WAKOSEFU TBS WAJISALIMISHE KUOMBA MSAMAHA







 
 
HomeJamii

WAKOSEFU TBS WAJISALIMISHE KUOMBA MSAMAHA

    Serikali imewataka baadhi ya wafanyakazi wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) walioshirikiana na wenzao wa Mamlak...

WANAFUNZI LUGALO WALIA NA MIUNDOMBINU KWA WALEMAVU
SERIKALI YATOLEA UFAFANUZI ULIPAJI WA PENSHENI WASTAAFU WA SHIRIKA LA POSTA NA SIMU
WATU WANNE WANAOSADIKIWA KUWA MAJAMBAZI WAUAWA MKOANI PWANI


 

 


Serikali imewataka baadhi ya wafanyakazi wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) walioshirikiana na wenzao wa Mamlaka ya Mapato (TRA) kupitisha makontena zaidi ya 100 bila kukaguliwa na shirika hilo katika Bandari ya Dar es Salaam kujisalimisha haraka.

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Bw.Charles Mwijage alitoa agizo hilo mwishoni mwa juma wakati akizindua baraza la wafanyakazi wa Shirika hilo.“Nimeanza kukusanya orodha ya majina ya watu waliosaidia kupitisha makontena haya na nikija nayo hawatapona,” alisema.

Aliwataka wote wanaojijua kuhusika kujisalimisha mapema na kutubu ili wasamehewe kabla haya hatua hiyo.Makontena hayo yalipitishwa katika bandari ya Dar es Salaam hivi karibuni bila ya kuthibitishwa na shirika hilo.

Pia aliitaka TRA kuacha kutoa makontena bila ya shirika hilo kuthibitisha au kukagua ubora wa bidhaa zinazoingizwa hapa nchini sababu mwenye mamlaka hiyo ni TBS.

Alisema watakaotubu kuwa walishiriki waseme walishiriki vipi na lini, walishirikiana na nani na wataje sehemu yalikopelekwa makontena hayo ili serikali iweze kusaidia kukomesha hali hiyo.Alisema anaamini kuwa waliofanya hivyo katika mamlaka hiyo walifanya kwa utashi wao bila ya ushiriki wa viongozi wao na kwamba sasa wakati umefika wa kukomesha tabia hiyo.

Alilitaka baraza hilo kushirikiana na menejimenti na kuhakikisha matatizo yanayojitokeza yanapatiwa ufumbuzi kwa maslahi ya nchi na kwamba serikali itahakikisha inaongeza vitendea kazi na watumishi ili kufikia malengo ya shirika.

Kwa mujibu wa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Dkt. Egid Mubofu, baraza hilo lina wajumbe 48 wanaotoka katika vitengo mbalimbali na litakaa kwa muda wa miaka mitano.“Baraza hili linaundwa kutokana na mkataba wa menejimenti na Chama cha Wafanyakazi (RAAWU),” alisema Dkt. Mubofu na kuongeza kuwa menejimenti itashirikiana na baraza kufanyakazi za shirika kwa tija.

Alisema wafanyakazi wanatakiwa kufanya kazi kwa weledi na uadilifu katika majukumu yao ya kila siku.Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi (TBS), Prof. Mekanya Maboko alilitaka baraza hilo kufanya kazi kwa kushirikiana na menejimenti na bodi kuhakikisha shughuli za udhibiti wa ubora zinafanyika kwa ufanisi.

“Bodi itaendelea kuisimamia menejimenti na kuishauri ifanye kazi kwa kuzingatia sera na sheria,” alisema.
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: WAKOSEFU TBS WAJISALIMISHE KUOMBA MSAMAHA
WAKOSEFU TBS WAJISALIMISHE KUOMBA MSAMAHA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg95Jf2OrYsKVk2L258MMZD86Ghxx3v0bPZ8chHXbHEo2IdLMXI4sMtF1kHnidVGWQPOG9nTHRanpDX6_5Q0T461ZOKfXnVdQS4FBYK1TNE7xjatcVwgKuyasw5lVczhqW3kKHEg9DqrQM/s320/1455697278-Charles_Mwijage+2.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg95Jf2OrYsKVk2L258MMZD86Ghxx3v0bPZ8chHXbHEo2IdLMXI4sMtF1kHnidVGWQPOG9nTHRanpDX6_5Q0T461ZOKfXnVdQS4FBYK1TNE7xjatcVwgKuyasw5lVczhqW3kKHEg9DqrQM/s72-c/1455697278-Charles_Mwijage+2.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2016/10/wakosefu-tbs-wajisalimishe-kuomba.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/10/wakosefu-tbs-wajisalimishe-kuomba.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy