KAMANDA WA POLISI TANGA AZUNGUMZIA BASI SIMBA COACH KUCHOMWA MOTO
HomeMikoani

KAMANDA WA POLISI TANGA AZUNGUMZIA BASI SIMBA COACH KUCHOMWA MOTO

Na Said Mwishehe, Globu ya Jamii JESHI la Polisi Mkoa wa Tanga limetoa ufafanuzi kuhusu tukio la kuchomwa moto kwa basi la Simba Coac...


Na Said Mwishehe, Globu ya Jamii

JESHI la Polisi Mkoa wa Tanga limetoa ufafanuzi kuhusu tukio la kuchomwa moto kwa basi la Simba Coach. 

Kwa mujibu wa taarifa zinaeleza basi hilo limechomwa leo na wananchi wenye hasira kali baada ya dereva wake kumgonga dereva wa bodaboda. 

Akizungumza na Michuzi Globu kwa njia ya simu muda huu, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga Edward Bukombe amefafanua ni kweli amesikia taarifa za kuchomwa moto basi hilo lakini halijachomwa mkoani Tanga kama inavyoelezwa na baadhi ya watu.

Amesema baada ya kuona taarifa za kuchomwa basi la Simba Coach waliamua kufuatilia lakini wamejiridhisha haikutokea kwenye mkoa wao ila basi hilo limechomwa nchini Kenya.

Kamanda Bukombe ameiambia Michuzi Globu kuwa basi hiyo ilikuwa inatoka Mombasa nchini Kenya na taarifa walizonazo limechomwa huko huko nchini Kenya kwani lilikuwa halijaingia kwenye mipaka ya nchi yetu ya Tanzania na hasa mkoani Tanga. 

Alipoulizwa iwapo anafahamu namba za basi hilo linalodaiwa kuchomwa moto na dereva aliyekuwa analiendesha ,amejibu wanaendelea kufuatilia kwa polisi wa nchini Kenya na kisha atatoa taarifa kuufahamisha umma. 

"Tunaendelea kukusanya taarifa na kwa kuwa limechomwa huko Kenya tunawasiliana na polisi wa huko ili tuwe na uhakika wa taarifa Kamili za tukio hilo.Hatujapata namba za basi.Wananchi wasubiri tutaeleza kwa usahihi tutakapokamilisha kupata ukweli zinazohusu tukio hilo, "amesema Kamanda Bukombe.

TAARIFA KUCHOMWA MOTO SIMBA MTOTO

Mapema asubuhi ya leo katika mitandao ya kijamii zilianza kuzagaa picha zinazoesha basi linaungua moto, na vyanzo vya moto huo ikawa inaelezwa ni wananchi wenye hasira wamechoma moto basi la Simba Coach. 

Taarifa hizo zikawa zinadai tukio hilo limetokea Mkoa wa Tanga lakini haikuwa inaonesha ni wananchi wa eneo gani walioamua kuchoma basi hilo.

Pia taarifa hiyo imedai basi limochomwa moto kutokana na dereva wake kugonga dereva wa pikipiki na hivyo wananchi wakaonesha hasira zao kwa kulichoma moto basi hilo. 






Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: KAMANDA WA POLISI TANGA AZUNGUMZIA BASI SIMBA COACH KUCHOMWA MOTO
KAMANDA WA POLISI TANGA AZUNGUMZIA BASI SIMBA COACH KUCHOMWA MOTO
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjcuxqHo7NdMC9XSq8HurJdwYkqR-SmHxYYZtGI7iO8pdPxffmGtTss5lvzRbaBxFsiJa6eRAkB5qhYHVlGDArgBcbzjMHouZhd9jSM8MJkKtHXFaxr1ra3dqdoZ4tMiEvf4p1G4JSSj-e-/s640/qq.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjcuxqHo7NdMC9XSq8HurJdwYkqR-SmHxYYZtGI7iO8pdPxffmGtTss5lvzRbaBxFsiJa6eRAkB5qhYHVlGDArgBcbzjMHouZhd9jSM8MJkKtHXFaxr1ra3dqdoZ4tMiEvf4p1G4JSSj-e-/s72-c/qq.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2018/01/kamanda-wa-polisi-tanga-azungumzia-basi.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2018/01/kamanda-wa-polisi-tanga-azungumzia-basi.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy