RAIS MHE. DKT. MAGUFULI AREJEA NCHINI MARA BAADA YA KUMALIZA ZIARA YAKE NCHINI UGANDA
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akipita kwenye gwaride la Kimya lililoandaliwa kwa heshma na Jeshi la Uganda mara baada ya kumaliza ziara yake ya siku tatu nchini Uganda na kurejea nchini.


HomeJamii

RAIS MHE. DKT. MAGUFULI AREJEA NCHINI MARA BAADA YA KUMALIZA ZIARA YAKE NCHINI UGANDA

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akipita kwenye gwaride la Kimya lililoandaliwa kwa heshma...

VIDEO: MAKALA FUPI YA KATIBU MKUU BI SIHABA NKINGA KATIKA MAKAZI YA WAZEE YA NJORO MOSHI NA MAGUGU BABATI
VIONGOZI WA MASHIRIKA YA UMMA NA BINAFSI WAMETAKIWA KUPIMA AFYA ZAO MARA KWA MARA – PROF MOHAMED JANABI
MANISPAA YA UBUNGO YAINGIA MIKATABA KAZI YA BILIONI NNE



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mke wake Mama Janeth Magufuli wakifurahia ngoma ya asili iliyokuwa ikipigwa na watoto wa nchini Uganda katika eneo la mpakani la Mutukula kabla ya kurejea nchini.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa mpakani Mutukula upande wa Tanzania mara baada ya kuwasili akitokea Uganda.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Mpakani mwa Tanzania na Uganda (Mutukula) kuhusu  ujenzi wa barabara ya Kutoka Miziro hadi Mutukula bila kupitia wilayani Misenyi. Pembeni yake ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akisikiliza.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Mpakani mwa Tanzania na Uganda (Mutukula) kuhusu  ujenzi wa barabara ya Kutoka Miziro hadi Mutukula bila kupitia wilayani Misenyi. Pembeni yake ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akisikiliza.






 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na viongozi wakuu wa Majeshi ya Uganda mara baada ya kumaliza ziara yake nchini Uganda.





Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia wananchi wa mpakani  Mutukula upande wa Uganda mara baada ya kumaliza ziara yake ya siku tau nchini Uganda. (PICHA NA IKULU)
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULUDescription: Description: Description: Description: Description: Coat of Arms
Simu: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: press@ikulu.go.tz
Tovuti : www.ikulu.go.tz               

Faksi: 255-22-2113425


OFISI YA RAIS,
     IKULU,
1 BARABARA YA BARACK OBAMA,   
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 11 Novemba, 2017 amemaliza ziara rasmi ya kiserikali ya siku 3 nchini Uganda na kurejea nchini Tanzania.
Mhe. Rais Magufuli ameagana na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni katika Mji wa Masaka na baadaye kusindikizwa na Makamu wa Rais wa Uganda Mhe. Edward Kiwanuka Sekandi hadi Mutukula, mpakani mwa Tanzania na Uganda.
Kabla ya kuagana na Mhe. Rais Magufuli, Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni ametoa tamko la kulaani uamuzi uliotolewa na Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai (ICC) ambayo imemuagiza mwendesha mashtaka wa mahakama hiyo kuanzisha uchunguzi dhidi ya mgogoro wa Burundi.
Majaji wa ICC wametoa uamuzi huo juzi tarehe 09 Novemba, 2017 na kumtaka mwendesha mashtaka wa mahakama hiyo kuchunguza vitendo vya kihalifu dhidi binadamu vilivyotokea nchini Burundi tangu ulipozuka mgogoro nchini humo miaka miwili iliyopita.
Katika tamko hilo Mhe. Rais Museveni ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki amesema ICC inaingilia mambo ya Jumuiya ya Afrika Mashariki bila kuwahusisha viongozi wa Jumuiya hiyo jambo ambalo sio sahihi na linarudisha nyuma juhudi za kutafuta amani ya Burundi.
Akizungumzia uamuzi huo Mhe. Rais Magufuli amesema hatua hiyo inarudisha nyuma hatua zilizochukuliwa na Jumuiya ya Afrika Mashariki ambayo iliunda Kamati ya usuluhishi wa mgogoro wa Burundi inayoongozwa na Mhe. Rais Museveni na Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu wa Tanzania Mhe. Benjamin William Mkapa.
Mhe. Rais Magufuli amesema hali ya Burundi sio mbaya kama inavyotangazwa kwa kuwa tayari wakimbizi wengi waliokuwa Tanzania wamerejea Burundi na wengine wanaendelea kurejea, na pia viongozi wanaosuluhisha mgogoro huo wamepanga kukutana tarehe 23 Novemba, 2017 kwa lengo kuendeleza mchakato wa kutatua mgogoro huo.


Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Masaka, Uganda

11 Novemba, 2017

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: RAIS MHE. DKT. MAGUFULI AREJEA NCHINI MARA BAADA YA KUMALIZA ZIARA YAKE NCHINI UGANDA
RAIS MHE. DKT. MAGUFULI AREJEA NCHINI MARA BAADA YA KUMALIZA ZIARA YAKE NCHINI UGANDA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEicxDY0wNHQ2TcwrdLTaeVZDOJrezKKU-xQ_I_dB5GFllY5z-1TPRfv6cafh_dd4gUWFGveH2Nta_ehrttpbpw-yk1T4c2-Gq-S-fUbGKXVbk1AqPQ6Bj1WYCW_RrQCric-lvxMZKuEcfo/s640/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEicxDY0wNHQ2TcwrdLTaeVZDOJrezKKU-xQ_I_dB5GFllY5z-1TPRfv6cafh_dd4gUWFGveH2Nta_ehrttpbpw-yk1T4c2-Gq-S-fUbGKXVbk1AqPQ6Bj1WYCW_RrQCric-lvxMZKuEcfo/s72-c/1.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/11/rais-mhe-dkt-magufuli-arejea-nchini.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/11/rais-mhe-dkt-magufuli-arejea-nchini.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy