MAZISHI YA MWANAMUZIKI MKONGWE, MAREHEMU SHEM IBRAHIM KARENGA KATIKA MAKABURI YA KISUTU JIJINI DAR LEO

Baadhi ya wadau wa muziki wakiwa wamebeba jeneza lililokuwa na mwili wa mwanamuziki mkongwe wa bendi ya Tabora Jazz, marehem...




Baadhi ya wadau wa muziki wakiwa wamebeba jeneza lililokuwa na mwili wa mwanamuziki mkongwe wa bendi ya Tabora Jazz, marehemu Shem Karenga wakati wa maziko yake kwenye makaburi ya Kisutu, jijini Dar es Salaam leo alasiri.



(Chini na juu) Ni taswira mbalimbali za wanamuziki, marafiki ndugu na jamaa waliojitokeza kumzika gwiji huyo wa muziki aliyezikwa leo jijini Dar es Salaam.


Ankali Michuzi alipokutana na mdau Ali Choki kwenye maziko hayo.




























(Picha kwa hisani ya Globu ya Jamii )
***************


THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
Website : www.ikulu.go.tz              

Fax: 255-22-2113425                                      


Coat of Arms
PRESIDENT’S OFFICE,
      STATE HOUSE,
              1 BARACK OBAMA ROAD,  
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia salamu za rambirambi Waziri wa Habari, Vijana Utamaduni na Michezo, Mheshimiwa Dkt. Fenella Mukangara kuomboleza kifo cha mwanamuziki mkongwe, Shem Ibrahim Karenga kilichotokea tarehe 15 Desemba, 2014 katika Hospitali ya Amana jijini Dar es Salaam alikokuwa amepelekwa kwa matibabu ya ugonjwa wa shinikizo la damu.
Enzi za uhai wake, Marehemu Karenga alijaaliwa kipaji cha muziki hususan upigaji wa gitaa la solo na uimbaji, kipaji ambacho kilimwezesha kufanya kazi katika bendi mbalimbali za muziki hapa nchini akianzia na Bendi ya Lake Tanganyika Jazz mwaka 1964, na baadaye Bendi Maarufu ya Tabora Jazz ikijulikana zaidi kama Wana Segere Matata.
 “Nimeshtushwa, nimesikitishwa na kuhuzunishwa sana kutokana na taarifa za kifo cha Mwanamuziki huyu Mkongwe na Mahiri ambaye, kupitia kipaji alichojaaliwa na Mwenyezi Mungu, alitoa mchango mkubwa katika kuiletea sifa nchi yetu”, amesema Rais Kikwete katika Salamu zake za Rambirambi.
 “Kutokana na msiba huu mkubwa, pokea salamu zangu za rambirambi kutoka dhati ya moyo wangu kwa kumpoteza mmoja wa Wasanii Mahiri katika Taifa letu, na kupitia kwako naomba salamu zangu ziwafikie wasanii kote nchini kwa kumpoteza mwenzao”, ameongeza kusema Rais Kikwete akiomboleza msiba huo.
Rais Kikwete ametoa salamu za pole kwa familia ya marehemu Karenga kwa kupoteza kiongozi na mhimili wa familia. Amewaomba wanafamilia wawe wavumilivu na watulivu wakati huu wanapopitia kipindi hiki kigumu cha kuondokewa na mpendwa wao, na anamuomba Mola aipokee na aiweke mahala pema peponi roho ya Marehemu Shem Ibrahim Karenga, Amina.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu – Dar es Salaam.
16 Desemba,2014
 

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: MAZISHI YA MWANAMUZIKI MKONGWE, MAREHEMU SHEM IBRAHIM KARENGA KATIKA MAKABURI YA KISUTU JIJINI DAR LEO
MAZISHI YA MWANAMUZIKI MKONGWE, MAREHEMU SHEM IBRAHIM KARENGA KATIKA MAKABURI YA KISUTU JIJINI DAR LEO
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiqOdaiwpbjmV88Gs_jPFsnDRPhYDknDA97834XE2Tkotz5sK_Ggtr_GgLM1G2FoofMjOVQJSFW0w9B2y9KjyXVAsdRUA31sDc9u1Xq9AqwtSFAOCFC0WTUPgtNKyfxfXvAOqMz-_AH2kPB/s1600/DSC_0807.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiqOdaiwpbjmV88Gs_jPFsnDRPhYDknDA97834XE2Tkotz5sK_Ggtr_GgLM1G2FoofMjOVQJSFW0w9B2y9KjyXVAsdRUA31sDc9u1Xq9AqwtSFAOCFC0WTUPgtNKyfxfXvAOqMz-_AH2kPB/s72-c/DSC_0807.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2014/12/mazishi-ya-mwanamuziki-mkongwe-marehemu.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2014/12/mazishi-ya-mwanamuziki-mkongwe-marehemu.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy