MAJALIWA AKUTANA NA WAFANYABIASHARA WA ARUSHA
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na wafanyabiashara wa Arusha kwenye Kituo cha Mikutano cha Arusha (AICC) Desemba 2, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
HomeJamii

MAJALIWA AKUTANA NA WAFANYABIASHARA WA ARUSHA

APIGA MARUFUKU UCHAPAJI HOLELA WA VITABU VYA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIA  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na...

MABALOZI WALIOAPISHWA JANA WAMUAGA MAKAMU WA RAIS
PROF. MBARAWA AAHIDI KUKAMILIKA KWA UJENZI WA DARAJA LA MTO MARA
MPINA AMUAGIZA KATIBU MKUU UVUVI, KUHARAKISHA MCHAKATO WA KUTAIFISHA MELI YA KAMPUNI YA BUAH NAGA ONE.


APIGA MARUFUKU UCHAPAJI HOLELA WA VITABU VYA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIA






 Baadhi ya wafanyabiashara wa Arusha wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipozungumza nao kwenye Ukumbi wa Simba katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha, Desemba  2, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imepiga marufuku uchapaji holela wa vitabu vya kufundishia na kujifunzia kwa wachapaji binafsi na badala yake uchapaji huo utasimamiwa na Taasisi ya Elimu Tanzania (TIE) ili kuthibiti ubora.

Amesema mbali na kudhibiti wa ubora pia uamuzi huo unalenga kuwa na kitabu kimoja kwa kila somo kwa kila mwanzfunzi kwa nchi nzima ili kuweka uwiano mzuri katika ufundishaji na upimaji wa wanafunzi .

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Ijumaa, Desemba 2, 2016) wakati akizungumza na walimu wa halmashauri ya Jiji la Arusha na wilaya ya Arusha kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC) akiwa katika siku ya kwanza ya ziara ya kikazi mkoani Arusha.

Ziara hiyo inalenga kukagua utelelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM,Utendaji wa Serikali, kusikiliza na kujionea kero zinazowakabili wananchi  wa Mkoa huo kwa kushirikiana na viongozi wa Mkoa ili kuweza kuzitafutia suluhisho.
Amesema kipindi cha nyuma vitabu vilikuwa vinachapwa na watu mbalimbali hivyo kusababisha malalamiko makubwa kutokana na vitabu hivyo kuwa na makosa mengi. “Sasa vitabu vikibainika kuwa na makosa tutaibana Taasisi ya Elimu Tanzania,”.
Aidha, amesema Serkali itahakikisha kila mtoto anakuwa na kitabu chake ili kuwawezesha kusoma vizuri na kuwa na uelewa wa kutosha ikiwa ni pamoja na kuwarahisishia walimu katika ufundishaji.
Hata hivyo, Waziri Mkuu amezungumzia kuhusu madeni ya walimu, ambapo  amewataka Wakurugenzi wa  Halmashauri zote nchini kutenga fedha katika mapato yao kwa ajili ya kulipa madai ya watumishi mbalimbali katika maeneo yao wakiwemo walimu.
Awali Waziri Mkuu alizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Jiji na wilaya ya Arusha na kumuagiza Kamanda wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Arusha kumchunguza Ofisa Utumishi wa wilaya ya Arusha, Bi. Imelda Isosi kufuatia tuhuma za rushwa, ufisadi, unyanyasaji kwa watumishi zilizotolewa dhidi yake.

Waziri Mkuu alitoa agizo hilo baada watumishi hao kupewa fursa ya kumuuliza maswali ambapo mhudumu wa Chumba cha kuhifadhia maiti wa Hospitali ya  Ortumet Wilayani Arusha, Bw. Bernard Mtei kudai kwamba halmashauri ya wilaya ya Arusha inanuka ufisadi na rushwa hususan katika sekta ya afya.

Baada ya kutoa madai hayo Bw. Mtei alimkabidhi Waziri Mkuu nyaraka mbalimbali zenye uthibitisho wa madai hayo, ambapo Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Bw. Mrisho Gambo amuhakikishia Waziri Mkuu kwamba watafanya uchunguzi wa kina dhidi ya tuhuma hizo na zikithibitika wahusika watachukuliwa hatua za kinidhamu na kisheria

Wakati huo huo Waziri Mkuu ameitaka Idara ya Uhamiaji kudhibiti wahamiaji haramu kwa kuanza kufanya misako katika nyumba za kulala wageni ili kuwabaini wageni wanaoingia nchini bila ya kibali kwani ni chanzo cha kuingiza silaha haramu nchini.
Amesema inashangaza kuona silaha za aina nyingi katika maeneo mbalimbali ambazo Tanzania hakuna ambazo zinadaiwa kuingia nchini kupitia maeneo ya mpakani. “Hivyo ni lazima Idara ya Uhamiaji ihakikishe wanadhibiti uingiaji wa wahamiaji kwenye mipaka mbalimbali nchini,”.
Waziri Mkuu amesema Serikali haizuii wageni kutoka mataifa mengine kuingia nchini ila ni lazima udhibiti wa wageni hao ufanyike ikiwa ni pamoja na kujiridhisha sababu za kuja nchini na muda watakao kuwepo.
Hata hivyo aliwasihi watumishi wa idara mbalimbali za Serikali kuhakikisha wanafanya kazi kwa nidhamu, weledi, uadilifu na kuwatumikia wananchi wanaohitaji huduma mbalimbali hata kama wamekosea kuuliza katika maeneo yao.
Amesema “baadhi ya wananchi  hawana uelewa juu ya wapi wapeleke malalamiko yao lakini kwa kuwa wewe ni mtumishi wa umma unapaswa kumsikiliza na kumwelekeza aende wapi badala ya kumtolea maneno yasiyofaa,”.


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU
IJUMAA, DESEMBA 2, 2016.
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: MAJALIWA AKUTANA NA WAFANYABIASHARA WA ARUSHA
MAJALIWA AKUTANA NA WAFANYABIASHARA WA ARUSHA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgFkBMwwU8bF4u1B64eTiKhagwoUXTT30Q0gD4_Jwccdum4sBy5f-S7dzNbZDI5I9kGV9Wms-4OR59obSqXvl0PM1S8NYyCHjYf0wEJTL30ERehJF47z87PqcDQkdiqxnsYWlhIYCY3Bf4/s640/RG1A5114.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgFkBMwwU8bF4u1B64eTiKhagwoUXTT30Q0gD4_Jwccdum4sBy5f-S7dzNbZDI5I9kGV9Wms-4OR59obSqXvl0PM1S8NYyCHjYf0wEJTL30ERehJF47z87PqcDQkdiqxnsYWlhIYCY3Bf4/s72-c/RG1A5114.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2016/12/majaliwa-akutana-na-wafanyabiashara-wa.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/12/majaliwa-akutana-na-wafanyabiashara-wa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy