SERIKALI KUJENGA DARAJA LA JUU ENEO LA BONDENI JESHINI
HomeJamii

SERIKALI KUJENGA DARAJA LA JUU ENEO LA BONDENI JESHINI

Na Daudi Manongi-MAELEZO, DODOMA. Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano imesema itajenga daraja la juu kwa aji...

MAJALIWA AMPA POLE SHEIKH MKUU WA TANZANIA KWA KUFIWA NA KAKA YAKE
BBC DIRA YA DUNIA JUMATATU 18.09.2017
KAMPUNI YA MATANGAZO YA KWANZA YATANGAZE NEEMA KWA WATANZAGAZI NA WACHAPISHAJI



Na Daudi Manongi-MAELEZO, DODOMA.

Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano imesema itajenga daraja la juu kwa ajili ya kivuko cha waenda kwa miguu (Over head Pedestrian Bridge) eneo la Kawe Bondeni.

Hayo yamesemwa Bungeni leo na Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhe.Isack Kamwelwe aliyekuwa akijibu swali la Mbunge wa  Kawe Mhe.Halima Mdee  kwa Niaba ya Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano. 

“Tatizo la kivuko cha waenda kwa miguu eneo la Kawe Bondeni hadi Jeshini Kata ya Mbezi Juu na Kawe Tayari limeshapatiwa ufumbuzi”, Aliongeza Mhe. Kamwelwe.

Amesema kwa sasa Mkandarasi wa kujenga daraja hilo yupo kwenye hatua za maandalizi ya kuanza ujenzi katika eneo hilo muhimu.

Aidha Serikali ina mpango wa kuweka taa za kuongozea magari katika Barabara  ya Mwenge-Tegeta ambapo Mkandarasi ameshapatikana wa kuweka taa hizo katika makutano ya Afrikana na anatarajia kuanza kazi wakati wowote.

Mbali na Hayo tatizo la Udogo wa mapokeo na matoleo ya maji ya mvua yanayosababisha kero katika eneo la Makonde hadi Mbuyuni,Serikali inakamilisha taratibu za kusaini mkataba wa ujenzi wa mtaro mkubwa eneo la Mbezi Samaki ambao utatatua kero ya barabara kujaa maji nyakati za mvua.

“Serikali ya Awamu ya Tano ni makini sana na itahakikisha changamoto hizi inazifanyia kazi ili wananchi waweze kutumia barabara zetu vyema”Aliongeza Mhe.Kamwelwe.
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: SERIKALI KUJENGA DARAJA LA JUU ENEO LA BONDENI JESHINI
SERIKALI KUJENGA DARAJA LA JUU ENEO LA BONDENI JESHINI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgvE3KKHJvGRNu-aFn6NlXKpjRaFaSJMNSU0ILxUdYBHhDAzmzzL_XyjH3FjhaOAZGPmoM5sKiKRXg2CkodqWgF16sVZUKiGkqRMSJ2k2oYfVtAPXnyT_iT7RRha3KD6KOxNYAxfP7MpQc/s640/DSCF9997.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgvE3KKHJvGRNu-aFn6NlXKpjRaFaSJMNSU0ILxUdYBHhDAzmzzL_XyjH3FjhaOAZGPmoM5sKiKRXg2CkodqWgF16sVZUKiGkqRMSJ2k2oYfVtAPXnyT_iT7RRha3KD6KOxNYAxfP7MpQc/s72-c/DSCF9997.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/05/serikali-kujenga-daraja-la-juu-eneo-la.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/05/serikali-kujenga-daraja-la-juu-eneo-la.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy