SALAMU ZA RAMBIRAMBI ZA CCM KIFO CHA MPIGANIA UHURU, HADIJA BINT KAMBA.
HomeSiasa

SALAMU ZA RAMBIRAMBI ZA CCM KIFO CHA MPIGANIA UHURU, HADIJA BINT KAMBA.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Kanali mstaafu Abdulrahman Kinana amemtumia salamu za rambi rambi Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa...



Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Kanali mstaafu Abdulrahman Kinana amemtumia salamu za rambi rambi Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es salaam Ndg. Ramadhan Madabida kufuatia kifo cha Muasisi wa TANU Bibi Hadija Bint Kamba, kilichotokea jana tarehe 30 Novemba, 2016 jijini Dar es salaam.

Bibi Hadija Bint Kamba ni miongoni mwa wanaharakati waliopigania uhuru na ukombozi wa Taifa letu. Ameshiriki kuanzisha Baraza la Wanawake Tanganyika mwaka 1955 na baadae Umoja wa Wanawake wa Tanganyika (UWT) tarehe 02 Novemba 1962 akishirikiana na Bibi Titi Mohamed.
Bibi Hadija hakuwahi kushika nafasi za uongozi ndani ya Chama na Serikali baada ya uhuru mpaka mwaka 1985 ambapo Mwalimu Nyerere alimtangaza mbele ya Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM na Baraza la Wazee wa Dar es salaam Diamond Jubilee, kuwa ni mtu aliyetoa mchango mkubwa katika ujenzi wa Chama na Nchi, tangu wakati huo Bibi Hadija Bint Kamba alihudhuria Mikutano mikuu ya Chama kama mjumbe mwalikwa mpaka umri ulipomzuia kuweza kushiriki.

Bibi Hadija Binti Kamba, atakumbukwa na wanachama wa CCM kwa uadilifu, uvumilivu, ujasiri na mchango wake mkubwa katika ujenzi na uimarishaji wa Chama chetu, na kwamba mchango wake katika kupigania uhuru na kuleta ukombozi na maendeleo kwa Wanawake wa taifa hili utaendelea kuenziwa na kuthaminiwa na Watanzania.

Hakika sisi ni wa MwenyeziMungu na kwake yeye ndio marejeo yetu. 

Imetolewa na:- 

Christopher Ole Sendeka (MNEC)
MSEMAJI WA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)
01.12.2016
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: SALAMU ZA RAMBIRAMBI ZA CCM KIFO CHA MPIGANIA UHURU, HADIJA BINT KAMBA.
SALAMU ZA RAMBIRAMBI ZA CCM KIFO CHA MPIGANIA UHURU, HADIJA BINT KAMBA.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiagwIf8lxjgHGs9VJG6A2dKHvQ9adp6-cwG_aMereQGD7JTvllcDSFEJIt5XwoxHWTHQDw_jUKRFqGe9e4aNPnRm2k84AQPPYX-vclLgFZtGxSf2N47Bw7CD4vJl0QEok2wvfvEEijyc1o/s200/kQsHYO2roTcAAAAASUVORK5CYII%253D.png
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiagwIf8lxjgHGs9VJG6A2dKHvQ9adp6-cwG_aMereQGD7JTvllcDSFEJIt5XwoxHWTHQDw_jUKRFqGe9e4aNPnRm2k84AQPPYX-vclLgFZtGxSf2N47Bw7CD4vJl0QEok2wvfvEEijyc1o/s72-c/kQsHYO2roTcAAAAASUVORK5CYII%253D.png
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2016/12/salamu-za-rambirambi-za-ccm-kifo-cha.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/12/salamu-za-rambirambi-za-ccm-kifo-cha.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy