WADAU WAOMBA MIUNDOMBINU STENDI YA MABASI MBAGALA JIJINI DAR ES SALAAM
HomeJamii

WADAU WAOMBA MIUNDOMBINU STENDI YA MABASI MBAGALA JIJINI DAR ES SALAAM

  Kijana akisukuma tolori huku akipita kwenye matope katika Stendi ya mabasi ya Mbagala Rangitatu jijini Dar es Salaam jana. Watumiaji...

KATIBU WA BUNGE, KIGAIGAI AZUNGUMZA NA WATUMISHI WA OFISI YA BUNGE KATIKA KIKAO CHA MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA BUNGE MJINI DODOMA
TOFAUTI KUBWA YA MISHAHARA SERIKALINI KUKOMA:MKUCHIKA
ZIMAMOTO WAKONGA NYOYO ZA WANANCHI MAONESHO YA WIKI YA NENDA KWA USALAMA BARABARANI




 Kijana akisukuma tolori huku akipita kwenye matope katika Stendi ya mabasi ya Mbagala Rangitatu jijini Dar es Salaam jana. Watumiaji wa stendi hiyo wameomba Manispaa ya Temeke kuwawekea miundombinu mizuri ili kuruhusu maji kupita katika kipindi hiki cha mvua.
 Muonekano wa stendi hiyo katika kipindi hiki cha mvua.
Wafanyabiashara wakiendelea na biashara zao kwenye stendi hiyo.

Na Dotto Mwaibale

WATUMIAJI wa Stendi ya Mabasi ya Mbagala Rangitatu jijini Dar es Salaam wameiomba Manispaa ya Temeke kuboresha miundombinu ya stendi hiyo katika kipindi hiki cha mvua ili kuondoa adha wanayokabiliana nayo ya kujaa maji.

Ombi hilo limetolewa Dar es Salaam jana na wafanyabiashara na madereva wanaotumia stendi hiyo wakati wakizungumza na waandishi wa habari kuhusu changamoto hiyo waliyonayo ya kujaa maji hasa katika kipndi hiki cha mvua za masika.

Mfanyabiashara ndogo ndogo katika stendi hiyo,  Afidh Abdallah alisema katika kipindi hiki cha mvua stendi hiyo imekuwa ikijaa maji na kusababisha matope hivyo kuwa kero kwao.

"Mvua ikinyesha hatuwezi kufanya biashara katika stendi hii tunashindwa kuzunguka kufuata wateja" alisema Abdallah.

Abdallah alisema kwa kutumia fedha wanazolipa ushuru kila siku manispaa hiyo inaweza kuwawekea hata molamu kwa kipindi hiki cha mvua ili kupunguza madimbwi ya maji wakati wakisubiri kujenga miundombinu ya kudumu.

Mama Lishe katika stendi hiyo Mwajabu Mohamed alisema maji yanapo jaa katika stendi hiyo wateja wao wamekuwa wakishindwa kufika kupata chakula kutoka maeneo mengine kwa kuhofia madimbwi na matope yanayokuwepo.

Said Khatibu ambaye ni dereva wa basi la Manshallah linalofanya safari zake kati ya Dar es Salaam na mikoa ya kusini alisema wakati huu wa mvua changamoto kubwa inayokuwepo eneo hilo ni kushindwa kupata nafasi ya kupakia na kushusha abiria kutokana na maji yanayojaa.

(Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: WADAU WAOMBA MIUNDOMBINU STENDI YA MABASI MBAGALA JIJINI DAR ES SALAAM
WADAU WAOMBA MIUNDOMBINU STENDI YA MABASI MBAGALA JIJINI DAR ES SALAAM
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjPYn6cf2UWYnis-1wx1wj0wMWO3kaz1cSzNwit2X7ofeZEOK5qWzXLbiQRs9cOOy7OnDNMwtX4Lu-vXShf35CdLTx7uWB2Bo9Xvs_exi6gkn-ipPbYodDy3TMbgR4PnMN55F0Iic0deROz/s640/IMG_5218.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjPYn6cf2UWYnis-1wx1wj0wMWO3kaz1cSzNwit2X7ofeZEOK5qWzXLbiQRs9cOOy7OnDNMwtX4Lu-vXShf35CdLTx7uWB2Bo9Xvs_exi6gkn-ipPbYodDy3TMbgR4PnMN55F0Iic0deROz/s72-c/IMG_5218.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/04/wadau-waomba-miundombinu-stendi-ya.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/04/wadau-waomba-miundombinu-stendi-ya.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy