NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII, JAPHET HASUNGA ATEMBELEA HIFADHI YA TAIFA YA KITULO, MAARUFU KAMA BUSTANI YA MUNGU
HomeJamii

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII, JAPHET HASUNGA ATEMBELEA HIFADHI YA TAIFA YA KITULO, MAARUFU KAMA BUSTANI YA MUNGU

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Makete, Veronika Kessy wakiangalia maua ya asili amb...

TANZANIA YATILIANA SAINI NA MFUKO WA MAENDELEO KIUCHUMI WA KUWAIT
KITABU CHA UWIANO WA TAKWIMU ZA WANAWAKE NA WANAUME CHAZINDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM
RAIS WA BENKI YA DUNIA AONDOKA NCHINI BAADA YA ZIARA YAKE YA KIKAZI YA SIKU TATU

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Makete, Veronika Kessy wakiangalia maua ya asili ambayo ni kivutio kikubwa cha utalii katika hifadhi ya Taifa ya Kitulo wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua shughuli za uhifadhi na utalii katika hifadhi hiyo kwenye wilaya ya Makete mkoani Njombe leo. Hifadhi hiyo ni maarufu duniani kwa kuwa na aina za maua zaidi ya 35 ya asili ambayo hayapatikani kwengineko duniani. Hifadhi hiyo ni maarufu kwa wenyeji kama 'BUSTANI YA MUNGU'.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (kushoto), Mkuu wa Wilaya ya Makete, Veronika Kessy (kulia) na baadhi ya viongozi wa Hifadhi ya Taifa ya Kitulo wakiangalia maua ya asili ambayo ni kivutio kikubwa cha utalii katika hifadhi hiyo wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua shughuli za uhifadhi na utalii katika hifadhi hiyo kwenye wilaya ya Makete mkoani Njombe leo. Hifadhi hiyo ni maarufu duniani kwa kuwa na aina za maua zaidi ya 35 ya asili ambayo hayapatikani kwengineko duniani. 
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (wa nne kulia), akiwa kwenye picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Makete, Veronika Kessy (wa tatu kulia) na baadhi ya viongozi wa Hifadhi ya Taifa ya Kitulo wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua shughuli za uhifadhi na utalii katika hifadhi hiyo kwenye wilaya ya Makete mkoani Njombe leo. Hifadhi hiyo ni maarufu duniani kwa kuwa na aina za maua zaidi ya 35 ya asili ambayo hayapatikani kwengineko duniani. 
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (kulia), Mkuu wa Wilaya ya Makete, Veronika Kessy na Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Kitulo, Pius Mzimbe wakiangalia maporomoko ya maji ya Mwakipembo ambayo ni kivutio cha utalii ndani ya hifadhi ya Kitulo wakati wa ziara ya kikazi ya kukagua shughuli za uhifadhi na utalii katika hifadhi hiyo kwenye wilaya ya Makete mkoani Njombe leo. Pamoja na kivutio hicho hifadhi hiyo ni maarufu duniani kwa kuwa na aina za maua zaidi ya 35 ya asili ambayo hayapatikani kwengineko duniani. Hifadhi hiyo ni maarufu kwa wenyeji kama 'BUSTANI YA MUNGU'.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (kulia) akipata maelezo kuhusu maporomoko ya maji ya Mwakipembo ambayo ni kivutio cha utalii ndani ya hifadhi ya Taifa ya Kitulo kutoka kwa Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi hiyo, Pius Mzimbe wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua shughuli za uhifadhi na utalii katika hifadhi hiyo kwenye wilaya ya Makete mkoani Njombe leo. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Makete, Veronika Kessy. Pamoja na kivutio hicho hifadhi hiyo ni maarufu duniani kwa kuwa na aina za maua zaidi ya 35 ya asili ambayo hayapatikani kwengineko duniani.
Muonekano mwanana wa Hifadhi ya Taifa ya Kitulo. Hifadhi hii ina aina zaidi ya 350 za maua huku aina 35 yakiwa ndwele na hupatikana katika hifadhi hiyo pekee duniani. Vivutio vingine vinavyopatikana katika hifadhi hiyo ni Maporomoko ya maji, ndege aina mbalimbali ambao wengine huama kutoka ulaya wakati wa baridi, wanyamapori aina Swala, Mbega na Nsya. Hata hivyo katika kutimiza mkakati wa Wizara kuboresha vivutio vya utalii, hifadhi hiyo ipo katika maandalizi ya kuanzisha makazi ya Pundamilia na wanyama wengine. Awamu ya kwanza ya kuhamisha pundamiliz 25 kutoka hifadhi ya taifa ya mikumi inatarajiwa kukamilika mwishoni mw mwaka huu. Hifadhi hiyo ni maarufu kwa wenyeji kama 'BUSTANI YA MUNGU'.
Aina mojawapo ya ua ambalo hupatikana katika hifadhi hiyo.
Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Kitulo, Pius Mzimbe (kushoto) akimuonyesha Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kulia) sehemu ya eneo lililochaguliwa ndani ya hifadhi hiyo kwa ajili ya kuanzisha makazi ya Pundamilia 25 watakaohamishwa kutoka Hifadhi ya Taifa ya Mikumi. Alisema kabla ya mwaka huu kuisha Pundamilia hao watakuwa wameshahamishiwa eneo hilo. Huo ni mkakati wa wizara na Serikali katika kuboresha vivutio vya utalii nchini ili kuongeza idadi ya watalii na mapato.
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga akisalimiana na wafanyakazi wa Hifadhi ya Taifa ya Kitulo alipowasili makao makuu ya hifadhi hiyo yaliyopo Makete mkoani Njombe jana.
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga akizungumza na wafanyakazi wa Hifadhi ya Taifa ya Kitulo makao makuu ya hifadhi hiyo yaliyopo Makete mkoani Njombe. Amewaaka watumishi hao kufanya kazi kwa bidii na ubunifu, kujiepusha na vitendo vya rusha, kuweka mikakati wa kudhibiti mifugo kuingia hifadhini na sio kusubiri iingie na kuanza kutangaza kuikamata au kuitaifisha, kupunguza malalamiko ya wananchi jirani na hifadhi hiyo, kuongeza idadi ya mapato ya hifadhi na kufanya kazi kwa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga akizungumza na wafanyakazi wa Hifadhi ya Taifa ya Kitulo. (Picha na Hamza Temba-Wizara ya Maliasili na Utalii)
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII, JAPHET HASUNGA ATEMBELEA HIFADHI YA TAIFA YA KITULO, MAARUFU KAMA BUSTANI YA MUNGU
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII, JAPHET HASUNGA ATEMBELEA HIFADHI YA TAIFA YA KITULO, MAARUFU KAMA BUSTANI YA MUNGU
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhjfxJyyv8gW9IEi4DOLFNSJQN1Ch6pxKjmRMZcopOk3mGy7qri7GBVdZYpsbeQJ65gvOmUbNrWeRcqKOYnhh6vNowYHCB_MiBiychvmtALqM5LLo7Xb8Xnj5haxryySmwRtSOrdoHs3EvH/s640/_DSC0165.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhjfxJyyv8gW9IEi4DOLFNSJQN1Ch6pxKjmRMZcopOk3mGy7qri7GBVdZYpsbeQJ65gvOmUbNrWeRcqKOYnhh6vNowYHCB_MiBiychvmtALqM5LLo7Xb8Xnj5haxryySmwRtSOrdoHs3EvH/s72-c/_DSC0165.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/12/naibu-waziri-wa-maliasili-na-utalii.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/12/naibu-waziri-wa-maliasili-na-utalii.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy