NAIBU WAZIRI TAMISEMI, JOSEPH KAKUNDA AFURAHISHWA NA MIRADI YA KUWAWEZESHA WANANCHI KUKABILIANA NA ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIA NCHI

Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi),Joseph Kakunda(kushoto) akipanda ngazi kukagua mradi wa m...



Naibu
Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za
Mitaa(Tamisemi),Joseph Kakunda(kushoto) akipanda ngazi kukagua mradi wa
maji wilayani Longido,akiwa na Mkuu wa wilaya ya Longido mkoa wa
Arusha,Godfrey Chongolo.


Naibu
Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za
Mitaa(Tamisemi),Joseph Kakunda(kulia) na Mkuu wa wilaya ya Longido(wa
pili kulia) wakimsikiliza Mhandisi wa Maji wilayani Longido,Ramadhani
Musiba(kushoto) utekelezaji wa miradi ya maji.


Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za
Mitaa(Tamisemi),Joseph Kakunda akipanda ngazi kukagua mradi wa
maji kijiji cha Eworendeke Kata ya Kimokouwa wilayani Longido.


Ujumbe
wa Naibu Waziri  wa Tamisemi,Joseph Kakunda pamoja na maafisa wa
halmashauri ya wilaya ya Longodo wakikagua moja ya miradi ya kuwawezesha
wananchi kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya Tabia Nchi.


Mhe Joseph Kakunda na Mkuu wa wilaya ya Longido,Godfrey Chongolo
wakijumuika na wananchi kuimba wimbo wa kufurahia mradi wa maji.


Mhe Joseph Kakunda na Mkuu wa wilaya ya Longido,Godfrey
Chongolo wakiagana na wananchi wa Kijiji cha Ranchi.

Na Mwandishi Wetu,Arusha

Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za
Mikoa na Serikali za
Mitaa(Tamisemi),Joseph Kakunda amepongeza ujenzi wa miradi ya maji
inayotekelezwa katika mpango wa kukabiliana na athari za mabadiliko ya
Tabia Nchi katika wilaya za Longido,Monduli na Ngorongoro.




Mradi huo unaosimamiwa kwa pamoja na
Ofisi ya Rais-Tamisemi,taasisi ya kimataifa ya maendeleo na
mazingira(IIED) na Haki Kazi Catalyst unatarajiwa kuwanufaisha wananchi
walio katika wilaya hizo tatu.



Akiwa katika Kijiji cha Eworendeke
Kata ya Kimokouwa alipongeza hatua iliyofikiwa ya kuwawezesha wananchi
kupata maji safi kwaajili ya matumizi ya nyumbani pamoja na mifugo yao
ikizingatiwa wilaya ya Longido asilimia 95 ya wakazi wake ni wafugaji.



Amesema
mkandarasi amekua mzalendo kwa kujenga miundombinu ya maji tenki pamoja
eneo la kunyweshea mifugo kwa thamani ya Sh 36 milioni na kuonya
wakandarasi wasio na uzalendo wanatekeleza miradi kwa gharama kubwa
lakini inakua haina ufanisi.



Mkuu wa
wilaya ya Longido,Godfrey Chongolo amesema wilaya yake ipo jumla ya
miradi 14 inayofadhiliwa na IIED kwa lengo la kuwawezesha wananchi
kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.



Naye
Flora Assey ambaye ni mratibu wa mradi huo kutoka Ofisi ya Mkuu wa mkoa
wa Arusha amesema lengo la mradi huo ni kuweka mfumo utakaowezesha
upimaji wa kiutendaji katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya
tabia nchi.




Imeandaliwa na mtandao wa www.rweyemamuinfo.blogspot.com

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: NAIBU WAZIRI TAMISEMI, JOSEPH KAKUNDA AFURAHISHWA NA MIRADI YA KUWAWEZESHA WANANCHI KUKABILIANA NA ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIA NCHI
NAIBU WAZIRI TAMISEMI, JOSEPH KAKUNDA AFURAHISHWA NA MIRADI YA KUWAWEZESHA WANANCHI KUKABILIANA NA ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIA NCHI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiOFTf3kykiR9lPeIbnTWshm7SKBcaJwRLqn6X472lyKjZlvjIAEhJPhqMtNKIVxtaTTxk1BfA1FidG4N0ybinV4zjZc3G5XcmwgKScOfrRaDHUSxu27FawAZtyf6Ta_owRGUVH0WrLosyn/s640/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiOFTf3kykiR9lPeIbnTWshm7SKBcaJwRLqn6X472lyKjZlvjIAEhJPhqMtNKIVxtaTTxk1BfA1FidG4N0ybinV4zjZc3G5XcmwgKScOfrRaDHUSxu27FawAZtyf6Ta_owRGUVH0WrLosyn/s72-c/1.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/12/naibu-waziri-tamisemi-joseph-kakunda.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/12/naibu-waziri-tamisemi-joseph-kakunda.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy