MAWAZIRI WAPONGEZA PPF, NSSF KWA KUUNGANISHA NGUVU KUWEKEZA KWENYE KIWANDA KIKUBWA CHA MIWA MKOANI MOROGORO
HomeJamii

MAWAZIRI WAPONGEZA PPF, NSSF KWA KUUNGANISHA NGUVU KUWEKEZA KWENYE KIWANDA KIKUBWA CHA MIWA MKOANI MOROGORO

NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID, NGERENGERE WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango na Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

WALIOKOSA MIKOPO SASA HESLB RUKSA KUKATA RUFAA
MAKAMU WA RAIS AFUNGUA TAMASHA LA MAZINGIRA NA MABADILIKO YA TABIA NCHI CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM LEO
OLOLOSOKWAN YAZINDUA UTABIBU KWA NJIA YA TEHAMA


NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID, NGERENGERE

WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu wa Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama, wamepongeza uamuzi wa Mfuko wa Pensheni wa PPF na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), wa kuunganisha nguvu na kuwekeza kwenye mradi wa kiwanda cha sukari, Mkoani Morogoro.

Pongezi hizo walizitoa kwa nyakati tofauti wakati wa mikutano ya hadhara na wananchi wa kijiji cha Kidunda, Kata ya Mkulazi, wilaya ya Morogoro mwishoni mwa wiki.
Mawaziri hao ambao walikuwa kwenye ziara ya kukagua maendeleo ya mradi huo utakaosimamiwa na kampuni ya Mkulazi Holding, iliyobuniwa na Mifuko hiyo kutekeleza mradi.

“Ninawapongeza, Mfuko wa PPF na NSSF kwa kuitikia mwito wa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt John Pombe Magufuli, kwa uamuzi wenu wa kuunga mkono mipango ya serikali ya awamu ya tano ya kujenga uchumi wa viwanda, kwa kuunganisha nguvu na kuwekeza kwenye mradi huu.” Alisema Dkt. Mpango.

Waziri huyo alihimiza taasisi hizo kufanya haraka kukamilisha upembuzi yakinifu, ili utekelezaji kamili wa mradi ufanyike.

Dkt Mpango aliwataka wahandisi kuhakikisha wanatoka maofisini ili kukagua ujenzi wa miundombinu inayoambatana na mradi huo ikiwemo barabara inayojengwa na kampuni ya ujenzi ya SUMA JKT kuelekea eneo la mradi  “Ile barabara ndio itatumika kusafirisha bidhaa mbalimbali  kutoka na kuelekea kiwandani ni vyema kusimamia kikamilifu” alisema Dkt Mpango huku akikisisitiza Kampuni ya SUMA JKT kutekeleza mradi huo kwa kiwango cha ubora ili kulinda imani ya Serikali kwa makampuni ya umma katika utekelezaji wa miradi yake mbalimbali.

Waziri Dkt. Mpango pia aliwapongeza wanakijiji kwa kuupokea mradi kwa ari ya hali ya juu, na kwamba serikali itahakikisha suala la fidia linakamilika kwa haraka ili kuepusha mivutano wakati tayari mradi umekwishakamilika.

Kwa upande wake Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama, naye aliipongeza Mifuko ya NSSF na PPF kwa uamuzi wake wa kuwekeza kwenye kiwanda hicho ambacho. “Kwa kweli nia ya serikali ni kutengeneza ajira kwa wananchi wetu, naomba watekelezaji wa mradi huu kuanza kuainisha mapema aina ya rasilimali watu watakaohitajika kwenye mradi huu ili serikali ianze kuwaanda vijana wa kitanzania kukamata ajira kwenye kiwanda hiki kikubwa.

Awali Mkuu wa mkoa wa Morogoro, Dkt. Kebwe Steven Kebwe, akizungumza wakati wa mkutano huo aliwashukuru NSSF na PPF kwa kuleta mradi huo katika mkoa wa Morogoro ambapo mradi huo utaenda sambamba na ujenzi wa huduma za kijamii ambapo Dkt Kebwe aliwataka vijana wa eneo hilo kufanya kazi na kuchangamkia mradi unaokuja badala ya kuwategemea wanawake na wazee katika shughuli za uzajishaji.


Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango, akihutubia wanakijiji wa kijiji cha Kidunda, Kata ya Mkulazi, Tarafa ya Ngerengere mkoani Morogoro wakati wa ziara yake na Waziri wa Nchi , Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na watu wenye ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama.(wakwanza kulia). Wengine ni Mkuu wa mkoa wa Morogoro, Dkt. Kebwe Steven Kebwe, Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Profesa Godius Kahyarara, Mkurugenzi Mkuu wa PPF, Bw. William Erio, na Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Mkulazi Holding, Bw. Ca


Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, akihutubia wanakijiji wa kijiji cha Kidunda



Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, Waziri Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu), Bi. Jenista Mhagama (watatu kulia), Mkurugenzi Mkuu wa PPF, Bw. William Erio, (wapili kulia), Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Profesa Godius Kahyarara, (wane kulia), na Mshauri wa Mradi wa Mkulazi, Bw.Suleiman Talqwa,wakiangalia ramani ya mradi huo.


Baadhi ya wanakijiji waliohudhuria mkutano huo.


Baadhi ya wanakijiji waliohudhuria mkutano huo.

 Mawaziri hao na ujumbe wao wakikagua ujenzi wa miundombinu ya barabara itokayo Ngerengere kwenda eneo la mradi, unaotekelezwa na kampuni ya SUMA JKT

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dkt. Kebwe Steven Kebwe, akihutubia


Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, akisalimiana na wanakijiji.


Mbunge wa jimbo la Morogoro Kusini Mashariki, Mh. Omary Mgumba akizungumza jambo na mawaziri hao kwenye eneo la mradi.

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: MAWAZIRI WAPONGEZA PPF, NSSF KWA KUUNGANISHA NGUVU KUWEKEZA KWENYE KIWANDA KIKUBWA CHA MIWA MKOANI MOROGORO
MAWAZIRI WAPONGEZA PPF, NSSF KWA KUUNGANISHA NGUVU KUWEKEZA KWENYE KIWANDA KIKUBWA CHA MIWA MKOANI MOROGORO
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjh-OeVjKKna4fN8tNZ6P37OlNh4eg88ZFhVBZRHhRUh7hEfxIvhLGH9s7SrHYmxu91K90NGGnd2rl6slIWGs8jh_fS22V2lSrD8dOdOLWxifcPxWhI991V0Xx01j56huyXjTQZF_kzW4o/s640/pix1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjh-OeVjKKna4fN8tNZ6P37OlNh4eg88ZFhVBZRHhRUh7hEfxIvhLGH9s7SrHYmxu91K90NGGnd2rl6slIWGs8jh_fS22V2lSrD8dOdOLWxifcPxWhI991V0Xx01j56huyXjTQZF_kzW4o/s72-c/pix1.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2016/12/mawaziri-wapongeza-ppf-nssf-kwa.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/12/mawaziri-wapongeza-ppf-nssf-kwa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy