OPERESHENI YA VIROBA YAFUMANIA KIWANDA CHA NYATI SPRIT KUWA VIROBA
HomeJamii

OPERESHENI YA VIROBA YAFUMANIA KIWANDA CHA NYATI SPRIT KUWA VIROBA

Na Lilian Lundo – MAELEZO. Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira ikishirikiana na Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Ma...

MAREKEBISHO VIDEO-ERIC SHITINDI:SERA MPYA YA VIJANA KUTATUTA CHANGAMOTO ZA VIJANA
SOKO KUBWA LA KUUZIA MAGARI YOTE KUANZA DAR KIGAMBONI
WAZIRI MKUU AKUTANA NA MKURUGENZI WA KAMPUNI YA NAMERA


Na Lilian Lundo – MAELEZO.
Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira ikishirikiana na Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA), Shirika la Viwango Tanzania (TBS) na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)  leo imefanya operesheni kwa baadhi ya wasambazaji wa pombe za kali zinazofungashwa katika plasti maarufu kama kiviroba ili kujiridhisha kama wameitikia wito wa kusitisha utengenezaji, usambazaji na uuzaji wa pombe hizo.
Akiongea na vyombo vya habari Mkurugenzi wa Idara ya Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais, Richard Muyungi amesema kuwa operesheni hiyo imeanza na wasambazaji, wauzaji na watumiaji huku wakiendelea kupitia baadhi ya maombi ya wamiliki wa viwanda juu ya usitishaji wa pombe hizo.
Aidha operesheni hiyo imefanyika katika wilaya za Kinondoni, Temeke na Ilala kwa kutembelea maghala yanayohifadhi pombe hizo ili kujua idadi ya pombe ambazo bado zipo katika maghala hayo pamoja na kufuatilia ikiwa wamiliki wa maghala hayo wametii amri ya kusimamisha usambazaji wa Pombe hizo zilizofungiwa kuanzia Marchi 01, 2017.
Msimamizi wa ghala la Pombe za Viroba  aina ya Kiroba Original lililopo Mabibo wilaya ya Kinondoni  Mhina Rashid amesema kuwa akiba ya pombe hizo za viroba zilizobaki katika maghala yao ni katoni 6600  za ujazo wa Ml 50 na katoni 4909 zenye ujazo wa Ml100.
“Kwa sasa tumefunga maghala na hakuna usambazaji wowote wa pombe aina ya kiroba unaofanyika hapa tunasubiri taratibu za Serikali kujua nini cha kufanya kwa pombe ambazo bado zipo katika maghala,” alifafanua Mhina Rashid.
Aliendelea kwa kusema kuwa ikiwezekana Serikali iongeze muda wa matumizi ya pombe hizo kutokana na kuwa na mzigo mkubwa katika maghala mengi yanayohifadhi pombe hizo.
Kwa upande wake, Afisa Mwandamizi wa Viwango na Mkaguzi wa TBS Banza Suleiman amesema kuwa viroba Original vina nembo ya TBS lakini kutokana na sheria mpya ambayo imepiga marufuku matumizi ya pombe hizo hivyo wasambazaji hawaruhusiwi kusambaza pombe hizo bali wanapaswa kusubiri maelekezo toka Serikalini.
Vile vile operesheni hiyo imefanyika katika kiwanda cha Afro American kilichopo Mwenge ambao ni watengenezaji wa pombe za viroba aina ya Zed, Royal na Dollors na kukuta zaidi ya tani 5 ya pombe hizo.
Msimamizi wa kiwanda hicho Muhandisi Sabra Voleti amesema kuwa wamesimamisha uzalishaji wa pombe za viroba huku wakisubiri maelekezo toka Serikalini. Aidha amesema kuwa kiwanda hicho kinaendelea na uzalishaji wa pombe ambazo vifungashio vyake ni vya chupa.
Kwa upande wake Mwanasheria wa NEMC Manchare Heche Suguta amesema kuwa adhabu ya matumizi ya vifungashio vya plastiki (Viroba) vinatofautiana kati ya mtengezaji, msambazaji, muuzaji na mtumiaji. Aidha adhabu yake ni faini kati ya shilingi elfu 50 na Milioni 5 au kifungo kisichopungua miaka 3.
Hivyo amewataka watanzania kujiepusha na matumizi ya pombe hizo pamoja ikiwa ni pamoja na utengenezaji na usambazaji wake.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Manyara Februari, 2017 aliagiza pombe hizo kutoendelea kutumika kuanzia Marchi 1, 2017.
Meneja wa Kanda ya Magharibi wa Mamlaka ya Dawa na Chakula (TFDA ), Emmanuel Alphonce akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufanya operesheni ya viroba katika kiwanda cha nyati sprit leo Vingunguti jijini Dar es Salaam.
Vijana wakipanga Viroba katika boksi walipokutwa na timu ya operesheni viroba iliyofika katika kiwanda cha Nyati Spirit leo jijini Dar es Salaam.Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii.
Sehemu ya Katoni za Viroba vilivyokutwa katika kiwanda cha nyati sprit leo jijini Dar es Salaam.
Mafisa wa serikali wakikagua nyaraka mbalimbali za kiwanda cha Nyati Sprit ikiwa ni uhalali wake wa kuendelea kufanya biashara katika mfumo mpya kutoendelea.
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: OPERESHENI YA VIROBA YAFUMANIA KIWANDA CHA NYATI SPRIT KUWA VIROBA
OPERESHENI YA VIROBA YAFUMANIA KIWANDA CHA NYATI SPRIT KUWA VIROBA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiyyb41XCUQuS5MVTULj_himV0yhCoogE7h-qGIkaJO2R_IpZ2T105P1vvOU3YBa9UQ4LMFWmWQMOCQ0pXTo-6_qnSMdmy9532-KLeM2MDB_GjBDl3KU7CqhFxuHFrtSmTn9OJxtEG63Myg/s640/1.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiyyb41XCUQuS5MVTULj_himV0yhCoogE7h-qGIkaJO2R_IpZ2T105P1vvOU3YBa9UQ4LMFWmWQMOCQ0pXTo-6_qnSMdmy9532-KLeM2MDB_GjBDl3KU7CqhFxuHFrtSmTn9OJxtEG63Myg/s72-c/1.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/03/operesheni-ya-viroba-yafumania-kiwanda.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/03/operesheni-ya-viroba-yafumania-kiwanda.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy