SHULE YA SEKONDARI MALANGALI YAPATA NEEMA KUTOKA MAAS

Hawa ndio baadhi ya wanafunzi waliowahi kusoma katika shule ya sekondari ya Malangali wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya ...








Hawa ndio baadhi ya wanafunzi waliowahi kusoma katika shule ya sekondari ya Malangali wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya  kuwasili katika shule hiyo na kukaangalia mazingira ya shule hiyo na kutafuta njia za kutatua baadhi ya changamoto kwa kushirikiana na serikali ya Jamhuri ya muungano ya Tanzania.
Mkurugenzi wa kampuni ya Yono Action Mart, Yono Kevela ambaye ni mlezi wa kundi la Malangali Alumni Association (MAAS) akizungumza na wanafunzi wa shule ya sekondari Malangali na kuwaeleza jinsi gani shule hiyo ilivyowapa mafanikio hadi sasa walipofikia. 
 



 Na Fredy Mgunda, Iringa

Wanafunzi waliowahi kusoma shule ya sekondari ya Malangali iliyopo wilaya ya Mufindi mkoani Iringa wamewataka vingozi, wafanyabiashara, wakulima na wajasiliamali mbalimbali walionufaika na elimu kutoka shule ya malangali kurudisha fadhila kwa shule hiyo.

Hayo yamesemwa na mkurugenzi wa kampuni ya Yono Auction Mart, Yono Kevela ambaye ni mlezi wa Umoja wa Malangali Alumni Association (MAAS), alisema kuwa maendeleo aliyoyapata sasa ni kutoka na shule ya Malangali hivyo ameamua kurudi na kuisadia shule hiyo. 

“Wafanyakazi na viongozi mbalimbali tunatakiwa kuboresha mazingira na miundombinu ya shule tulizosoma ili kuendeleza na kukuza elimu ya hapa nchini Tanzania.” alisema Kevela.

Pia amesema kuwa shule nyingi walizosoma viongozi, wafanya biashara na wajasiriamali mbalimbli zinahitajika kukarabatiwa, hivyo amewataka wadau wote kuzikumbuka shule walizosoma.

Naye Padre wa kanisa la Kikatoliki mkoani Mbeya Telesipholi Tweve aliwakata wanafunzi mbalimbali waliosoma katika shule kongwe kurudisha upendo katika shule hizo kwa kuwa ndio chanzo cha mafanikio yao ya sasa.

“Leo nimerudi katika shule hii ya Malangali kuja kusaidia kutatua changamoto ambazo zipo katika shule hii ukizingatia kuwa shule hii inauchakavu wa majengo na miundombinu hivyo sisi kama MAAS tumeanza kwa kukarabati ukumbi ambao utakuwa na faida kwao kwa kutumia kwenye sherehe na kukodishwa pia”. alisema Tweve

Kwa upande wake mwenyekiti wa Malangali Alumni Association (MAAS), Paul Mng’ong’o alisema kuwa wameanza kuisaidia shule ya Malangali muda mrefu kwa kuwa tayari wameshakarabati ukumbi wa shule, wamewanunulia Televisheni na King’amuzi kwa ajili ya habari na wanaendelea kutatua matatizo ya shule hiyo.

“Hebu angalia sisi tuliosoma hapa tumepata mafanikio lakini shule yetu bado ipo pale pale na inazidi kuchakaa hivyo inatulazimu kuchangishana ili kurudisha fadhila kwa kuwa wengi wetu tumepata mafanikio makubwa kwa kusomea kwenye shule hii, tuna viongozi wengi, wenye uwezo wengi, wakulima wakubwa sana hapa nchini wengi wamesoma katika shule hii”, alisema Mng’ong’o

Lakini pia Mng’ong’o alisema kuwa lengo la umoja wa MAAS ni kuunganisha wanafunzi wote waliowahi kusoma shule hiyo kuweza kupeana mawazo ya maendeleo na kusaidiana kufikia malengo.

Shule ya Malangali ni kati ya shule kongwe ambazo viongozi mbalimbali katika serikali, taasisi za umma na sekta binafsi walijengewa msingi wa awali wa maisha.

Katika mwaka wa bajeti huu serikali imetenga bajeti ya kukarabati shule kongwe zipatazo thelethini na saba (37) jambo ambalo wananfunzi hao wameomba serikali kuharakisha utekelezaji wake.  

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: SHULE YA SEKONDARI MALANGALI YAPATA NEEMA KUTOKA MAAS
SHULE YA SEKONDARI MALANGALI YAPATA NEEMA KUTOKA MAAS
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhYs7QBTwNQQfctDFd0e-eUggSVlVWqAUgYr63ia0eT8zIcxrzezMB7LkF6YCmqK5pWpy1B3B-v3smjCiOjLp7Y8gG6SZemnHgiXvIIYgYUKaKJIWYyVwtmxaQlMpIHSHGMfhcSDABsnlKe/s640/IMG_20161015_182642.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhYs7QBTwNQQfctDFd0e-eUggSVlVWqAUgYr63ia0eT8zIcxrzezMB7LkF6YCmqK5pWpy1B3B-v3smjCiOjLp7Y8gG6SZemnHgiXvIIYgYUKaKJIWYyVwtmxaQlMpIHSHGMfhcSDABsnlKe/s72-c/IMG_20161015_182642.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2016/10/shule-ya-sekondari-ya-malangali-yapata.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/10/shule-ya-sekondari-ya-malangali-yapata.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy