WATU 34 WAFARIKI KATIKA MATUKIO YA KUSHINIKIZA RAIS KABILA AJIUDHULU BAADA YA KWISHA MUDA WAKE WA UTAWALA
HomeSiasa

WATU 34 WAFARIKI KATIKA MATUKIO YA KUSHINIKIZA RAIS KABILA AJIUDHULU BAADA YA KWISHA MUDA WAKE WA UTAWALA

Hali ya mambo katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imezidi kuwa tete huku makum...









Hali ya mambo katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imezidi kuwa tete huku makumi ya watu wakiuawa katika maandamano na mapigano ya kikabila.

Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch
limesema idadi ya watu waliouawa hadi sasa katika maandamano
yalioyaoanza Jumatatu dhidi ya Rais Joseph Kabila baada ya muhula wake wa uongozi kumalizika imeongezeka na kufikia watu 34.

Ida Sawyer, Mkurugenzi wa eneo la Afrika ya Kati wa Human Rights Watch amesema, watu 19 wameuawa na maafisa usalama katika maandamano mjini Kinshasa, watano mjini Lubumbashi na sita katika miji bandari ya Goma na Matadi, magharibi mwa nchi. Hata hivyo serikali ya Kinshasa imesema ni watu 22 pekee waliouawa katika makabaliano kati ya waandamanaji na maafisa usalama na kwamba polisi kadhaa pia wameuawa.


Hii ni katika hali ambayo, watu wengine 18 akiwemo afisa wa
polisi wameuawa leo Alkhamisi katika mapigano yaliyotokea kati ya makundi mawili hasimu ya waasi katika mkoa wa Mongala, Kaskazini Magharibi mwa nchi.


Captain Guillaume Djike, msemaji wa polisi katika mkoa huo amesema baadhi wameuawa kwa kufyatuliwa risasi na wengine kwa kukatwa kwa mapanga, baada ya kujiri mapigano kati ya kundi la waasi la Mai Mai Mazembe wa kabila la Nande na wapiganaji wa Nyatura wa kabila la Hutu.


Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anayeondoka Ban Ki-moon ametoa wito kwa pande zote zinazohusika katika mgogoro wa kisiasa huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kutatua mgogoro huo kwa njia za amani.




Rais Joseph Kabila wa DRC anayekabiliwa na mashinikizo ya kuachia ngazi

Upinzani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo umewataka wananchi kutomtambua tena Joseph Kabila kama rais wa nchi hiyo na umewahimiza kuonesha upinzani wao dhidi ya Kabila kwa njia ya amani.
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: WATU 34 WAFARIKI KATIKA MATUKIO YA KUSHINIKIZA RAIS KABILA AJIUDHULU BAADA YA KWISHA MUDA WAKE WA UTAWALA
WATU 34 WAFARIKI KATIKA MATUKIO YA KUSHINIKIZA RAIS KABILA AJIUDHULU BAADA YA KWISHA MUDA WAKE WA UTAWALA
http://media.ws.irib.ir/image/4bk9e2bfea0f0becqa_800C450.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2016/12/watu-34-wafariki-katika-matukio-ya.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/12/watu-34-wafariki-katika-matukio-ya.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy