA WA UTAPELI

Msemaji wa Polisi, Advera  Bulimba – ACP Na Dotto Mwaibale JESHI la Polisi nchini limefanikiwa  kumkamata mtuhumiwa wa utap...






Msemaji wa Polisi, Advera  Bulimba – ACP



Na Dotto Mwaibale


JESHI la Polisi nchini limefanikiwa  kumkamata mtuhumiwa wa utapeli anayejulikana kwa jina la  Wilfred Masawe (36) , Kabila mchaga na  mkazi wa  Buza, Temeke jijini Dar es Salaam.


Akitoa taarifa hiyo kwa vyombo vya habari Dar es Salaam leo, Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini Kamishna Msaidi wa Polisi (ACP), Advera  Bulimba amesema  mtuhumiwa huyo alikuwa akitumia mbinu mbalimbali kutapeli zikiwemo kujitambulisha kama kiongozi wa serikali kwa kutumia mtandao wa Whatsapp,  huku akieleza kuwa yupo nje ya nchi na kuna tatizo la msiba ambao umetokea nchini na unamuhusu na hivyo alikua akitoa maelekezo kwa watendaji wa serikali waweze kusaidia gharama za matibabu hospitalini, gharama za kusafirisha mwili wa marehemu na gharama za mazishi.


Alisema pia alikuwa akitumia mbinu ya kujifanya kiongozi mkubwa wa dini ya kikristo (Askofu) na kuwaambia waumini na viongozi mbalimbali kuhusu maandalizi ya makongamano ya kidini kwa lengo la kuwaomba michango kuweza kufanikisha makongamano hayo.


Alitaja baadhi ya matukio aliyofanikiwa kutapeli ni pamoja na kuwatapeli viongozi wa serikali, wafanyabiashara, mameneja na wakurugenzi wa taasisi za umma, wanasiasa pamoja na waumini wa madhehebu ya dini.


Aidha, matukio yote hayo alikuwa akiyafanya peke yake na alikua akiyaendesha kwa mawasiliano ya njia ya ujumbe mfupi (SMS) bila kuzungumza kwa simu.


Bulimba alisema Jeshi la Polisi linakamilisha taratibu za kisheria ili mtuhumiwa huyo afikishwe mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake.


Jeshi la Polisi nchini linaendelea kutoa tahadhari kwa wananchi wote kuwa makini na mtandao wa matapeli hao na yeyote mwenye  taarifa za matapeli anaombwa kuzifikisha haraka katika kituo chochote  cha Polisi kilicho karibu ili waweze kushugulikiwa haraka.


COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: JESHI LA POLISI LAMTIA MBARONI MTUHUMIWA WA UTAPELI
JESHI LA POLISI LAMTIA MBARONI MTUHUMIWA WA UTAPELI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiCAX1-AQE4hHAQPB4mPDc2UhAlq6mo9jCiq8akwlDop_KWK-KECc4tfWp1KbiFKl4tatEj7Fol3_6IlGoR-ObVdDDkh6liONI8q5GfXw3QloHyQKjkIrd4aRv1ggfTud9SvpkEp2dJjSIH/s320/Advera-Bulimba.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiCAX1-AQE4hHAQPB4mPDc2UhAlq6mo9jCiq8akwlDop_KWK-KECc4tfWp1KbiFKl4tatEj7Fol3_6IlGoR-ObVdDDkh6liONI8q5GfXw3QloHyQKjkIrd4aRv1ggfTud9SvpkEp2dJjSIH/s72-c/Advera-Bulimba.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2016/12/jeshi-la-polisi-lamtia-mbaroni.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/12/jeshi-la-polisi-lamtia-mbaroni.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy