RAIS MSTAAFU BENJAMIN MKAPA APONGEZWA WAKATI WA JUBILEE YAKE YA MIAKA 75 JANA

Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa, akizima mishumaa. Kulia ni Mkewe Mama Anna na wajukuu wao.   Rais mstaafu wa Awamu ya Tatu Benjamin M...

Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa, akizima mishumaa. Kulia ni Mkewe Mama Anna na wajukuu wao.
 
Rais mstaafu wa Awamu ya Tatu Benjamin Mkapa na mke wake Mama Anna wakipokewa na wasimaizi wa kanisa Katoliki la Parokia ya Immaculate Upanga Dar es Salaam kwa ibada walipowasili kwa ibada ya misa maalum ya shukrani katika kuadhimisha jubilee ya miaka 75 ya kuzaliwa kwake Novemba 12 2013. (Picha na Mpigapicha Wetu)
Baadhi ya maaskofu wa Kanisa hilo kutoka majimbo mbalimbali wakiwa kwenye ibada hiyo.



Rais mstaafu Benjamin Mkapa akibadilishana mawazo na Mwenyekiti wa chama Cha NCCRA-Mageuzi, Pia Mbunge wa Kuteuliwa kabla ya kuanza kwa ibada hiyo.



Maaskofu wakiwa katika maadamano pia kuelekea kanisani.

MTAZIMO WA NDANI WAKATI WA IBADA.

Kumbukumbu ya pamoja na wanakwaya.

Kumbukumbu ya pamoja na wanakwaya wengine.


Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT), Dk Alex Malasusa akiribishwa na mmoja wa wasimamizi wa kanisa baada ya kuwasili kushiriki ibada hiyo.





Picha ya pamoja na mapadri. Wa tatu (kushoto) ni Waziri Mkuu wa mstaafu, David Cleopa Msuya.


Rais mstaafu wa Awamu ya tatu Benjamin Mkapa na mke wake Mama Anna wakielekea kwenye  maadamano kuingia kanisani. 

Rais mstaafu Benjamin Mkapa na Mkewe Mama Anna, Mkuu wa Kanisa Katoliki Nchini, Muadhama Polycarp Cardinal Pengo (mwenye fimbo) pamoja na Balozi wa Vatican Tanzania, Askofu Mkuu, Francisco Montecillo Paddila wakiwa katika picha ya pamoja na maaskofu mbalimbali baada ya ibada hiyo. Pamoja nao ni Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana Nchini, Dk Valentino Mokiwa (wa kwanza kushoto aliyesimam), Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT), Dk Alex Malasusa (wa pili kushoto aliyesimama) na Oscar Mnung’a (wa tatu kushoto aliyesimama).



Rais Mstaafu Benjamin Mkapa na Mke wake Mama Anna wakikabidhi vipaji vya ibada hiyo kwa Mkuu wa Kanisa Katoliki Nchini Muadhama Polycarp Cardinal Pengo. Pamoja nao ni Kijana wao, Steven na wajukuu, Benedict na Nathaniel. 


Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT), Dk Alex Malasusa wakati wa utambulisho.






Rais Mstaafu Benjamin Mkapa na Mke wake Mama Anna wakikabidhi vipaji vya ibada hiyo kwa Mkuu wa Kanisa Katoliki Nchini Muadhama Polycarp Cardinal Pengo. Pamoja nao ni Kijana wao, Steven na wajukuu, Benedict na Nathaniel. 

Mke wake Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, Mama Anna pamoja watoto na wajukuu wao, Benedict na Nathaniel.

Pamoja na wasimamizi wa kanisa.



Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa jana aliadhimisha miaka 75 ya kuzaliwa kwake kwa kufanya Ibada ya Misa iliyoongozwa na Mkuu wa Kanisa Katoliki Nchini, Muhadhama Polycarp Kadinali Pengo. 

Katika ibada hiyo ya shukrani iliyofanyika Kanisa Katoliki la Immakulata, Upanga jijini Dar es Salaam, Mkapa aliwataka Watanzania kumshukuru Mungu kwa kila jambo.

“Tunamshukuru Mungu kwa majaliwa aliyoipatia nchi yetu ya Tanzania na tunamwomba azidi kuijalia umoja katika yote tunayofanya na tunayokusudia kuyafanya,” alisema Mkapa.

Mkapa pia aliwashukuru waumini wenzake katika kanisa hilo, huku akifichua siri kwamba, Kadinali Pengo alimtaka ahamie Kanisa la Mtakatifu Joseph wakati alipokuwa rais, lakini hakukubali.

Kwa upande wake, Kardinali Pengo aliwataka Watanzania kuwa na tabia ya kumshukuru Mungu kwa kila jambo.

“Alichofanya Rais Mstaafu Mkapa ni cha kuigwa. Tunatakiwa kutambua kuwa hatuishi kwa nguvu zetu bali kwa uwezo wa Mungu hivyo ni lazima tumshukuru kama alivyofanya mwenzetu,” alisema Kardinali Pengo.

Baadhi ya viongozi waliohudhuria ibada hiyo ni pamoja na Mawaziri Wakuu Wastaafu, Edward Lowassa na Cleopa Msuya, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu wa Bunge), William Lukuvi, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Utawala Bora na Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia.

Wengine ni Mawaziri wa zamani, Sir George Kahama, Bazili Mramba, Profesa Philemon Sarungi, Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk Alex Malasusa, Mkuu wa Kanisa la Anglikana Nchini, Dk Valentino Mokiwa, Askofu wa Mtwara, Oscar Mnung'a pamoja wakuu wa zamani wa Majeshi, Majenerali, Robert Mboma na George Waitara.

SHEREHE YA MIAKA 75 YA RAIS MSTAAFU, BENJAMIN MKAPA, 'HAPPY BIRTHDAY BEN'

Mandhari ya ukumbi uliofanyika sherehe ya kumpongeza Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa ya kutimiza miaka 75, iliyofanyika kwenye ukumbi wa Msimbazi Center Dar es Salaam, jana usiku.
Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa, akijumuika na mkewe Mama Anna Mkapa na wana familia yake kukata keki, ikiwa ni ishara ya kupongezwa kwa kutimiza miaka 75.
 Shamra shamra ukumbini wakati wa sherehe hiyo.

Baadhi ya wageni waalikwa, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Mohammed Gharib Bilal, Mama Asha Bilal, (kushoto) Mama Zakhia Bilal na baadhi ya viongozi, wakijumuika kumpongeza Mkapa.
 Zawadi ya Benjamin kutoka kwa marafiki zake wakaribu.
 Baadhi ya wageni waalikwa pamoja na mawaziri wastaafu na viongozi wa serikali.
 Wageni waalikwa.
 wageni waalikwa.
 Msanii akitoa burudani.
Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa, akilishwa keki na mkewe Mama Anna Mkapa.
  Wakati wa sala katika hafla hiyo.
 Baadhi ya wageni maarufu wakiwa katika sherehe hiyo. Kulia ni Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa na Mkewe Regina, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa mstaafu, Dk Salim Ahmed Salim na Mkwewe na Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana. 
 Mkapa na keki yake.
 
  Ben Mkapa akipongezwa na mke wa Rais, Mama Salma.
  WAGENI MAARUFU KATIKA SHEREHE HIYO.
 Makamu wa Rais pamoja na wake zake (kulia na kushoto kwake) wakijiandaa kugonganisha glass na Waziri Mkuu mstaafu David Cleopa Msuya (kulia), Rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi na mkewe Mama Siti wakati wa sherehe hiyo.
 Zawadi.......akikabidhiwa mkapa.
 Rais Mstaafu Mkapa, akizungumza wakati wa sherehe hiyo.
 Makamu wa Rais Dk Bilal, akizungumza kwa niaba ya Serikali.
 Makamu wa Rais Dk Bilal. akimpongeza Mkapa.
Picha ya pamoja


COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: RAIS MSTAAFU BENJAMIN MKAPA APONGEZWA WAKATI WA JUBILEE YAKE YA MIAKA 75 JANA
RAIS MSTAAFU BENJAMIN MKAPA APONGEZWA WAKATI WA JUBILEE YAKE YA MIAKA 75 JANA
http://3.bp.blogspot.com/-NYlBhEnCBh8/UoMUmfOG--I/AAAAAAAA6yQ/RIG5eiXoOGs/s640/02.jpg
http://3.bp.blogspot.com/-NYlBhEnCBh8/UoMUmfOG--I/AAAAAAAA6yQ/RIG5eiXoOGs/s72-c/02.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2013/11/benjamin-mkapa-apongezwa-wakati-wa.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2013/11/benjamin-mkapa-apongezwa-wakati-wa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy