Na Sultani Kipingo, Globu ya Jamii Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imezitaka Michuzi TV, AYO TV na Global TV kusitisha hudum...
Na Sultani Kipingo, Globu ya Jamii
Mamlaka
ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imezitaka Michuzi TV, AYO TV na Global
TV kusitisha huduma zao za TV mtandaoni hadi hapo kanuni za usajili
rasmi ambazo mamlaka hiyo imesema inaandaa kwa huduma hizo zitapokuwa
tayari.
Barua
hiyo, iliyosainiwa na Mkurugenzi Mkuu Mhandisi James Kilaba tarehe 30
January mwaka huu, imevitaka vyombo hivyo ambavyo vinapendwa sana nchini
na nje ya nchi kuacha mara moja kutoa huduma za TV mtandaoni.
"Kwa
mujibu wa section 13 (1) of the electronic and postal communications
Act Cap 306, sheria za Tanzania zinahitaji watoa huduma zozote za aina
hiyo wanahitaji leseni kutoka mamlaka ya mawasiliano", imesema barua
hiyo.
Wamiliki
wa mitandao hiyo - Millard Ayo, Ankal Issa Michuzi na Abdallah Mrisho
- wameeleza kushtushwa kwao kwa agizo hilo la ghafla, tena wakati hata
kanuni zenyewe hazijawekwa.
"Gloval
TV ipo tayari hata leo kukamilisha taratibu za usajili - kama
zingekuwepo - na kwa sababu bado kukamilika tunaomba kupewa muda zaidi
chini ya uangalizi wakati tunasubiria kanuni hizo mpya," alisema
Abdallah Mrisho, Meneja Mkuu wa Global Publishers.
Ankal
Michuzi na Millard Ayo waliunga mkono kauli hiyo na kwa pamoja watatu
hao wameomba kuonana na mkurugenzi wa TCRA ili kuwasilisha maombi rasmi
ya kuruhisiwa kuendelea kutoa huduma hiyo kwa muda wakati kanuni
zikisubiriwa.
Bahati mbaya Mhandisi Kilaba alikuwa safari na swala hilo limepangwa kushughuliwa ataporejea wiki ijayo.
"Ukizingatia
kwamba tumekuwa tunatoa huduma hii kwa muda mrefu na haijulikani kanuni
zitakuwa tayari lini tunaomba TCRA iangalie namna ya kufanya ili
wananchi wanaotutegemea sana wasikose huduma hii", alisema Ankal. Hata
hivyo vituo hivyo vitatu vinaendelea kuhudumu nje ya mchakato wa TV
mtandao.
Ayo
TV, Michuzi TV na Global TV, ambazo zinaongoza kwa mbali kwa kutazamwa
na watu wengi nchini na nje ya nchi, ni TV mtandao pekee zilizoitikia
mwito wa TCRA, kati ya vituo mtandao takriban 51 vilivyopata barua
hiyo.
Ankal
Issa Michuzi wa Michuzi TV, Millard Ayo (wa pili kulia), Askofu wa Ayo TV na Abdallah
Mrisho wa Global TV (wa pili kushoto) wakitoka makao makuu ya Mamlaka ya Mawasiliano
walikoitwa kuchukua barua zao zinazowazuia kuendelea kutoa huduma za TV
mtandao hadi hapo kanuni za usajili na leseni utapokamilika.
COMMENTS