BOHARI YA DAWA (MSD) YAZINDUA MPANGO MKAKATI WA KATI 2017-2020
HomeJamii

BOHARI YA DAWA (MSD) YAZINDUA MPANGO MKAKATI WA KATI 2017-2020

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Mpoki Ulisubisya akihutubia wakati akizindua  Mpango M...

UNESCO KUENDELEA KUSAIDIA REDIO JAMII KUKUZA DEMOKRASIA
BOHARI YA DAWA (MSD) YAPIGA HATUA KUWEZESHA UZALISHAJI DAWA KWA NJIA YA UBIA NA SEKTA BINAFSI (PPP)
UTOAJI TAARIFA ZA MIRADI YA UJENZI WA MIUNDOMBINU YA UMMA UNAVYOSAIDIA KUPAMBANA NA RUSHWA



Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Mpoki Ulisubisya akihutubia wakati akizindua Mpango Mkakati wa Kati 2017 – 2020 wa Bohari ya Dawa (MSD) jijini Dar es Salaam leo.

Mkurugenzi Mkuu wa MSD,  Laurean Bwanakunum akizungumza katika uzinduzi huo.

Kaimu Mkurugenzi wa Fedha na Mipango wa SMD, Sako Mwakalobo, akielezea mpango huo mbele ya mgeni rasmi, Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Mpoki Ulisubisya.
Wafanyakazi wa MSD na wadau wengine wakiwa kwenye uzinduzi huo.
uzinduzi ukiendelea.
Wadau na wafanyakazi wa MSD wakiwa kwenye uzinduzi huo.

Viongozi wa idara mbalimbali wa MSD wakiwa kwenye uzinduzi huo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Mpoki Ulisubisya, akihutubia kwenye uzinduzi huo.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Mpoki Ulisubisya (wa pili kulia), Mganga Mkuu wa Serikali, Mohamed Kambi Bakari ( kulia) wakisaini hati ya mkataba maalumu wa utendaji kazi (Performance Contract) na Mkurugenzi Mkuu wa MSD,  Laurean Bwanakunu ( kulia). Wengine wanao shuhudia tukio hilo ni Mfamasia Mkuu wa Serikali, Daud Msasi na Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa MSD, Victoria Ilangwa.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Mpoki Ulisubisya, akimkabidhi hata hizo za mkataba Mkurugenzi Mkuu wa MSD Laurean Bwanakunu.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Mpoki Ulisubisya, akikata utepe kuashiria uzinduzi huo.


Na Dotto Mwaibale

BOHARI ya Dawa (MSD)imezindua Mpango Mkakati wa Kati 2017 – 2020 ili kuongeza kasi ya usambazaji wa dawa na vifaa tiba nchini. 

Akizindua mpango mkakati huo jijini Dar es Salaam leo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya ameipongeza MSD kwa kuandaa upya mpango huo ambao wamejikosoa na kuboresha maeneo muhimu ili kuendana na vipaumbele vya serikali na mahitaji ya wananchi wa Tanzania, hususan vituo vya Afya vya Umma.

Maeneo hayo muhimu ni pamoja na Kujitegemea kifedha, kuuhuisha Mnyororo wa Ugavi, Kuboresha mfumo wa Tehama, Matumizi yenye tija ya Rasilimali Watu, Utawala na 
Ushirikishwaji wadau.

Katika  hatua nyingine Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Dkt.Mpoki Ulisubisya ameingia mkataba maalumu wa utendaji kazi (Performance Contract)na Mkurugenzi Mkuu wa MSD Laurean Bwanakunu ili kuhakikisha utekelezwaji wa haraka wa Mpango mkakati uliozinduliwa.

Aidha katika uzinduzi huo Mkurugenzi Mkuu wa MSD Laurean Bwanakunu amesema atahakikisha Mpango Mkakati 2017-2020 unatekelezwa ambapo kila Mkurugenzi na Mameneja wa MSD wameingia mikataba inayopimika  ya utendaji kazi. 

Bwanakunu aliongeza kuwa ufuatiliaji wa utendaji utafanywa kupitia Ofisi  maalumu ya kusimamia utekelezaji wa mikakati ya MSD(Strategic Management Office)Tayari kila Mkurugenzi na mameneja wa MSD wamesaini mkataba kutekeleza Mpango Mkakati huo wa Kati.


(Imeandaliwa na mtandao wa habari za jamii.com-simu namba 0712727062)
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: BOHARI YA DAWA (MSD) YAZINDUA MPANGO MKAKATI WA KATI 2017-2020
BOHARI YA DAWA (MSD) YAZINDUA MPANGO MKAKATI WA KATI 2017-2020
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiJXbZVUzmPoALDH957vvLfq8KNdxMOgd_EImjJr9TIIIKo60LVDw7svI11WSJWufpz265J4HCZQx9y689a2d0mz5YVddpsW84Arroc8ouqcWo1emTYDu9NNfDcPMo5wB-kmuhoOta1t6B6/s640/1.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiJXbZVUzmPoALDH957vvLfq8KNdxMOgd_EImjJr9TIIIKo60LVDw7svI11WSJWufpz265J4HCZQx9y689a2d0mz5YVddpsW84Arroc8ouqcWo1emTYDu9NNfDcPMo5wB-kmuhoOta1t6B6/s72-c/1.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/12/bohari-ya-dawa-msd-yazindua-mpango.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/12/bohari-ya-dawa-msd-yazindua-mpango.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy