MAKAMU WA RAIS, SAMIA SILUHU HASSAN AFUNGUA MKUTANO WA WADAU WA MAENEO TENGEFU YA VIWANDA VYA USINDIKAJI VYAKULA
HomeJamii

MAKAMU WA RAIS, SAMIA SILUHU HASSAN AFUNGUA MKUTANO WA WADAU WA MAENEO TENGEFU YA VIWANDA VYA USINDIKAJI VYAKULA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati ufunguzi wa mkutano wa Wada...

SERIKALI KUREJESHA MIKOPO KWENYE MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII
WAFANYAKAZI WA TAASISI YA MOYO JAKAYA KIKWETE (JKCI) WAUAGA MWILI WA MFANYAKAZI MWENZAO AMBAYE NI DAKTARI BINGWA WA USINGIZI KWA WATOTO NA WAGONJWA MAHUTUTI ALIYEFARIKI TAREHE 02/05/2018.
WAZIRI MAHIGA NA WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA UJERUMANI WAKUTANA KWA MAZUNGUMZO RASMI





Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati ufunguzi wa mkutano wa Wadau wa kuendeleza maeneo Tengefu ya Viwanda vya Usindikaji Vyakula uliofanyika kwenye ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati ufunguzi wa mkutano wa Wadau wa kuendeleza maeneo Tengefu ya Viwanda vya Usindikaji Vyakula uliofanyika kwenye ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam ambapo aliwapongeza TAFOPA kwa kazi nzuri wanayoifanya lakini pia aliwataka Wasindikaji kuongeza ushirikiano ili kufikia maendeleo na mafanikio ya juu.
Wadau waliohudhuria na kushiriki wakimsikiliza kwa makini Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati ufunguzi wa mkutano wa Wadau wa kuendeleza maeneo Tengefu ya Viwanda vya Usindikaji Vyakula uliofanyika kwenye ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam. 
 
 
 
Mwenyekiti wa TAFOPA Bi. Suzy Laizer akihutubia wakati ufunguzi wa mkutano wa Wadau wa kuendeleza maeneo Tengefu ya Viwanda vya Usindikaji Vyakula uliofanyika kwenye ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam, mgeni rasmi kwenye mkutano huu alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.
 
 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiangalia bidhaa mbalimbali za vyakula vilivyosindikwa zinazotengenezwa na wajasiriamali muda mfupi kabla ya kufungua wa mkutano wa Wadau wa kuendeleza maeneo Tengefu ya Viwanda vya Usindikaji Vyakula uliofanyika kwenye ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.

.................................................................

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amesema Serikali ipo mbioni kupunguza muda wa utoaji wa leseni za biashara nchini ili kutoa fursa kwa wananchi wengi zaidi kupata leseni hizo kwa ajili ya shughuli za kibiashara.

Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan ametoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere wakati anafungua mkutano wa wadau wa kuendeleza maeneo tengefu ya viwanda vya usindikaji wa vyakula nchini.
Makamu wa Rais amesema mpango utaenda pamoja na kupunguza baadhi ya kodi na tozo ambazo ni kero kwa wananchi hasa wenye viwanda kama hatua ya kukuza biashara na uwekezaji katika sekta ya viwanda nchini.

Amesisitiza kuwa Serikali inaendelea na mazungumzo na wenye mabenki hususani benki ya TIB ili kutoa mikopo yenye riba nafuu kwa wawekezaji wenye nia ya kuanzisha viwanda.
Kuhusu usindikaji wa bidhaa nchini, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan ambaye pia ni Mjumbe katika jopo la Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa la kumuwezesha mwanamke kiuchumi akiwakilisha nchi za ukanda wa Kusini na Mashariki mwa Afrika amepongeza jitihada zinazofanywa na wasindikaji wadogo nchini katika utengenezaji wa bidhaa mbalimbali ambazo zitakidhi katika masoko ya ndani na nje ya nchi.

“Serikali inafarijika sana kuona kuwa wasindikaji wadogo nchini wamethubutu na wana uwezo wa ushindani katika biashara ya ndani na hata nje, hivyo tunayohaki ya kujigamba kwa kuthubutu, Tumeweza na Tuendelea Kusonga mbele

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amesema umefika wakati kwa Wizara na taasisi za Serikali na wadau wa maendeleo kuona umuhimu wa kuhakikisha viwanda vinajengwa vijijini ili mkulima mdogo anapolima awe na uhakika wa kupata soko katika viwanda hivyo.
Amesema kuwa hali hiyo itaondoa changamoto ya kusafirisha bidhaa nyingi ambazo zinaharibika njiani au zinapofika sokoni na hivyo kukosesha jamii kipato kilichotarajiwa.
Makamu wa Rais pia amehimiza watafiti nchini wajielekeza katika kufanya tafiti ambazo zitasaidia sekta binafsi na serikali kwa ujumla kuhusu namna bora ya kukuza sekta ya viwanda nchini.
Kwa upande wake, Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Charles Mwijage amekiri kuwa bado kuna changamoto kubwa ya maeneo ya yatakayojengwa viwanda na kwamba Serikali imeliona tatizo hilo na inalifanyia kazi ambapo tayari imeshaziagiza Halmashauri zote nchini kujenga maeneo kwa ajili ya viwanda.
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: MAKAMU WA RAIS, SAMIA SILUHU HASSAN AFUNGUA MKUTANO WA WADAU WA MAENEO TENGEFU YA VIWANDA VYA USINDIKAJI VYAKULA
MAKAMU WA RAIS, SAMIA SILUHU HASSAN AFUNGUA MKUTANO WA WADAU WA MAENEO TENGEFU YA VIWANDA VYA USINDIKAJI VYAKULA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhNFXMhRuVSHFh7FX0zmBnwl4K2H9992sNf8gO-aNZPaveoCCCm3Pctb_4VTgA7cMw44Zn64KwOpEIdOnOUH2ITq1nsbnCrezXnEnk0s3tcXV-QQL_uIxqzWq4FhoiT4coqV9N-jeo4luY/s640/18.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhNFXMhRuVSHFh7FX0zmBnwl4K2H9992sNf8gO-aNZPaveoCCCm3Pctb_4VTgA7cMw44Zn64KwOpEIdOnOUH2ITq1nsbnCrezXnEnk0s3tcXV-QQL_uIxqzWq4FhoiT4coqV9N-jeo4luY/s72-c/18.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2016/12/makamu-wa-rais-samia-siluhu-hassan.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/12/makamu-wa-rais-samia-siluhu-hassan.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy