SERIKALI YANUNUA MTAMBO WA KISASA WA MILIONI 101
HomeJamii

SERIKALI YANUNUA MTAMBO WA KISASA WA MILIONI 101

Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO. Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali wamenunua mtambo mpya wa kisasa unaojulikana kama ...

KIPINDUPINDU CHAPIGA HODI JIJINI DAR ES SALAAM CHAUA MTU MMOJA WENGINE 12 WALAZWA HOSPITALI
WAKANDARASI WAZAWA WAIOMBA SERIKALI KUWAPA KIPAUMBELE KATIKA MIRADI YA UJENZI
RAIS DKT. MAGUFULI AMJULIA HALI WAZIRI MKUU MSTAAFU CLEOPA MSUYA NYUMBANI KWAKE UPANGA JIJINI DAR ES SALAAM


Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO.
Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali wamenunua mtambo mpya wa kisasa unaojulikana kama ‘Energy Dispersive X-Ray Fluorescence Spectrometer’ (EDXRF) kwa ajili ya kurahisisha uchunguzi wa kimaabara.
Mtambo huo uliogharimu kiasi cha shilingi 101,785,200 umesimikwa katika Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Kanda ya Nyanda za Juu Kusini mkoani Mbeya kuanzia Februari 21 hadi 23 mwaka huu.
Hayo yamebainishwa leo jijini Dar es Salaam na Mkemia Mkuu wa Serikali. Prof. Samwel Manyele alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu matumizi ya mtambo huo.

Prof. Manyele amesema kuwa mtambo huo umesimikwa mkoani mbeya ikiwa ni moja ya hatua za kuboresha maabara za Kanda zilizopo Arusha, Dodoma, Mbeya, Mtwara na Mwanza, kusogeza shughuli za uchunguzi karibu na wananchi ili kupunguza gharama za kusafirisha sampuli kuja mkoani Dar es Salaam kwa ajili ya uchunguzi.
“Kuwepo kwa mtambo huo ni suluhisho kwa Serikali, Wizara, Viwanda, Mashirika, Wachimbaji wa madini, wajasiriamali na wananchi kwa ujumla ambao walikuwa wanahitaji kufahamu ubora na usalama wa bidhaa mbalimbali za viwandani na mashambani, kutambua uwepo wa madini ya thamani kwenye udongo na bidhaa za vito pamoja na sampuli zinazohusiana na usalama wa afya na mazingira,”alisema Prof. Manyele.
Ameyataja matumizi mengine ya mtambo huo kuwa ni kufanya uchunguzi wa sampuli za migodini, kupima bidhaa za mbao ili kubaini kiwango cha kemikali zinazotumika kutibu mbao, kupima sampuli za mafuta ya kula kwa kuangalia kiwango cha madini ya phosphorus, kupima sampuli za pembejeo za kilimo pamoja na kufanya uchunguzi wa sampuli na vielelezo vinavyohusiana na makosa ya jinai.
Prof. Manyele amefafanua hoja zitakazojibiwa na matumizi ya mtambo huo zikiwemo za kufahamu dhahabu kiasi gani ipo katika udongo unaohitaji kuchenjuliwa, kufahamu mbogamboga zinazolimwa bondeni zina kiasi gani cha madini yanayoathiri watumiaji, kufahamu kiasi cha uranium katika ardhi na vyanzo vya maji pamoja na kufahamu athari za aina ya madini yaliyopo katika maji ya visima virefu na vifupi kwa watumiaji.

Aidha, Mkemia Mkuu amebainisha kuwa baada ya kuzinduliwa kwa mradi huo, Maabara ya Nyanda za juu kusini itakua na majukumu ya kukusanya sampuli za vinasaba vya binadamu (DNA) pamoja na kuwa kituo rasmi cha kukusanyia sampuli nyingine mbalimbali.
Maabara hiyo kwa sasa ipo Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya ambapo kuanzia mwezi Aprili mwaka huu itahamia katika eneo la Lwambi lililopo mkoani humo.
Mkemia Mkuu wa Serikali, Prof. Samwel Manyele (katikati) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) leo jijini Dar es Salaam kuhusu kuanza kazi kwa mtambo mpya wa kisasa wa Energy Dispersive X-Ray Fluorescence (EDXRF) kwa ajili ya kufanyia uchunguzi wa kimaabara. Kutoka (kulia) ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Huduma za Ubora wa Bidhaa,  Daniel Ndiyo, Mkurugenzi Idara ya Usimamizi na Udhibiti wa Kemikali Nchini, Sabanitho Mtega, Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Biashara George Kasinga (kushoto) pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Sayansi Jinai na Huduma za Vinasaba, David Elias.
 
Baadhi ya watumishi wa Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali na Waandishi wa Habari wakimsikiliza Mkemia Mkuu wa Serikali, Prof. Samwel Manyele (hayupo pichani) jijini Dar es Salaam wakati akizungumza kuhusu kuanza kazi kwa mtambo mpya wa kisasa wa Energy Dispersive X Ray Fluorescence (EDXRF) kwa ajili ya kufanyia uchunguzi wa kimaabara. Mtambo huo umefungwa kwenye Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Mkoani Mbeya.
 
Mtambo wa Energy Dispersive X– Ray Fluorescence (EDXRF) unaotumika kupima sampuli mbalimbali zenye asili ya yabisi na vimiminika kama vile vyakula, bidhaa za mafuta, maji, simenti, makaa ya mawe, bidhaa za chuma ili kutambua kiwango cha madini kilichomo ndani ya sampuli hizo. Mtambo huo umefungwa kwenye Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Mkoani Mbeya.
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: SERIKALI YANUNUA MTAMBO WA KISASA WA MILIONI 101
SERIKALI YANUNUA MTAMBO WA KISASA WA MILIONI 101
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjb6Xf7AQMEYDATCuDkP6G7zv6b-oOddXJ3chydBZswtCmLcerwBt8fiXj7Tb72ZrzPQQ96f1zVlqJqCAKSRxJFi_md7eMfak5OEmCEWcAYpCwDWmc7MKh7HwlQLKeSFbpzy3MYwGu1AUI/s640/1.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjb6Xf7AQMEYDATCuDkP6G7zv6b-oOddXJ3chydBZswtCmLcerwBt8fiXj7Tb72ZrzPQQ96f1zVlqJqCAKSRxJFi_md7eMfak5OEmCEWcAYpCwDWmc7MKh7HwlQLKeSFbpzy3MYwGu1AUI/s72-c/1.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/03/serikali-yanunua-mtambo-wa-kisasa-wa.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/03/serikali-yanunua-mtambo-wa-kisasa-wa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy