WATUMISHI WA UMMA SASA KUFANYA MAZOEZI MARA MOJA KILA WIKI
HomeJamii

WATUMISHI WA UMMA SASA KUFANYA MAZOEZI MARA MOJA KILA WIKI

Mkurugenzi Msaidizi wa magonjwa yasioambukiza (NCD) Prof. Ayoub Magimba akisisitiza jambo mbele ya madaktari na wadau wa a...

RAIS DKT MAGUFULI AMJULIA HALI MEJA JENERALI MSTAAFU VICENT MRITABA ALIYEJERUHIWA KWA RISASI
POLISI WAKANUSHA ASKARI WAKE KUMFUATILIA MBUNGE LISSU KENYA
MAREKEBISHO VIDEO-ERIC SHITINDI:SERA MPYA YA VIJANA KUTATUTA CHANGAMOTO ZA VIJANA





Mkurugenzi Msaidizi wa magonjwa yasioambukiza (NCD) Prof. Ayoub Magimba akisisitiza jambo mbele ya madaktari na wadau wa afya ngazi ya mkoa na wilaya hawapo pichani wakati wa kufunga mkutano Wa siku tatu Wa Madaktari na wadau Wa afya ngazi ya mkoa na wilaya katika kupata mpango mkakati wa kujikinga na magonjwa yasioambukiza uliofanyika mkoani Morogoro. 

Baadhi ya Madaktari na wadau wa afya ngazi ya mkoa na wilaya hawapo waklijadili sera na mipango wakati wa kufunga mkutano Wa siku tatu Wa Madaktari na wadau Wa afya ngazi ya mkoa na wilaya katika kupata mpango mkakati wa kujikinga na magonjwa yasioambukiza uliofanyika mkoani Morogoro. 


Na Ally Daud-MAELEZO-MOROGORO

WATUMISHI wa Umma wametakiwa kufanya mazoezi ya viungo Mara moja kwa wiki ili kujiepusha na magonjwa yasioambukiza ili kujenga watumishi wenye afya imara kwa maendeleo ya taifa.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Msaidizi wa magonjwa yasioambukiza (NCD) Prof. Ayoub Magimba wakati Wa kufunga mkutano Wa siku tatu Wa Madaktari na wadau Wa afya ngazi ya mkoa na wilaya katika kupata mpango mkakati wa kujikinga na magonjwa yasioambukiza uliofanyika mkoani Morogoro.

“Katika mkutano huu wa kupata mpango mkakati wa kujikinga na magonjwa yasioambukiza tumeazimia kua na Sera inayoelekeza watumishi wote wa Umma wafanye mazoezi ya viungo siku moja kwa wiki ikiwa ni sehemu ya majukumu yao” alisema Prof. Magimba

Aidha Prof. Magimba amesema kuwa mazoezi hayo ni sehemu ya majukumu ya watumishi wa Umma ili kuwasaidia wale wanaokosa muda wa kufanya mazoezi majumbani kwao ili kujikinga na magonjwa hayo.

Mbali na hayo Prof. Magimba amesema kuwa watanzania wanatakiwa kuepuka matumizi ya Mara kwa mara ya Sigara na vileo kwa pamoja na badala yake wajikite kwenye mazoezi na utumiaji wa vyakula asilia. Kwa upande wake Daktari bingwa Wa magonjwa ya ndani Dkt. Meshack Shimwela ambaye ni mshiriki wa mkutano huo amesema kuwa watanzania wanatakiwa kuzingatia na utekelezaji wa Sheria za barabarani ili kupunguza idadi ya vifo vinavyotokana na ajali mpaka kufikia mwaka 2030.

“Watanzania hasa madereva wa vyombo vya moto wanatakiwa kuzingatia na kutii Sheria za barabarani hususani kuacha kuendesha vyombo vyao wakati wamelewa ili kupunguza asilimia 50 ya vifo vitokanavyo na ajali za barabarani hadi kufikia 2030” alisema Dkt. Shimwela Aidha Dkt. Shimwela amesema kuwa katika mkutano huo wameadhimia kuishauri serikali kutenga maeneo maalum ya kuvutia Sigara pamoja na kuweka muda maalumu wa kunywa pombe ili kujikinga na kuepuka magonjwa hayo.

Mkutano huo uliokutanisha madaktari wa ngazi za mkoa na wilaya zote nchini umelenga kutengeneza Sera na mikakati ya mwaka 2017 hadi 2020 katika kupambana na magonjwa yasioambukiza kama kisukari, kansa,shinikizo la damu, ajali za barabarani na uzito kuzidi kiasi ili kujenga taifa lenye afya na Maendeleo.
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: WATUMISHI WA UMMA SASA KUFANYA MAZOEZI MARA MOJA KILA WIKI
WATUMISHI WA UMMA SASA KUFANYA MAZOEZI MARA MOJA KILA WIKI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhd-Fk_m_E0e3KNd42BBkR29-i0K8jAkrfXS5cGzClTACYFuVVjuV8cScwX-TeL77p0bhRabUTZL-TcXepuar0DOWadvvB0evbUsf5qe2NDtreidEOsI6eEdz9sEEYBsSrcp1hStIXkM_M/s640/taku1-768x512.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhd-Fk_m_E0e3KNd42BBkR29-i0K8jAkrfXS5cGzClTACYFuVVjuV8cScwX-TeL77p0bhRabUTZL-TcXepuar0DOWadvvB0evbUsf5qe2NDtreidEOsI6eEdz9sEEYBsSrcp1hStIXkM_M/s72-c/taku1-768x512.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2016/11/watumishi-wa-umma-sasa-kufanya-mazoezi.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/11/watumishi-wa-umma-sasa-kufanya-mazoezi.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy