NAIBU WAZIRI MAWASILIANO ATEMA CHECHE,WAKWEPA KODI MARUFUKU TBIII
Mhandisi Balton Komba wa Tanroads (wa nne kushoto) akimpa maelezo ya jengo la tatu la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA-TBIII), Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Uchukuzi na Mawasiliano), Mhe. Mhandisi Atashasta Ndikiye (wa tatu kushoto), na Wakwanza kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela.
HomeJamii

NAIBU WAZIRI MAWASILIANO ATEMA CHECHE,WAKWEPA KODI MARUFUKU TBIII

Na Mwandishi Wetu WAFANYABIASHARA wenye kulipa kodi na kuingizia serikali mapato kwa wakati ndio watakaopata nafasi ya kuwekeza kwe...

MATEMBEZI YA HISANI YA WANAFUNZI ST. JOSEPH'S NURSERY NA PRIMARY SCHOOLS DAR YAFANA
MTOTO WA MKULIMA WAZIRI MKUU MSTAAFU PINDA ATAJA MUAROBAINI WA KUZUIA UCHOMAJI MISITU
VIDEO; MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA UJUMBE KUTOKA UNICEF NA BALOZI WA JAPAN




Na Mwandishi Wetu
WAFANYABIASHARA wenye kulipa kodi na kuingizia serikali mapato kwa wakati ndio watakaopata nafasi ya kuwekeza kwenye jengo la Tatu la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA-TBIII), imeelezwa.
Kauli hiyo imetolewa leo na Naibu Waziri wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Uchukuzi na Mawasiliano), Mhe. Mhandisi Atashasta Nditiye alipofanya ziara ya kutembelea Makao Makuu ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) na kumalizia TBIII.
Mhandisi Nditiye amesema baada ya kukamilika kwa jengo hilo baadaye mwakani, wafanyabiashara watakaopewa kupaumbele hususan waliopo kwenye Jengo la zamani (TBI) na jengo la pili (TBII) ni wale tu wanaozingatia ulipaji wa kodi na mapato yote ya serikali kwa wakati.
“Tunajua wapo wengi waliojitokeza kuomba maeneo ya kufanya biashara, lakini wale ambao watahama kutoka majengo yetu haya mawili la TB I na TBII tunawaambia wazi kabisa kuwa wale waaminifu na waadilifu wenye kulipa kodi ya pango na mapato mengine ya serikali kwa wakati ndio wanafikiriwa kwanza, na wale wasiolipa kwa wakati hawatapewa nafasi kabisa ya kuwekeza kwenye jengo hili,” amesisitiza Mhe. Nditiye.
Hata hivyo, Mhe. Nditiye amesema tayari ameuagiza uongozi wa TAA kuhakikisha wanapitia mikataba yote ya biashara kwenye majengo hayo ya abiria na kutengeneza upya ile yenye matatizo ili iweze kuleta tija kwa taifa, kwani kwa sasa kumekuwa na mikataba ya hovyo.
Amesema TBIII inafursa za biashara ambapo inaeneo kubwa la kujenga hoteli, migahawa na sehemu za kupumzikia watu, hivyo kuwataka wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kuwekeza.
“Juzi tu nilikutana na Wajerumani nikawaeleza tunaeneo la uwekezaji hapa TBIII na kule Msalato mnapotarajia kujenga kiwanja cha kimataifa, na wameonesha nia ya kuja kuwekeza, nia ya serikali na tupo pamoja katika uwekezaji wa maeneo yetu mbalimbali, ili kujiimarisha katika uchumi,” amesema Mhandisi Nditiye.
Naye Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAA, Bw. Richard Mayongela amesema kuwa wanatarajia watoa huduma na wafanyabiashara watakaokidhi vigezo na masharti ya kutoa huduma bora ndio wakaopata nafasi kwenye jengo hilo la tatu.
“Pia tunatarajia watoa huduma na wafanyabiashara ni wale wanaokodhi vigezo kwa hiyo yote yanalenga katika kuhudumia watanzania na kukuza sekta ya usafiri wa anga na kuhudumia vizuri wale wanaopita hapa,” amesema Bw. Mayongela.
Amesema jengo hilo likikamilika litakuwa na uwezo wa kuhudumia abiria takribani milioni sita (6) kwa mwaka ambalo ni ongezeko kubwa ukilinganisha na jengo la sasa la TBII linauwezo wa kuihudumia kati ya abiria milioni 1.2 hadi 1.5 kwa mwaka.
Hivyo tunaishukuru serikali kwa kutupa ushirikiano katika kuendeleza viwanja vya ndege,  pia kwa upande wa TAA wamekuwa wakifanya matengenezo madogo madogo kwa kutumia fedha za bajeti ya ndani.
Hivi karibuni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe. Prof. Makame Mbarawa ameitaka TAA kuwaondoa wafanyabiashara wote wasiolipa kodi na mapato mengine ya serikali kwa wakati, kutokana na kukwamisha juhudi za serikali za ukusanyaji mapato.



 

Mkuu wa Kituo cha Zimamoto na Uokoaji cha Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (wa pili kulia), Juma Yange akimfafanulia jambo Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Uchukuzi na Mawasiliano), Mhe. Mhandisi Atashasta Nditiye (aliyeshika karatasi) alipotembelea kituo hicho. Wa kwanza kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela


Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Uchukuzi na Mawasiliano), (mbele katikati), Mhe. Mhandisi Atashasta Nditiye akiongea na Menejimenti ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) Makao Makuu, kabla ya kuanza kwa ziara ya kutembelea majengo matatu ya abiria ya Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) Oktoba 24 2017.




    Name

    analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
    ltr
    item
    Okandablogs: NAIBU WAZIRI MAWASILIANO ATEMA CHECHE,WAKWEPA KODI MARUFUKU TBIII
    NAIBU WAZIRI MAWASILIANO ATEMA CHECHE,WAKWEPA KODI MARUFUKU TBIII
    https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgv4H8oTYRld0Y7jFGise6610zTF42yezNoFSypJdcOd91oHmYjJzdHWKcvjlZ9sCGqH1Dup6rCGH4sQWdKB00YFeJCDTU-s5Bnqfl0enPKU5zQvVpV7zq4sr_LVZWXnQgVTol_WBAumDs/s640/ziara1.jpg
    https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgv4H8oTYRld0Y7jFGise6610zTF42yezNoFSypJdcOd91oHmYjJzdHWKcvjlZ9sCGqH1Dup6rCGH4sQWdKB00YFeJCDTU-s5Bnqfl0enPKU5zQvVpV7zq4sr_LVZWXnQgVTol_WBAumDs/s72-c/ziara1.jpg
    Okandablogs
    https://robertokanda.blogspot.com/2017/10/naibu-waziri-mawasiliano-atema.html
    https://robertokanda.blogspot.com/
    http://robertokanda.blogspot.com/
    http://robertokanda.blogspot.com/2017/10/naibu-waziri-mawasiliano-atema.html
    true
    7708052459372695991
    UTF-8
    Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy