RAIS MHE. DKT. MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA WAGENI KUTOKA UMOJA NA AFRIKA (AU) NA MISRI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM
HomeJamii

RAIS MHE. DKT. MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA WAGENI KUTOKA UMOJA NA AFRIKA (AU) NA MISRI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Simu: 255-22-2114512, 2116898 E-mail: press@ikulu....

SSRA NA NIDA WANAENDELE NA ZOEZI LA UANDIKISHAJI WA VITAMBULISHO VYA TAIFA KWA WANACHAMA WA MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII
DK. KIGWANGALLA AFANYA MAZUNGUMZO NA MUWAKILISHI WA BENKI YA DUNIA NCHINI KWA AJILI YA KUBORESHA MRADI WA REGROW
RAIS MTEULE WA ROTARY INTERNATIONAL AWASILI NCHINI TANZANIA
KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU




JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
Simu: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: press@ikulu.go.tz
Tovuti : www.ikulu.go.tz               

Faksi: 255-22-2113425


OFISI YA RAIS,
     IKULU,
1 BARABARA YA BARACK OBAMA,   
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 20 Aprili, 2018 amefanya mazungumzo na Kamishna wa amani na usalama wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika Mhe. Balozi Smail Chergui ambaye amewasilisha ujumbe wa Mwenyekiti wa Kamisheni hiyo Mhe. Moussa Faki Mahamat.
Mhe. Chergui amesema katika mazungumzo yake na Mhe. Rais Magufuli yaliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, wamejadili kuhusu masuala yahusuyo amani na usalama barani Afrika hususani ukanda wa maziwa makuu pamoja na masuala ya wakimbizi.
Mhe. Chergui amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa ushauri wake na mchango wake wa mawazo na uzoefu, wenye lengo la kuimarisha amani na usalama.
Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amekutana na Msaidizi wa Rais wa Misri na Waziri Mkuu Mstaafu wa Misri Mhe. Ibrahim Roshdy Mahlab ambaye amewasilisha ujumbe kutoka kwa Rais wa Misri Mhe. Abdel Fattah el-Sisi.
Baada ya mazungumzo hayo Mhe. Mahlab amesema katika mazungumzo yake na Mhe. Rais Magufuli wamejadili namna ya kuimarisha zaidi uhusiano na ushirikiano kati ya Tanzania na Misri, hasa ikizingatiwa kuwa zipo fursa nyingi ambazo nchi hizi mbili marafiki zinapaswa kuzifanyia kazi.
Mhe. Mahlab amebainisha kuwa utekelezaji wa makubaliano yaliyowekwa wakati wa ziara ya Rais wa Misri Mhe. Abdel Fattah el-Sisi hapa nchini umeanza ambapo tume ya pamoja ya ushirikiano kati ya nchi hizi imeshakutana  nchi Misri na kuainisha maeneo yenye fursa na yanayopaswa kufanyiwa kazi.


Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
20 Aprili, 2018




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Kamishna wa Amani na Usalama wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika Balozi Smail Chergui Ikulu jijini Dar es Salaam.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na Kamishna wa Amani na Usalama wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika Balozi Smail Chergui Ikulu jijini Dar es Salaam.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Kamishna wa Amani na Usalama wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika Balozi Smail Chergui Ikulu jijini Dar es Salaam.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Waziri Mkuu Mstaafu wa Misri ambaye kwasasa ni Mshauri wa Rais wa Misri Injinia Ibrahim Mahlab kabla ya kuanza mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Waziri Mkuu Mstaafu wa Misri ambaye kwasasa ni Mshauri wa Rais wa Misri Injinia Ibrahim Mahlab kabla ya kuanza mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Waziri Mkuu Mstaafu wa Misri ambaye kwa sasa ni Mshauri wa Rais wa Misri Injinia Ibrahim Mahlab mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam.




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na Waziri Mkuu Mstaafu wa Misri ambaye kwasasa ni Mshauri wa Rais wa Misri Injinia Ibrahim Mahlab Ikulu jijini Dar es Salaam. (PICHA NA IKULU)



Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: RAIS MHE. DKT. MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA WAGENI KUTOKA UMOJA NA AFRIKA (AU) NA MISRI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM
RAIS MHE. DKT. MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA WAGENI KUTOKA UMOJA NA AFRIKA (AU) NA MISRI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM
https://lh3.googleusercontent.com/0gsGOZ_bR2IqPBQR01WS0BYdYYqJU3toWT8YuMXZDFaTyO0I8fvia_OynzuV2Y_AUs-XpohsUZ29lflCPBnbw33FP2cNb-tWKOyoEBt7C8uebFSVTiTbrCru-eAaRCp7cf2_3KR2L0msajuEpQ
https://lh3.googleusercontent.com/0gsGOZ_bR2IqPBQR01WS0BYdYYqJU3toWT8YuMXZDFaTyO0I8fvia_OynzuV2Y_AUs-XpohsUZ29lflCPBnbw33FP2cNb-tWKOyoEBt7C8uebFSVTiTbrCru-eAaRCp7cf2_3KR2L0msajuEpQ=s72-c
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2018/04/rais-mhe-dkt-magufuli-akutana-na.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2018/04/rais-mhe-dkt-magufuli-akutana-na.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy