KIWANDA CHA NONDO KUIINGIZIA SERIKALI BILIONI 200 ZA KODI

SERIKALI inatarajia kukusanya sh. B ilioni 200 kwa mwaka, ikiwa ni mapato ya kodi baada ya kukamilika kwa ujenzi wa kiwanda cha kimatai...




SERIKALI inatarajia kukusanya sh. Bilioni 200 kwa mwaka, ikiwa ni mapato ya kodi baada ya kukamilika kwa ujenzi wa kiwanda cha kimataifa cha Kiluwa Steel Group kitakachokuwa na uwezo wa kuzalisha tani 3,000 za nondo kwa siku.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua kiwanda cha nondo cha Mohamed Kiluwa Group and Company  cha Mlandizi Mkoani Pwani, wakati alipokitembelea Julai 12, 2016.Kulia kwake ni Mkuu wa mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarest Ndikilo na kushoto kwake ni mmiliki wa kiwanda, Mohammed Kiluwa. (PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU)
Baadhi ya wakazi wa Mlandizi mkoani Pwani waliofika kwenye kiwanda  cha  nondo cha Mohamed Kiluwa Group and Company Limited  wakati Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  alipokitembelea Julai 12, 2016.
Baadhi ya wakazi wa Mlandizi mkoani Pwani waliofika kwenye kiwanda  cha  nondo cha Mohamed Kiluwa Group and Company Limited  wakati Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  alipokitembelea Julai 12, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua kiwanda cha nondo cha Mohamed Kiluwa Group and Company  cha Mlandizi Mkoani Pwani, wakati alipokitembelea Julai 12, 2016.Kulia kwake ni Mkuu wa mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarest Ndikilo na kushoto kwake ni mmiliki wa kiwanda, Mohammed Kiluwa. 
 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua kiwanda cha nondo cha Mohamed Kiluwa Group and Company  cha Mlandizi Mkoani Pwani, wakati alipokitembelea Julai 12, 2016.Kulia kwake ni Mkuu wa mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarest Ndikilo na kushoto kwake ni mmiliki wa kiwanda, Mohammed Kiluwa.

Awamu ya kwanza ya ujenzi wa kiwanda hicho kinachomilikiwa na mwekezaji mzawa kwa kushirikiana na Wachina, inatarajiwa kukamilika Oktoba, mwaka huu ambapo fedha hizo zitapatikana baada ya kukamilika awamu tatu za ujenzi wake.

Akizungumza mbele ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aliyetembelea kiwanda hicho jana (Jumanne, Julai 12, 2016), Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda hicho, Bw. Mohammed Kiluwa alisema ujenzi huo utasaidia kuimarisha uchumi.

“Kukamilika kwa mradi huo, kutaongeza kasi ya ukuaji wa uchumi wa nchi, upatikanaji wa ajira pamoja na kufanikisha azma ya serikali ya awamu ya tano ya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya maendeleo ya viwanda,” alisema.

Alisema kiwanda hicho kitazalisha nondo kwa matumizi ya ujenzi pamoja na vifaa vingine vinavyohusiana na bidhaa za chuma. “Lengo ni kuweza kuuza malighafi hizo kwenye viwanda vingine vya chuma nchini na nchi jirani kwa kuzingatia ubora unaokidhi mahitaji ya soko la kimataifa,” alisisitiza.

“Katika awamu ya kwanza ya ujenzi, tunatarajia kutumia dola milioni 40; awamu ya pili tutatumia dola milioni 50 na dola milioni 200 zitatumika kwenye awamu ya tatu ili kukamilishia ujenzi wa kiwanda hiki,” alisema.

Kiluwa alisema, awamu ya kwanza inatarajiwa kukamilika Oktoba mwaka huu, ambapo awamu ya tatu itakamilika Februari mwakani. Kikikamilika, kinatarajiwa kuajiri vijana zaidi ya 500 wa Kitanzania.

Kwa upande wake, Waziri Mkuu alisema lengo la ziara hiyo ni kukagua maendeleo ya ujenzi wa kiwanda hicho kikubwa cha kwanza kinachojengwa na mwekezaji mzawa.

“Uwekezaji sio lazima ufanywe na watu wa nje, Watanzania wana nafasi ya kuwekeza katika sekta mbalimbali, Kiluwa amefungua njia hivyo wengine wafuate nyayo zake. Uwezo tunao na sababu ya kuwekeza tunayo, kwani tunataka tuzalishe bidhaa mbalimbali sisi wenyewe,” alisema.

Aliongeza kuwa uwepo wa kiwanda hicho katika eneo la Disunyara, Mlandizi mkoani Pwani, utawezesha kuboresha hali ya uchumi kwa wakazi wa eneo hilo na Taifa kwa ujumla.

Waziri Mkuu alitolea mfano kwa wakazi wa Mtwara, ambao wamenufaika kutokana na ujenzi wa kiwanda cha saruji cha Dangote ambapo awali walikuwa wakinunua saruji kwa sh. 17,000, lakini hivi sasa wanainunua kwa sh. 7,000.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu alilitaka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) lipeleke umeme mapema kwenye eneo hilo ili kuharakisha shughuli za uwekezaji.


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
2 MTAA WA MAGOGONI,
S.  L. P. 3021,
11410 DAR ES SALAAM.
JUMATANO, JULAI 13, 2016

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: KIWANDA CHA NONDO KUIINGIZIA SERIKALI BILIONI 200 ZA KODI
KIWANDA CHA NONDO KUIINGIZIA SERIKALI BILIONI 200 ZA KODI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgVl2ObNzEurEBObVmYpPv7sNzfu-9jOlH_Jld8TABnwVIhjpVyRpBZ7k6iwGmHMW-3z6BsVNscPJCt_MrqkIgd4VT3RRimTCNr2SoHUqvtUS28KYhsy9dniK6nYygxJFDW2oD6AjIs7OY/s640/IMGS5175.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgVl2ObNzEurEBObVmYpPv7sNzfu-9jOlH_Jld8TABnwVIhjpVyRpBZ7k6iwGmHMW-3z6BsVNscPJCt_MrqkIgd4VT3RRimTCNr2SoHUqvtUS28KYhsy9dniK6nYygxJFDW2oD6AjIs7OY/s72-c/IMGS5175.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2016/07/kiwanda-cha-nondo-kuiingizia-serikali.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/07/kiwanda-cha-nondo-kuiingizia-serikali.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy