RC MTAKA: VIONGOZI WA DINI NA WATANZANIA TUENDELEE KUMUOMBEA RAIS JOHN POMBE MAGUFULI
Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka
HomeMikoani

RC MTAKA: VIONGOZI WA DINI NA WATANZANIA TUENDELEE KUMUOMBEA RAIS JOHN POMBE MAGUFULI

Na Ismail Ngayonga MAELEZO Dar es Salaam 4.12.2016 MKUU wa Mkoa wa Simiyu, Antony Mtaka amewata Viongozi wa Dini na Watan...



Na Ismail Ngayonga
MAELEZO
Dar es Salaam
4.12.2016
MKUU wa Mkoa wa Simiyu, Antony Mtaka amewata Viongozi wa Dini na Watanzania kuendelea kumuombea Rais John Pombe Magufuli katika jitihada zake za kurejesha misingi ya maadili, nidhamu na uwajibikaji katika utumishi wa umma iliyoachwa na Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

 

 Anasema katika kipindi cha mwaka mmoja wa Utawala wa Rais John Pombe Magufuli, Serikali ya Awamu ya tano imejipambanua kwa vitendo katika kupiga vita rushwa, ufisadi na kusimamia nidhamu na miiko ya Uongozi katika utumishi wa Umma.

Hayo yameelezwa leo Jijini Dar es Salaam na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Antony Mtaka wakati wa mahojiano maalum na mwandishi wa habari hizi kuelekea katika maadhimisho ya miaka 55 ya uhuru wa Tanzania Bara.

“Ndani ya Rais Magufuli anaonekana, Mwalimu Nyerere ambaye alikuwa mstari wa mbele katika kukemea hadharani vitendo vya uvunjifu wa maadili ya mtumishi wa umma ikiwemo rushwa na ufisadi” anasema Mtaka.

Kwa mujibu wa Mtaka anasema hatua zinazoendelea kuchuliwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli katika kurejesha nidhamu katika utumishi wa umma ikiwemo mapambano dhidi ya rushwa na ufisadi ni jambo la kupongezwa, kwa kuwa limelenga katika kuwakumbusha watendaji kuwa Uongozi ni dhamana.

Alisema kuwa hatua zinazochuliwa na Rais John Pombe Magufuli, zinaendelea kuongeza heshima ya Viongozi wa Tanzania katika medani ya kimataifa ya kusimamia nidhamu, maadili na miiko ya Uongozi ambayo imetekelezwa katika kipindi chote cha miaka 55 ya uhuru.

Anaongeza kuwa, hatua hizo zilizofikiwa na Viongozi hao ni changamoto kwa Viongozi Vijana waliopo nchini kuendelea kuheshimu misingi iliyoachwa na waasisi wa taifa, na hivyo kuiwezesha Tanzania kuendelea kupiga hatua kubwa za maendeleo katika siku za usoni.

Mtaka alisema Kiongozi wa Umma ni kioo na kiunganishi katika jamii anayoiongoza, hivyo ni wajibu wa kila kiongozi wa umma kujenga taswira chanya ya kiutawala katika kuwahudumia wananchi kwa kutambua kuwa dhamana ya kiongozi ndio tumaini la watawaliwa.

“Katika siku za hivi karibuni tumeshudia sekta binafsi zikichukua watumishi waaandamizi kutoka Serikalini, hiki ni kiashiria kuwa nidhamu na maadili ya kazi yameimarika kwa kiasi kikubwa sana Serikalini” alisema Mtaka.

Akifafanua zaidi Mtaka alisema katika kipindi cha mwaka mmoja wa Serikali ya Awamu ya Awamu ya tano pamekuwepo na mageuzi makubwa katika utendaji na uwazi wa shughuli mbalimbali za Serikali, hatua iliyosaidia kuokoa kiasi kikubwa cha fedha kilichokuwa kikipotea katika miaka ya nyuma.
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: RC MTAKA: VIONGOZI WA DINI NA WATANZANIA TUENDELEE KUMUOMBEA RAIS JOHN POMBE MAGUFULI
RC MTAKA: VIONGOZI WA DINI NA WATANZANIA TUENDELEE KUMUOMBEA RAIS JOHN POMBE MAGUFULI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiyC-Gk1XE64AU0y7u-7WC13JdZH9U6fMSBfnfR_LszgbwSLq_yBzq-cXZjAu50Ab3mDcuqZWBvjXyvAvx78vUg99YD0oj_zxenB7aLTuCcxGfeGgn96SEM1Yan4MklHz92S0dSozu9yEs/s640/Mhe.+Antony+Mtaka.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiyC-Gk1XE64AU0y7u-7WC13JdZH9U6fMSBfnfR_LszgbwSLq_yBzq-cXZjAu50Ab3mDcuqZWBvjXyvAvx78vUg99YD0oj_zxenB7aLTuCcxGfeGgn96SEM1Yan4MklHz92S0dSozu9yEs/s72-c/Mhe.+Antony+Mtaka.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2016/12/rc-mtaka-viongozi-wa-dini-na-watanzania.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/12/rc-mtaka-viongozi-wa-dini-na-watanzania.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy