(TADB) KWA KUWAFIKIA WANANCHI WALIOWENGI-DK. KIJAJI.
HomeJamiiMikoani

(TADB) KWA KUWAFIKIA WANANCHI WALIOWENGI-DK. KIJAJI.

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii. MAENDELEO ya Viwanda yanahitaji mali ghafi za kilimo hivyo Benki ya Maendeleo ya  Kilimo nchini (T...

MAJALIWA AZINDUA KIWANDA CHA PLASTIC CHA LODHIA JIJINI ARSHA
RC MTAKA: VIONGOZI WA DINI NA WATANZANIA TUENDELEE KUMUOMBEA RAIS JOHN POMBE MAGUFULI
RC SINGIDA AWAAGA VIJANA WAHADZABE 43 WANAOENDA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA JESHI

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.
MAENDELEO ya Viwanda yanahitaji mali ghafi za kilimo hivyo Benki ya Maendeleo ya  Kilimo nchini (TADB) inawajibu ya kuwafikia wakulima ili matokeo ya viwanda yaweze kuonekana ikiwemo na kuwa na masharti ya riba nafuu au kuondolewa kabisa.

Hayo ameyasema leo Naibu Waziri wa Fedha , Uchumi na Mipango, Dk. Ashantu Kijaji wakati wa uzinduzi wa Bodi ya Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB), amesema kuwa sekta ya kilimo inaajiri watanzania asilimia 70 huku ikichangia pato la Taifa kwa asilimia 28 ambayo ni kidogo kutokana na ukuaji wa sekta ambayo inatakiwa kwenda na viwanda ambapo TADB ndio yenye kuweza kuleta mapinduzi hayo viwanda kwa kuwafikia watanzania waliowengi.

Amesema bodi ya wakurugenzi ya TADB inajukumu la kutekeleza na kuboresha sekta ya kilimo kwa kuwafikia watanzania wengi katika maeneo ya kijijini kutokana ni kuwa wazalishaji wa mazao mbalilmbali ambayo ndio yanaweza kuzalisha viwanda na nchi ikaweza kukua kiuchumi pamoja na kuongeza pato la taifa.

Dk. Ashantu amesema benki ya kilimo ihakikishe wanatafuta vyanzo vya fedha ili waweze kukuza mtaji na kutoa mikopo kwa wakulima kwa masharti nafuu katika kumfanya mkulima kuweza kunufaika kilimo chake.

"TADB ina deni kubwa kwa wakulima sasa ni wakati umefika wa bodi kufanya kazi kwa uadilifu katika kuinua sekta ya kilimo kwa kutoa mikopo na sio kwa bodi kufanya mikutano nje ya nchi na kuacha kutatua changamoto ya mikopo katika sekta hiyo" amesema Dk. Ashantu.

Nae Mweenyekiti wa Bodi hiyo, Rosebudy Kurwijla ameiomba serikali kuiwezesha benki ili kuweza kufikia wananchi waliowengi na wanahitaji ya kukopeshwa na TADB katika kuendeleza kilimo.
Amesema kilio cha TADB ni mtaji na bila kufanya hivyo itakuwa ni vigumu kuwafikia wananchi waliowengi.

Kwa upande wa Mkurugenzi Mwendeshaji wa TADB, Thomas Samkyi amesema mpango wao ni kufanya mazungumzo na wadau mbalimbali ikiwemo Benki ya Maendeleo ya Afrika  katika kuweza kupata mtaji wa kuweza kuwakopesha wakulima ili kuweza kutimiza adhima ya serikali ya awamu ya tano ya Tanzania ya Viwanda.
Mwenyekiti wa Bodi wa TADB, Rosebudy Kurwijila akizungumza katika uzinduzi juu ya majukumu ya bodi hiyo leo jijini Dar es Salaam.
 Naibu Waziri wa Fedha, Uchumi na Mpango, Ashantu Kijaji akizungumza wakati uzinduzi wa Bodi ya Maendeleo ya Kilimo (TADB) leo jijini Dar es Salaam.
 Naibu Waziri wa Fedha, Uchumi na Mipango, Ashantu Kijaji akipokea mfano wa hundi ya Sh.milioni tano kwa ajili ya tetemeko la Ardhi mkoani Kagera leo jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Fedha, Uchumi na Mpango, Dk.Ashantu Kijaji akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa bodi wa TADB leo jijini Dar es Salaam.
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: (TADB) KWA KUWAFIKIA WANANCHI WALIOWENGI-DK. KIJAJI.
(TADB) KWA KUWAFIKIA WANANCHI WALIOWENGI-DK. KIJAJI.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi7Wi2XEiI5F7x7odPcBMZWrGb-c55vbMoph_okufHVrsMWBB1-mVdkQrElRya8g1v38jyjTOW8wUI8MKJoyeQcKbQY-Wi5R6-z5xTNFuHz61S4cXvhxC1GRbJAgFFqz4JTGUV3_Ogk-j8/s640/0D6A8108.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi7Wi2XEiI5F7x7odPcBMZWrGb-c55vbMoph_okufHVrsMWBB1-mVdkQrElRya8g1v38jyjTOW8wUI8MKJoyeQcKbQY-Wi5R6-z5xTNFuHz61S4cXvhxC1GRbJAgFFqz4JTGUV3_Ogk-j8/s72-c/0D6A8108.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2016/10/maendeleo-ya-viwanda-yatatokana-na.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/10/maendeleo-ya-viwanda-yatatokana-na.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy