SERIKALI YATAKIWA KUBAINISHA STENDI ZA DALADALA JIJINI MWANZA
HomeJamii

SERIKALI YATAKIWA KUBAINISHA STENDI ZA DALADALA JIJINI MWANZA

 Mwenyekiti wa Madereva Kanda ya ziwa Hassan Dede akihojiwa na waandishi wa habari. Askari wa kikosi cha usalama barabarani ...

VIDEO;: MAKAMU WA RAIS AFUNGUA MKUTANO MKUU WA 28 WA CHAMA CHA WANASHERIA WANAWAKE TANZANIA
CHUO KIKUU ARDHI (ARU) CHATOA ELIMU KWA WANAFUNZI WA SEKONDARI DAR
MAKAO MAKUU HALMASHAURI YA BUMBULIKUJENGWA KWEHANGALA



 Mwenyekiti wa Madereva Kanda ya ziwa Hassan Dede akihojiwa na waandishi wa habari.





Askari wa kikosi cha usalama barabarani wakiwa wamezisimamisha Daladala kwa kosa la kupakia abira eneo ambalo sio rasmi.




 Jinsi magari yanavyogeuza katika eneo la Buhongwa
 Eneo la stendi isiyokuwa rasmi ya Buhongwa ilivyo katika kadhia ya ubovu
 Mwenyekiti wa Madereva Kanda ya ziwa Hassan Dede akikagua eneo la barabara ya Buhongwa ambayo inatumiwa na madereva Daladala kama stendi
 Gari likigeuza katikati ya barabara kutokana na kukosekana kwa eneo maalumu la stendi


 Wajasiriamali wakiwa katika eneo la biashara huku Daladala zikitumia eneo hilo pia kupakia na kushusha abiria
 Gari inageuza kituoni ambapo ni barabarani huku watu wakiendelea kuvuka barabara
 Dede akikagua barabara iliyoharibika
 Gari ikiwa imepaki katika eneo bovu la barabara ya Buhongwa



 Mwandishi wa habari wa www.wazo-huru.blogspot.com Mathias Canal akimhoji moja ya madereva katika eneo la Buhongwa

 Mwenyekiti wa madereva Kanda ya ziwa Bw Hassan Dede akisalimia na wakazi wa eneo la Nyashishi mara baada ya kuzuru katika eneo hilo ambalo ndilo amependekeza kuwa stendi ya daladala, kushoto kwake ni Mwandishi wa habari wa www.blogspot.com Ndg Mathias Canal

Na Mathias Canal, Mwanza

Uongozi wa Mkoa wa Mwanza umetakiwa kubainisha stendi za Daladala, maeneo maalumu kwa ajili ya kufanyia biashara za mbogamboga na matunda kwa kina mama sambamba na kubainisha maeneo maalumu ambayo daladala haziruhusiwi kusimama kwani kufanya hivyo kutaondoa urasimu uliopo baina ya madereva wa Daladala na askari wa usalama barabarani.

Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa madereva Kanda ya ziwa Bw Hassan Dede wakati alipozuru kujionea kadhia wanazokumbana nazo madereva wawapo barabarani sambamba na kujionea kandia wanayoipata kutokana na ubovu wa barabara na kutokuwa na stendi ya Daladala katika Mtaa wa Buhongwa nje kidogo ya Halmashauri ya Manispaa ya Nyamagana.

Dede alisema kuwa ni ajabu kwa nchi yetu kuwa na kituo cha daladala chenye mwanzo lakini hakina mwisho hivyo kuwafanya madereva kugeuza mahala pasipokuwa rasmi ambapo ni hatari kwa uhai na magari na madereva hao.

Katika eneo la Buhongwa zinapogeuzia daladala kama kituo, barabara yake ni mbovu huku pembeni kukiwa na machinga sambamba na wajasiriamali wanaouza mbogamboga na matunda jambo ambalo linaweza kusababisha hatari kwa wafanyabiashara hao endapo kama gari litaharibika kutokana na hitilafu ya breki.

Hata hivyo alisema kuwa kumekuwa na wimbi la ukamataji na kutozwa faini na askari wa usalama barabarani kwa madereva hao kutokana na kuegesha magari katika eneo la barabara kwa ajili ya kupakia abiria jambo ambalo ni kinyume na utaratibu kwani hakuna kituo katika eneo hilo pamoja na madereva hao kulipia ushuru kila siku.

Dede alisema kuwa katika njia itokayo Kishiri, Airport, Ilemela na Kisesa kuelekea Buhongwa kuna jumla ya Daladala 1900 ambayo kwa siku moja kila gari inalipia ushuru wa shilingi 1000 ambapo kwa gari zote 1900 kwa siku serikali inakusanya kodi ya jumla ya shilingi 1,900,000/=.

Katika kipindi cha mwezi mmoja serikali inakusanya jumla ya shilingi 57,000,000/= huku ikiwa inakusanya jumla ya shilingi 693,500,000 kwa mwaka.

Dede amehoji fedha zote hizo serikali inafanyia nini kama imeshindwa kukarabati barabara itokayo Mwanza Mjini kuelekea Airport sambamba na kukarabati na kubainisha eneo maalumu la stedi kwa ajili ya Daladala.

Sambamba na hayo pia Dede amependekeza serikali kuhamisha kituo cha daladala kisichokuwa rasmi cha Buhongwa kuhamia katika eneo la Nyashishi lililopo mwanzoni mwa Wilaya ya Misungwi kwani kupitia kuwepo kwa eneo hilo daladala zote zitafanikiwa kuingia katika stendi hiyo na serikali itakusanya mapato mengi kwani itakuwa rahisi kuwabana madereva wote.

Katika Barabara itokayo Makao makuu ya Mkoa wa Mwanza (Ofisi ya Mkuu wa Mkoa) kuelekea eneo hilo la Buhongwa kuna vituo rasmi visivyopungua sita huku vituo visivyo rasmi vipo zaidi ya 15 hivyo ni vyema uongozi wa Mkoa wa Mwanza kupitia ofisi ya usalama barabarani kusimamia jambo hilo na kuweka alama mahususi zitakazobainisha vituo hivyo.
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: SERIKALI YATAKIWA KUBAINISHA STENDI ZA DALADALA JIJINI MWANZA
SERIKALI YATAKIWA KUBAINISHA STENDI ZA DALADALA JIJINI MWANZA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiaFasfeh2JYIaYSC6y2qgSRTfp3MBnSlx3Y6rUHZulnMm_7C70MpxxZQbUzud5OHVSPEReVVV6UzV1J9AHbo3nBQY57nGEiWAfAbEn3gmMfgslFC0BGsHGjYXzPNWwYNMOildHXHvbQQyW/s640/1.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiaFasfeh2JYIaYSC6y2qgSRTfp3MBnSlx3Y6rUHZulnMm_7C70MpxxZQbUzud5OHVSPEReVVV6UzV1J9AHbo3nBQY57nGEiWAfAbEn3gmMfgslFC0BGsHGjYXzPNWwYNMOildHXHvbQQyW/s72-c/1.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2016/12/serikali-yatakiwa-kubainisha-stendi-za.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/12/serikali-yatakiwa-kubainisha-stendi-za.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy