WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII JINSIA WAZEE NA WATOTO YAKEMEA VITENDO VYA UKEKETAJI WANAWAKE NCHINI
Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Jinsia, Julius Mbilinyi akifafanua jambo mbele ya  waandishi wa habari hawapo pichani kuhusu siku ya kimataifa ya kuzuia ukeketaji. Pamoja naye ni Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Watoto Bi. Margaret Mussai-
HomeJamii

WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII JINSIA WAZEE NA WATOTO YAKEMEA VITENDO VYA UKEKETAJI WANAWAKE NCHINI

Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Jinsia, Julius Mbilinyi akifafanua jambo mbele ya  waandishi wa habari hawapo pichani kuhusu siku ...


WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII JINSIA WAZEE NA WATOTO YAKEMEA VITENDO VYA UKEKETAJI WANAWAKE NCHINI
Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Jinsia, Julius Mbilinyi akifafanua jambo mbele ya  waandishi wa habari hawapo pichani kuhusu siku ya kimataifa ya kuzuia ukeketaji. Pamoja naye ni Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Watoto Bi. Margaret Mussai-
Masuala ya ukatili wa kijinsia ikiwemo ukeketaji yameendelea kuwa tatizo kwa taifa na ulimwengu mzima na ili kukabiliana na tatizo hili, kumekuwa na mwitikio mkubwa wa kimataifa na kitaifa katika kukabilana na vitendo vya ukatili wa kijinsia.
Akiongea na vyombo vya Habari Jijini Dar es Salaam leo  Kaimu Mkurugenzi Idara ya Watoto wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Margaret Mussai amesema Serikali inalaani na kukemea vikali ukatili kwani unadhalilisha na kunyanyasa hadhi na utu wa mwanamke na mtoto wa kike akisema jambo hili halikubaliki.
Aidha aliongeza kuwa ni lazima jitihada za makusudi zichukuliwe na wadau wote kuhakikisha kuwa tunashiriki kwa pamoja kuzuia na hatimaye kutokomeza ukatili wa kijinsia katika jamii zetu, hususan kuzua ukeketaji.
Aidha kulingana na takwimu za Tafiti ya Idadi ya Watu na Afya (TDHS 2010)  inakadiriwa kuwa ukeketaji kwa wasichana na wanawake wenye umri wa miaka 15- 49 ni asilimia 14.6,  hii imepungua kidogo ukilinganisha na asilimia 17.9 mwaka 1996.     Aidha, takwimu hizo kwa mwaka 2015/16 zinaonyesha kiwango cha ukeketaji kwa wanawake na watoto kimepungua kutoka asilimia 14.6 ya mwaka 2010 hadi kufukia asilimia 10.
Margaret ametaja mikoa inayoongoza kwa vitendo vya ukeketaji ni Manyara (58%), ikifuatiwa na Dodoma (47%) na Arusha (41%) akitaja kuwa kupunguwa kwa vitendo vya ukeketaji  kunatokana na kampeni za uhamasishaji, uelewa na kujitambua kwa wasichana wanaofanyiwa vitendo hivyo, hofu ya kufungwa kutokana na uwepo wa sheria zinazotekelezwa, hivyo mangariba na wazee wa kimila kwa kiasi kikubwa wanaamua kuacha mila hii ya ukeketaji.  
Aidha Serikali inahimiza kuendeleza mila zenye manufaa na kujenga utamaduni chanya kwa jamii. Amewaomba  wadau mabalimbali wakiwemo wana habari, mashirika yasiyo ya kiserikali, Taasisi za dini, sekta binafsi na mamlaka za serikali za mitaa kuendelea kuongeza juhudi za kuelimisha jamii kuachana na mila zinazochochea ukeketaji.
Aidha Serikali imetunga sera, sheria, miongozo na kuandaa mikakati mbalimbali katika jitihada za kupambana na tatizo la ukatili wa kijinsia,ikiwemo ukeketaji, Sera ya Wanawake na Maendeleo ya Jinsia (2000) na Mkakati wa Maendeleo ya Jinsia (2005), Sera ya Maendeleo ya Mtoto (2008). Sheria ya Makosa ya Kujamiiana -SOSPA (1998) na Sheria ya Mtoto (2009) vyote vikiwa na lengo la kuzuia ukatili dhidi ya wanawake na watoto.

Katika kuongeza jitihada za kutokomeza ukeketaji serikali imeandaa Mpango wa kazi wa Taifa wa miaka mitano wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto (2017/18-2021/22). Mpangokazi umeanisha maeneo nane muhimu mojawapo ni la kuondoa mila na desturi zenye madhara. Kupitia mpango huu serikali imedhamiria kupunguza ukeketaji kwa wanawake kwa asilimia 50ifikapo mwaka 2022.
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII JINSIA WAZEE NA WATOTO YAKEMEA VITENDO VYA UKEKETAJI WANAWAKE NCHINI
WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII JINSIA WAZEE NA WATOTO YAKEMEA VITENDO VYA UKEKETAJI WANAWAKE NCHINI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjYCkwKSx_vcFKrhz0pEr7sRWoasORgHXAvi4xddjg6L0HxOONbMI4agq6UzLcfmWc3EsnbZ8y6cXgr_7idhbE0qHOae-AdW-x7t05HgfKEGptDXaAeNDVTBnbJV0re7ttFDKYNJswskvez/s640/unnamed+%252850%2529.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjYCkwKSx_vcFKrhz0pEr7sRWoasORgHXAvi4xddjg6L0HxOONbMI4agq6UzLcfmWc3EsnbZ8y6cXgr_7idhbE0qHOae-AdW-x7t05HgfKEGptDXaAeNDVTBnbJV0re7ttFDKYNJswskvez/s72-c/unnamed+%252850%2529.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/02/wizara-ya-afya-maendeleo-ya-jamii.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/02/wizara-ya-afya-maendeleo-ya-jamii.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy