CAG KUCHUNGUZA MAPATO YA SHIRIKA LA NDEGE TANZANIA-MAJALIWA
HomeJamii

CAG KUCHUNGUZA MAPATO YA SHIRIKA LA NDEGE TANZANIA-MAJALIWA

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema atamuagiza Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kuchunguza ukusanyaji wa mapa...

MAJALIWA AFUTURISHA KWENYE VIWANJA VYA BUNGE
WATCH "SEMBENE!" TONIGHT AT 7:30PM.
HOTUBA YA BAJETI KUU YA SERIKALI MWAKA 2017/2018 ILIYOWASILISHWA BUNGENI MJINI DODOMA



WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema atamuagiza Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kuchunguza ukusanyaji wa mapato ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL).
Ametoa kauli hiyo leo (Alhamis, Februari 9, 2017) alipotembelea Makao Makuu ya shirika hilo Jijini Dar es Salaam kwa lengo la kujionea mwenendo wa uendeshaji wake.
“Nitamuagiza CAG  aje aangalie mwenendo wa ukusanyaji wa mapato ya shirika hili kuanzia mwaka jana lilipoanza kufanya kazi hadi sasa,” amesema.
Waziri Mkuu amesema Serikali haiko tayari kuona shirika hilo linakufa tena, hivyo amewataka viongozi wake wahakikishe linaendeshwa kwa mafanikio kwa manufaa ya Taifa. Pia amewataka waache kukusanya mapato kwa kutumia  risiti za kuandika kwa mkono na badala yake waanze kutumia mfumo wa kieletroniki ili kuzuia upotevu wa mapato hayo.
“Vitu vingi vinavyoenda manual ni rahisi kufa. Serikali tumeagiza malipo yote yafanyike kielektroniki na kote tunakotumia mfumo huu tumepata mafanikio,”amesema. Katika hatua nyinginre, Waziri Mkuu amemtaka Kaimu Mkurugenzi wa Fedha na Utawala, Bi. Witness Mbaga ajiridhishe na fedha zinazokusanywa katika eneo la mizigo kama ziko sahihi, lengo ni kudhibiti upotevu wa mapato.
Hata hivyo Waziri Mkuu amewataka viongozi wa shirika hilo kuhakikisha wanazingaria ratiba ya njia na muda wa safari ili wasipoteze wateja.


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P. 980,
DODOMA.
ALHAMIS, FEBRUARI 9, 2017
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na viongozi wa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) wakati alipokwenda kwenye Ofisi kuu ya ATCL kufuatilia mwenendo wa uendeshaji wa Shirika na usimamizi wa mapato , Februari 9, 2017. Kushoto kwake ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawailiano, Profesa Makame Mbarawa na kulia kwake ni Mtendaji Mkuu wa ATCL, Mhandisi Ladislaus Matindi.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na viongozi wa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) wakati alipokwenda kwenye Ofisi kuu ya ATCL kufuatilia mwenendo wa uendeshaji wa Shirika na usimamizi wa mapato , Februari 9, 2017. Kushoto kwake ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawailiano, Profesa Makame Mbarawa na kulia kwake ni Mtendaji Mkuu wa ATCL, Mhandisi Ladislaus Matindi.
 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na viongozi wa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) wakati alipokwenda kwenye Ofisi kuu ya ATCL kufuatilia mwenendo wa uendeshaji wa Shirika na usimamizi wa mapato , Februari 9, 2017. Kushoto kwake ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawailiano, Profesa Makame Mbarawa na kulia kwake ni Mtendaji Mkuu wa ATCL. Mhandisi Ladislaus Matindi.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa Regini Masoud (kulia) kuhusu mfumo mpya wa ukusanyaji mapato kwa njia ya kielektroniki wakati alipotembelea ofisi kuu ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) jijini Dar es salaam kufuatilia mwenendo wa uendeshaji wa Shirika na usimamizi wa mapato, Februari 9, 2017. Kushoto kwake ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawailiano, Profesa Makame Mbarawa na kulia kwake ni Mtendaji Mkuu wa ATCL, Mhandisi Ladislaus Matindi.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa Regini Masoud (kulia) kuhusu mfumo mpya wa ukusanyaji mapato kwa njia ya kielektroniki wakati alipotembelea ofisi kuu ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) jijini Dar es salaam kufuatilia mwenendo wa uendeshaji wa Shirika na usimamizi wa mapato, Februari 9, 2017. Kushoto kwake ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawailiano, Profesa Makame Mbarawa na kulia kwake ni Mtendaji Mkuu wa ATCL, Mhandisi Ladislaus Matindi. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: CAG KUCHUNGUZA MAPATO YA SHIRIKA LA NDEGE TANZANIA-MAJALIWA
CAG KUCHUNGUZA MAPATO YA SHIRIKA LA NDEGE TANZANIA-MAJALIWA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgrf8_rNXTaULbDUwk_gPUMn3YifDLRnyGgD5Oj5OJ5l8JD33VGJUJHQttuVbgOYfYLdeDgk11HHVWEfqFX5_JAXisOWa4VEpEbdCZyCD39sXkNhGyilZ0hPXpYfoVE-YfzKOh4D-RbMvw/s640/RG1A6095.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgrf8_rNXTaULbDUwk_gPUMn3YifDLRnyGgD5Oj5OJ5l8JD33VGJUJHQttuVbgOYfYLdeDgk11HHVWEfqFX5_JAXisOWa4VEpEbdCZyCD39sXkNhGyilZ0hPXpYfoVE-YfzKOh4D-RbMvw/s72-c/RG1A6095.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/02/cag-kuchunguza-mapato-ya-shirika-la.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/02/cag-kuchunguza-mapato-ya-shirika-la.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy