HUONI HAFIFU HUCHANGIA MATOKEO MABAYA KWA WANAFUNZI DARASANI
HomeJamii

HUONI HAFIFU HUCHANGIA MATOKEO MABAYA KWA WANAFUNZI DARASANI

  Mwalimu wa shule ya Msingi Nguvumali Jijini Tanga akichukua maelezo ya wanafunzi kabla ya kuanza z...

MHANDISI LWENGE: HAKUNA MUDA UTAKAO ONGEZWA MSIPOKAMILISHA MRADI KWA WAKATI
RAIS DKT MAGUFULI AMWANDALIA RAIS MUSEVENI WA UGANDA DHIFA YA KITAIFA JIJINI TANGA
SERIKALI YAOMBWA KUDHIBITI KONOKONO WAHARIBIFU WA MAZAO MKOANI LINDI


HUONI HAFIFU HUCHANGIA MATOKEO MABAYA KWA WANAFUNZI DARASANI

 Mwalimu wa shule ya Msingi
Nguvumali Jijini Tanga akichukua maelezo ya wanafunzi kabla ya kuanza
zoezi la upimaji wa huduma ya macho
wakati wa siku ya afya ya macho duniani ambapo siku
hiyo iliendana na sambamba na upimaji macho ulioendeshwa na Duka la
Miwani la Noor Optics kwa kushirikiana na halmashauri ya Jiji hilo kwa
wanafunzi wa shule za msingi za mabokweni,kwanjeka na nguvumali,
 Mratibu wa Huduma za Macho Mkoa wa Tanga,Dkt Frida Kassiane akiwapima
macho mwanafunzi wa darasa la pili katika shule ya msingi Nguvumali
Jijini Tanga wakati wa siku ya afya ya macho duniani ambapo siku
hiyo iliendana na sambamba na upimaji macho ulioendeshwa na Duka la
Miwani la Noor Optics kwa kushirikiana na halmashauri ya Jiji hilo kwa
wanafunzi wa shule za msingi za mabokweni,kwanjeka na nguvumali,


 Amina Nasoro ambaye Mratibu wa Huduma ya Afya ya Macho katika kampuni ya kampuni ya Noor Optics
inayojishughulisha na matibabu ya macho na utoaji wa miwani Jijini Tanga akichukua maeleza ya wanafunzi kabla ya kuwapima


 Amina Nasoro ambaye Mratibu wa Huduma ya Afya ya Macho katika kampuni ya kampuni ya Noor Optics
inayojishughulisha na matibabu ya macho na utoaji wa miwani Jijini Tanga akichukua maeleza ya wanafunzi kabla ya kuwapima




 Zoezi la Uandikishaji wa majina wanafunzi wa shule ya Msingi Nguvumali kwa ajili ya upimaji wa macho likiendelea
Zoezi la kuwapima wanafunzi likiendelea
SABABU
kubwa za wanafunzi wa shule za msingi  kutokufanya vizuri darasani
imeelezwa inatokana  na uoni hafifi kwa baadhi yao na sio kwamba hawana
akili .


Lakini pia imebainishwa pia kati ya watu 100 kati ya 15
wana kabi liwa na tatizo la macho ambalo limekuwa likiwaathiri kwa asilimia na
kushindwa kufikia malengo yao.


Hayo yalibainishwa juzi na Mratibu wa Huduma za Macho Mkoani
Tanga Dkt Frida Kassiane wakati wa siku ya afya ya macho duniani ambapo yalienda
sambamba na upimaji wa macho uliokuwa ukiendeshwa na kampuni ya Noor Optics
inayojishughulisha na matibabu ya macho na utoaji wa miwani Jijini Tanga.


Alisema hatua hiyo inatokana na baadhi ya wanafunzi
kuumwa macho huku wakiwa hawajitambui kutokana na kutokuwepo kwa utaratibu za
utoaji wa huduma za upimaji machi kwao hususani mashuleni.


“Ukiangalia leo hii baadhi ya wanafunzi utakuwa walikuwa
wakifanya vizuri katika mitihani yao lakini ghafla wanaanza kushuka kiwango na
hili unaweza kukuta linasababishwea na tatizo la macho kama lilivyogundulika
kwa wanafunzi wachache kwenye shule tulizopita “Alisema.


Alisema suala hilo linasababishwa pia na lishe dunia kwa
asilimia kubwa ya watoto wengi ikiwemo kukosa kupata vyakula vilivyokuwa na
virutubisho vinavyoweza kuongeza nguvu na kinga ya macho.


Alisema zoezi hilo ambalo limeanza siku nne zilizopita
limewafikia zaidi ya wanafunzi 1500 katika shule za Msingi,Kwanjeka,Mabokweni
na Nguvumali ambapo baadhi yao walibainika kuna matatizo hayo na kusaidia
matitabu zaidi na kampuni hiyo.


Naye kwa upande wake Mkurugenzi wa Kampuni ya Noor Optics,
Raouf Nasser alisema lengo kubwa ni kutoa huduma hiyo katika shule zote za
msingi ili kusaidia kubaini changamoto za macho zinazowakabili na namna ya
kupatiwa ufumbuzi.


Alisema alisema kampuni hiyo kwa kushirikiana na
halmashauri ya Jiji la Tanga wameamua kuendesha zoezi hilo kila mwaka ili
kuweza kuwasaidia watoto ambao watabainika wanakabiliwa na matatizo hayo ili
waweze kufikishwa kwa wataalamu kwa matibabu zaidi.


“Asilimia kubwa ya wazazi hawana uwezo wa kuwapeleka
watoto wao katika hospitali kufanyiwa vipimo vya matatizo hayo hivyo sisi
tumeamua kwa nia moja kusaidia jamii ikiwa ni kurudisha faida kwao kutokana na
huduma tunazotoa “Alisema.


Aidha alisema msingi mzuri wa kuyatunza macho ni lazima
kuwepo utaratibu wa kuyafanyia vipimo mara kwa mara hasa wanapokuwa kwenye
hatua ya ukuaji kabla ya kufikia umri mkubwa ambapo tatizo hilo linaweza kuwa
kubwa zaidi.
Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: HUONI HAFIFU HUCHANGIA MATOKEO MABAYA KWA WANAFUNZI DARASANI
HUONI HAFIFU HUCHANGIA MATOKEO MABAYA KWA WANAFUNZI DARASANI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjKyRA_AddjyQtJDxUoEhTDtzBBnTPzhoAgxCCWQ1ccVFKwE7ijuiUV_FA3cFqLEnU2BWOCcXL65BShKIqSqTbUxWkl9_gqASVlBB-2d37rCCaqRFQuT8u3NyD52lFY_K3zAMYskjTiqkHh/s640/IMG_9225.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjKyRA_AddjyQtJDxUoEhTDtzBBnTPzhoAgxCCWQ1ccVFKwE7ijuiUV_FA3cFqLEnU2BWOCcXL65BShKIqSqTbUxWkl9_gqASVlBB-2d37rCCaqRFQuT8u3NyD52lFY_K3zAMYskjTiqkHh/s72-c/IMG_9225.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/10/huoni-hafifu-huchangia-matokeo-mabaya_13.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/10/huoni-hafifu-huchangia-matokeo-mabaya_13.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy