KAMATI YA PAC YARIDHISHWA NA MIRADI YA REA
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (kushoto) akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza( kulia) mara baada ya kuwasili mkoani huo kwa ziara ya kukagua utekelezaji wa Miradi ya Umeme Vijijini katika Mkoa huo.
HomeJamii

KAMATI YA PAC YARIDHISHWA NA MIRADI YA REA

Na Zuena Msuya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) imeridhishwa na utekelezaji wa Miradi ya Umeme Vijijini, unao...

TIGO YATANGAZA WASHINDI WAWILI WA SHINDANO LA DIGITAL CHANGEMAKERS, YAWAZAWADIA DOLA 40,000 JIJINI DAR ES SALAAM LEO
KATIBU MKUU UN AIPONGEZA TANZANIA KWA KUWA KINARA WA AMANI BARANI AFRIKA
EfG YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI SOKO LA TEMEKE STERIO JIJINI DAR ES SALAAM




Na Zuena Msuya
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) imeridhishwa na utekelezaji wa Miradi ya Umeme Vijijini, unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika Awamu ya kwanza na ya Pili ili kuona thamani halisi ya matumizi ya fedha za Serikali katika mradi huo.
Mwenyekiti wa PAC, Livingstone Lusinde alisema hayo mkoani Iringa wakati wa ziara ya kukagua utekelezaji wa mradi wa REA, katika vijiji na Taasisi mbalimbali  zilizopitiwa na Mradi huo.
Lusinde alifafanua kuwa wameridhishwa na utekelezaji wa miradi hiyo baada ya kuona miundombinu iliyotumika na maendeleo ya wananchi katika maeneo ambayo  yamepitiwa na miradi hiyo.
" Tumepita katika vijiji mbalimbali hapa Iringa ambayo nimepitiwa na REA, tumeona namna ambavyo mradi huo umetekelezwa na tumeona miundombinu iliyotumika na maendeleo yake hivyo hatuna budi kusema wazi kuwa tumeridhishwa na utekelezaji wa mradi huu", Alisema Lusinde.
Lusinde aliwasisitiza wakandarasi wanaotekeleza Mradi wa Umeme vijijini, kutumia miundombinu imara inayokwenda sambamba na thamani halisi ya matumizi ya fedha za Serikali katika kutekeleza wa miradi hiyo ili kutimiza malengo yaliokusudiwa na kuondoa hasara za makusudi zinazoweza kujitokeza.
Vilevile aliwataka wakandarasi hao kukamilisha zoezi za kuwaunganisha na huduma ya umeme wananchi na Taasisi zilizoomba huduma hiyo katika maeneo machache yaliyosalia ili kila mwananchi aliyeomba huduma hiyo aweze kuipata kwa wakati na kuitumia.
Kwa upande wake Naibu Waziri wa Nishati na Madini DKt. Medard Kalemani alisema kuwa Awamu ya Tatu ya utekelezaji wa Mradi wa Umeme wa Vijijini utashirikisha Viongozi Serikali za mitaa, Madiwani, Wabunge, Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa.
Alifafanua kuwa lengo la kufanya hivyo ni kutoa fursa kwa wananchi kutoa vipaumbele vya maeneo wanayotaka kufikiwa kwa huduma ya umeme kwa wakati na kuvifikia vijiji vyote nchini.
" Mradi wa REA Awamu ya Tatu utakuwa shirikishi, kwakuwa kabla ya mkandarasi kuanza kazi yake, atatakiwa kuwasiliana na Viongozi wa Serikali ya mitaa, Madiwani, Wabunge, Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa ili wao watoe vipaumbe cha maeneo wanayotaka kufikiwa na mradi huo", alifafanua Dkt. Kalema.
Dkt. Kalemani alibainisha kuwa utaratibu huo utawezesha kuviunganisha vijiji vyote nchini na huduma ya umeme ili kutimiza azma ya Serikali ya kufikia ya uchumi wa Kati ifikapo mwaka 2025.
Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Serikali (PAC) inafanya ziara ya kukagua Miradi ya Umeme Vijijini inayotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Nchini (Tanesco) kwa lengo la kuona thamani hali matumizi ya fedha ya Serikali katika mradi huo.


Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (kulia) akisamilia na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Livingstone Lusinde walipowalisi mkoani wa Iringa, kwa ziara ya kukagua utekelezaji wa Miradi ya Umeme Vijijini mkoani huo.

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (kulia) na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Livingstone Lusinde wasikiliza hoja za Wajumbe wa Kamati ya PAC, (hawapo pichani) kabla ya kuanza ziara ya kukagua utekelezaji wa Miradi ya Umeme Vijijini mkoani Iringa.

Wajumbe wa Kamati ya PAC, wakisikiliza taarifa ya Mkoa wa Iringa, kabla ya kuanza ziara ya kukagua utekelezaji wa Miradi ya Umeme vijijini mkoani Iringa.

Wajumbe wa Kamati ya PAC, wakikagua Miradi ya Umeme Vijijini katika kijiji cha Nyamahana mkoani Iringa.

Add caption

Mwenyekiti wa Kamati ya PAC, Livingstone Lusinde  akiruka pamoja na wanafunzi wa shule ya Sekondari Idodi, wakati wa ziara ya kukagua Miradi ya Umeme Vijijini.

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani akisalimiana na wanafunzi wa shule ya Sekondari Idodi, wakati wa ziara ya kukagua Miradi ya Umeme Vijijini.
Mjumbe wa Kamati ya PAC, Shally Raymond akisisitiza jambo kwa wanafunzi wa shule ya Sekondari Idodi, wakati wa ziara ya kukagua utelezaji wa Miradi ya Umeme Vijijini.























Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: KAMATI YA PAC YARIDHISHWA NA MIRADI YA REA
KAMATI YA PAC YARIDHISHWA NA MIRADI YA REA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhDkwTlPJ-wLR0NHzbB_5H6oBHas7bjwMA1vkAwuAZKsv0LyzyG5m1pZT5xRrNoG3n5p_vtMnx7-Uu3_vekcDHGQ0P5RNuwegFxbKG0FtO-oAvQup8iMgxsVeZJV6XJ5bNrnlq3LzvkugQ/s640/PIX+1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhDkwTlPJ-wLR0NHzbB_5H6oBHas7bjwMA1vkAwuAZKsv0LyzyG5m1pZT5xRrNoG3n5p_vtMnx7-Uu3_vekcDHGQ0P5RNuwegFxbKG0FtO-oAvQup8iMgxsVeZJV6XJ5bNrnlq3LzvkugQ/s72-c/PIX+1.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/01/kamati-ya-pac-yaridhishwa-na-miradi-ya.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/01/kamati-ya-pac-yaridhishwa-na-miradi-ya.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy