PUMA YAZINDUA MPANGO WA MAFUNZO YA USALAMA BARABARANI KWA WANAFUNZI
HomeJamii

PUMA YAZINDUA MPANGO WA MAFUNZO YA USALAMA BARABARANI KWA WANAFUNZI

  Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Mbande, Dar es Salaam, Nasri Mustafa akumuonesha  Meneja Mkuu wa Puma Energy Tanzania, Philipp...

HUAWEI YAENDELEA KUCHANGIA SEKTA YA ELIMU KUPITIA PROGRAMU YA ‘SEEDS FOR THE FUTURE’
RC MAKONDA ATEMBELEA WODI MPYA YA KINA MAMA HOSPITALI YA AMANA JIJINI DAR ES SALAAM
TANZANIA YAJIPANGA KUISHAWISHI UINGEREZA, FURSA ZA UWEKEZAJI NISHATI, MADINI NCHINI;






 Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Mbande, Dar es Salaam, Nasri Mustafa akumuonesha Meneja Mkuu wa Puma Energy Tanzania, Philippe Corsaletti (kulia) picha aliyoichora na kushinda tuzo  ya usalama barabarani 2017, wakati wa uzinduzi wa mpango wa Puma wa  mafunzo ya ya usalama barabarani kwa wanafunzi, jana katika Makao Makuu ya Puma, Dar es Salaam. Wa pili kulia ni Matibu Mbunja aliyemwakilisha Kamanda wa Kikosi cha Poilisi cha  Usalama Barabarani Tanzania.Wa pili kushoto ni SajentiHussein Ramadhan Mwalimu wa Trafiki Makao Makao Makuu ya Usalama Barabarani.Imeandaliwa na Richard Mwaikenda.


Na Mwandishi Wetu


KAMPUNI ya Puma Energy Tanzania imezindua kampeni maalumu ya mafunzo ya usalama barabarani kwa wanafunzi wa shule za msingi kwa lengo la kueneza elimu hiyo kuanzia ngazi ya chini. 


Kampeni hiyo inayokwenda sambamba na mashindano ya uchoraji michoro ya usalama barabarani imezinduliwa Dar es Salaam jana na ofisa wa Polisi, ASP Mbuya Matibu, kutoka Makao Makuu ya Kikosi cha Usala,ma Barabarani.


AKizungumza kwenye uzinduzi wa kampeni hiyo, ASP Matibu,  alisema Puma Energy Tanzania, wana mchango mkubwa katika utoaji elimu ya usalama barabarani, hivyo kuwataka wadau wengine kuiga mfano huo.


Pia, aliwataka madereva nchini wasiendeshe magari kwa kukariri sheria,  bali wazitambue ili waweze kuzitumia vizuri kupunguza ajali.


Kwa upande wake Meneja Mkuu wa Puma Energy Tanzania, Philippe Corsaletti, alisema elimu ya usalama kwa wanafunzi ni muhimu, kwani inawapa uelewa wa matumizi ya barabara kwa usalama.


"Tunawaangalia sana watoto wa shule za msingi kwani wao wanakabiliwa na hatari nyingi za barabarani," alisema Corsaletti na kuongeza;


"Hivyo kwa kuwafundisha usalama barabarani tunawapa ufahamu wa kuwajenga katika matumizi salama ya barabara...hiki ndicho kipaumbele chetu."


Alifafanua kwamba baada ya mafunzo  wanafunzi wanapewa nafasi ya kuchora michoro ya usalama barabarani na mshindi pamoja na shule anayotoka wanazawadiwa.


Corsaletti alisema kampuni hiyo ilianzisha mafunzo hayo mwaka 2013 na imeendelea kufanya hivyo hadi sasa kwa kufikia shule 47 na kuwafundisha wanafunzi 60,000 kutoka mikoa ya Dar es Salaam, Arusha, Kilimanjaro na Geita.


Aliongeza kuwa uchunguzi uliofanywa umeonesha kuwa kiwango cha ajali katika shule zilizopatiwa mafunzo kimepungua.




Corsaletti, alisema kampuni hiyo itaendelea na kampeni ya usalama barabarani na kuahidi kufanyakazi pamoja na Kikosi cha Usalama Barabarani, maofisa kutoka manispaa au wilaya zinakotoka shule  zilizochaguliwa ili kuhakikisha lengo linatimia.





 Meneja Mkuu wa Puma Energy Tanzania, Philippe Corsaletti (kulia), akimshukuru Mbunja kwa kuzindua mpango huo.

 Matibu Mbunja aliyemwakilisha Kamanda wa Kikosi cha Poilisi cha  Usalama Barabarani Tanzania, akihutubia wakati wa uzinduzi wa mpango huo.







Meneja Rasilimali Watu wa Puma Tanzania Bi Loveness Hoyange  akiiweka sawa picha iliyochorwa na Mwanafunzi Nasri Mustafa na kushinda tuzo ya Usalama barabarani 2027

 Shemu ya wadau wa usalama barabarani

 Baadhi ya walimu na wanafunzi waliohudhuria uzinduzi huo

 Wanahabari wakiwa kazini

 Sehemu ya wadau wa usalama barabarani

 Mwanafunzi Nasri Mustafa akionesha picha aliyoichora ya usalama barabarani. Picha hiyo ilishinda tuzo ya kwanza 2017



 Wadau wa usalama barabrani wakisikiliza kwa makini wakati wa uzinduzi a mpango huo

 Mgeni rasmi, Mbunja na Meneja Mkuu wa Puma,Corsaletti wakiwa na furaha

  Meneja Mkuu wa Puma,Corsaletti, Akisalimiana na wadau baada ya uzinduzi

 Wakiwa katika picha ya pamoja




Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: PUMA YAZINDUA MPANGO WA MAFUNZO YA USALAMA BARABARANI KWA WANAFUNZI
PUMA YAZINDUA MPANGO WA MAFUNZO YA USALAMA BARABARANI KWA WANAFUNZI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiP_7tA7M1Y6dOGPBaKSha3wY9vMtmTp9pmLrmVTTjSvDoCnqHpW5-JZqMZUbgtrFs0srILtVIAIzsaZewjkVzo1l08SpHlKQYOFuNFZDiGi5RdzNMX9Iymze7Rd_pv2OKYLvJ6hY90GKd5/s640/01.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiP_7tA7M1Y6dOGPBaKSha3wY9vMtmTp9pmLrmVTTjSvDoCnqHpW5-JZqMZUbgtrFs0srILtVIAIzsaZewjkVzo1l08SpHlKQYOFuNFZDiGi5RdzNMX9Iymze7Rd_pv2OKYLvJ6hY90GKd5/s72-c/01.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2018/04/puma-yazindua-mpango-wa-mafunzo-ya.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2018/04/puma-yazindua-mpango-wa-mafunzo-ya.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy