ZIARA YA NAIBU WAZIRI TAMISEMI YAMUINGIZA KIKAANGONI MGANGA MKUU MANISPAA YA KIGOMA

Naibu Waziri wa Tamisemi, Selemani Jafo akikagua mradi wa Maji Katika wilaya ya Mbogwe mkoani Geita.       Naibu Wazi...










Naibu Waziri wa Tamisemi, Selemani Jafo akikagua mradi wa Maji Katika wilaya ya Mbogwe mkoani Geita.
 
 
 


Naibu Waziri Selemani Jafo akikagua ujenzi wa Hospital ya Rufaa ya Mkoa wa Mara mjini Musoma.

Naibu Waziri wa Tamisemi Selemani Jafo akikagua kiwanda cha vijana cha kutengeneza Chaki mjini Maswa mkoani Simiyu.
 



Naibu Waziri Selemani Jafo akiwa na mtoto wa baba wa Taifa Madaraka Nyerere pamoja na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Edo Mapunda, nyumbani kwa Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Nyerere Butiama.
 


Naibu Waziri wa Tamisemi, Selemani Jafo akiwa na Mbunge wa Mbogwe Silivester Massele wakikagua jenereta la kusukuma maji Katika wilaya ya Mbogwe.

Naibu waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Selemani Jafo amefanya ziara katika Mkoa wa Kigoma huku akimuagiza Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma kuunda timu ya uchunguzi juu ya malalamiko ya wananchi kuhusu tuhuma za wizi wa madawa na ujenzi wa wodi ya kina Mama ya Buhando na ujenzi ulio fanyika Katika zahanati zingine ndani ya Manispaa ya kigoma

Hatua hiyo ya Jafo ilitokana na kutoridhishwa na utendaji wa mkuu wa idara ya Afya ya Manispaa ya Kigoma, John Maganga kutokana na usimamizi mbovu wa miradi hiyo katika idara yake sambamba na kuwepo kwa malalamiko mengi ya ubadhilifu wa madawa ndani ya Manispaa hiyo.

Jafo alitembelea jengo la wazazi la Zahanati ya Buhanda ambapo hakuridhishwa kabisa na maelezo ya ubora wa jengo hilo na mganga mkuu huyo kushindwa kumpa Naibu Waziri maelezo ya kuridhishwa juu ya gharama za ujenzi wa jengo hilo ambalo limejengwa chini ya kiwango na kuwepo mashaka makubwa ya upotevu wa fedha nyingi katika ujenzi wa jengo hilo lililo zinduliwa kinyemela na DMO huyo.

Kutokana na simtofahamu hiyo Naibu Waziri amemtaka Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma kuunda timu ya uchunguzi na kwamba lengo la ziara hiyo ni kuleta ufanisi katika kuwahudumia wananchi ndani ya halmashauri mbalimbali hapa nchini.

Jafo katika Mikoa minne ya Mara, Simiyu, Geita na Kigoma ambapo alizifikia Halmashauri 19 na kuongea na watumishi zaidi ya 6000 pamoja na kukagua miradi mbalimbali 25 ya barabara, maji, afya, elimu na ujasiliamali imeleta tija sana kwa kuinua hamasa ya utendaji kazi kwa watumishi wa halmashauri za wilaya.

Ziara hiyo aliifanya baada ya kufunga Mkutano Mkuu wa 32 wa Jumuiya ya Taasisi za Serikali za Mitaa (ALAT) uliofungwa rasmi tarehe 24 September 2016 mjini Musoma Mkoani Mara. Ziara ya Naibu Waziri huyo ilianza tarehe 25 September hadi 30 September 2016 ambapo alikagua miradi na kuongea na watumishi.

Jambo kubwa lililo sisitizwa Katika ziara hiyo ni umuhimu wa watumishi wa halmashauri kufanya kazi kwa kuzingatia taaluma zao pamoja na kuweka maslahi ya Taifa mbele.Aliwataka wakurugenzi kuwekeana malengo ya utekelezaji na wakuu wao wa Idara, na wakuu wa idara kuwekeana malengo na watendaji wao wa chini wanao waongoza.

Kadhalika, Aliwataka watendaji wa halmashauri wabadilike katika utendaji wao. Amewataka wakuu wa idara kutowabagua baadhi ya watumishi katika idara zao.

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: ZIARA YA NAIBU WAZIRI TAMISEMI YAMUINGIZA KIKAANGONI MGANGA MKUU MANISPAA YA KIGOMA
ZIARA YA NAIBU WAZIRI TAMISEMI YAMUINGIZA KIKAANGONI MGANGA MKUU MANISPAA YA KIGOMA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhYxH_oTYXC4hzyxS7EC5-G2mglh4stdchTH7QvzS0KRnEtetbm2WbzYjlnXaav_CTLPmZ3-XebrGMpsNgllysMOq8VuKyAA1pdumpoB7Hz_b9YBmyINX1_xTZOebWy70loN987ReTRTnmg/s640/IMG-20161002-WA0074.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhYxH_oTYXC4hzyxS7EC5-G2mglh4stdchTH7QvzS0KRnEtetbm2WbzYjlnXaav_CTLPmZ3-XebrGMpsNgllysMOq8VuKyAA1pdumpoB7Hz_b9YBmyINX1_xTZOebWy70loN987ReTRTnmg/s72-c/IMG-20161002-WA0074.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2016/10/ziara-ya-naibu-waziri-tamisemi.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/10/ziara-ya-naibu-waziri-tamisemi.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy