HABARI NJEMA KWA WANA UKEREWE, KUPATA UMEME JUNI 2018
HomeJamii

HABARI NJEMA KWA WANA UKEREWE, KUPATA UMEME JUNI 2018

Na Greyson Mwase, Dar es Salaam Visiwa vidogo vilivyopo katika Ziwa Viktoria vinatarajiwa kupata umeme wa uhakika ifikapo Juni mw...

JICA YAAHIDI KUENDELEA KUIMARISHA MIUNDOMBINU YA TANZANIA
MAKAMU WA RAIS MSTAAFU, DKT. BILAL AONGOZA MAHAFALI KIDATO CHA NNE FEZA BOYS & GIRLS JIJINI DAR ES SALAAM
RAIS DKT MAGUFULI ATEMBELEA MELI YA HOSPITALI YA CHINA, AAGANA NA KUSHUKURU WANAMAJI NA MADATARI WALIOKUJA NAYO


Na Greyson Mwase, Dar es Salaam

Visiwa vidogo vilivyopo katika Ziwa Viktoria vinatarajiwa kupata umeme wa uhakika ifikapo Juni mwakani.

Hayo yalielezwa na Kamishna Msaidizi- Nishati Jadidifu kutoka Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Styden Rwebangila, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam wakati alipokuwa akielezea mafanikio yaliyopatikana Sekta ya Nishati kupitia Nishati Jadidifu chini ya Idara ya Nishati katika upatikanaji wa umeme wa uhakika.

Alisema kuwa, wakandarasi wameshaanza kuweka miundombinu kwa ajili ya umeme wa jua ambapo miradi hiyo inatarajiwa kukamilika kwa asilimia mia moja ifikapo mwezi Juni mwakani.

Akielezea mipango ya Serikali katika kuhakikisha kuwa nishati ya umeme inakuwa ni ya uhakika Mhandisi Rwebangila alisema Wizara inahamasisha vyanzo vingine vya uzalishaji wa umeme kama vile jua, upepo, jotoardhi na kuongeza kuwa inakaribisha wawekezaji kutoka ndani na nje ya nchi kutafiti na kutumia vyanzo hivyo.

Alisema kwa upande wa jotoardhi utafiti ulifanyika na kuonesha maeneo ya Songwe na Ziwa Ngozi mkoani Mbeya na Mlima Meru mkoani Arusha yana viashiria vya jotoardhi.Aliongeza kuwa mara baada ya utafiti kukamilika mwishoni mwa mwaka huu, visima vinatarajiwa kuanza kuchimbwa kwa ajili ya uzalishaji wa nishati ya jotoardhi.

Aliendelea kutaja mipango mingine kuwa ni pamoja na uanzishwaji wa mwongozo kwa ajili ya mfumo wa umeme kwenye majengo na wa udhibiti wa matumizi ya umeme viwandani.

Alisema pia, Wizara inatarajia kuanzisha mfumo mpya wa uhifadhi data na utoaji taarifa za Nishati Jadidifu ujulikanao kama Tanzania Renewable Energy Management Information System (TREMIS) utakaowezesha wawekezaji ndani na nje ya nchi kubaini fursa za uwekezaji zilizopo katika sekta ya Nishati Jadidifu.

Alisema katika mfumo huo kutawekwa taarifa mbalimbali kuhusu, tafiti mbalimbali na fursa za uwekezaji katika nishati jadidifu , sera, sheria na taratibu ili kuvutia wawekezaji kutoka ndani na nje ya nchi.
“Kupitia mfumo huu kutakuwa hakuna haja ya mwekezaji kutoka nje ya nchi kufunga safari hadi Tanzania kwa ajili ya kupata taarifa, taarifa zote zitakuwepo katika mfumo huu utakaounganishwa na tovuti ya Wizara,” alisema Mhandisi Rwebangila.
Kamishna Msaidizi- Nishati Jadidifu kutoka Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Styden Rwebangila, (kushoto) akielezea mafanikio ya sehemu ya nishati jadidifu chini ya Idara ya Nishati katika upatikanaji wa umeme wa uhakika katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika jijini Dar es Salaam mapema tarehe 06 Februari, 2017. Kulia ni Mtaalam wa Nishati Jadidifu, Emillian Nyanda.
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: HABARI NJEMA KWA WANA UKEREWE, KUPATA UMEME JUNI 2018
HABARI NJEMA KWA WANA UKEREWE, KUPATA UMEME JUNI 2018
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj_kldNY4jDCiYI-qxJpv0AVig-YDlYzJKbkfJ_t3JT_TjGTwUjU73L4PXO3HnROft5gc-PyNObJUnlRYx4VnPs9S1RbN2h5-qGIwrXCPrCZKi7RicHf3w2UZky4xj5z3irAXBoHK95xMM/s640/PICHA+NA+1.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj_kldNY4jDCiYI-qxJpv0AVig-YDlYzJKbkfJ_t3JT_TjGTwUjU73L4PXO3HnROft5gc-PyNObJUnlRYx4VnPs9S1RbN2h5-qGIwrXCPrCZKi7RicHf3w2UZky4xj5z3irAXBoHK95xMM/s72-c/PICHA+NA+1.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/02/habari-njema-kwa-wana-ukerewe-kupata.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/02/habari-njema-kwa-wana-ukerewe-kupata.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy