WAZIRI MKUU AAGIZA MAPATO YA HOSPITALI YA NACHINGWEA YAKUSANYWE KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI
HomeSiasa

WAZIRI MKUU AAGIZA MAPATO YA HOSPITALI YA NACHINGWEA YAKUSANYWE KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na Mkewe Mery Majaliwa wakimsalimia Bahati Omary kutoka kijiji cha Nangao Wilaya Liwale ambaye ...










Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na Mkewe Mery Majaliwa wakimsalimia Bahati Omary kutoka kijiji cha Nangao Wilaya Liwale ambaye amejifungua mtoto wa kike katika Hospitali ya wilaya ya Nachingwea Waziri mkuu alifika katika Hospitali hapo kujionea jinsi huduma za afya zinavyo tolewa kwa wagonjwa waziri mkuu yupo katika ziara ya kikazi katika wilaya ya Nachingwea na Ruwangwa  Mkoani Lindi.
 
luw2
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiongea na watumishi wa Hospitali ya Nachingwea pamoja na wananchi waliofika katika Hospitali ya nachingwea Waziri Mkuu alifanya ziara ya kutembelea hospitalini hapo kwa ajili yakuona na kusikiliza wagonjwa wanavyo pata huduma.
 
luw3
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Liwale Sarah Chiwanga ambaye nimiongoni wa viongozi wa mkoa wa Lindi waliofika katika kiwanja cha ndege Nachingwea kumpokea Waziri mkuu na mkewe Mary Majaliwa na kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi Godfrey Zambi ambao wamewasili katika Mkoa wa Lindi kwa ziara ya kikazi katika wilaya ya Nachingwea na Ruwangwa.
(Picha na Chris Mfinanga)
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametoa mwezi mmoja kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Nachingwea, Bw. Bakari Mohammed kuhakikisha hospitali ya wilaya hiyo inakusanya mapato kwa kutumia mfumo wa kielektroniki.
Ametoa agizo hilo leo (Jumapili, Oktoba 16, 2016) wakati alipotembelea hospitali ya wilaya ya Nachingwea akiwa kwenye ziara yake ya kikazi ya siku tatu mkoani Lindi.

Waziri Mkuu amesema Serikali ilishaagiza taasisi zote za umma kutumia mfumo wa kielektroniki katika ukusanyaji wa mapato kwa lengo la kudhibiti mianya ya upotevu wa fedha za umma.

Amesema taasisi ambazo tayari ziameanza kutumia mfuko huo katika ukusanyaji wa mapato zimeweza kuongeza kiwango cha makusanyo kutoka sh. 300,000 hadi milioni nne kwa siku.

Pia aliwaagiza viongozi wa wilaya hiyo kuendelea kuwahamasisha wananchi kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) ambao utawawezesha kupata huduma ya matibabu bure katika kipindi cha mwaka mzima.

Akizungumzia kuhusu matibabu kwa wazee, Waziri Mkuu amemuagiza Bw. Mohammed kuhakikisha anafungua dirisha la kuwahudumia wazee ili kuwarahisishia upatikanaji wa huduma wanapofika hospitalini hapo.

“Mkurugenzi hakikisha watendaji wako wa kata na vijiji wamebaini wazee wote katika maeneo yao na kuwatengenezea vitambulisho vitakavyowawezesha kupatibiwa bure,” amesema.

Naye Mganga Mkuu wa wilaya hiyo Dk. Samwel Laizer amesema muamko mdogo wa jamii kujiunga na CHF ni moja kati ya changamoto zinazowakabili katika utoaji wa huduma za afya.

Dk. Laizer amasema kati ya kaya 30,000 zilizoko wilayani Nachingwea ni kaya 7,133 tu ndizo zilizojiunga na mfuko wa CHF.

Awali Waziri Mkuu alizungumza na watumishi wa wilaya hiyo kwenye ukumbi wa Chuo Cha Walimu na kuwataka wabadilike ili waweze kuwatumikia wananchi kwa uadilifu bila ya kujali itikadi zao za kidini na kisiasa.

Amesema Serikali haitamvumilia mtumishi yeyote atakayeshindwa kutekeleza wajibu wake wa kuwatumikia wananchi. “Serikali haitaridhika kuona wananchi wakizagaa kwenye ofisi za halmashauri hiyo bila ya kusikilizwa,” amesema.



IMETOLEWA NA:

OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMAPILI, OKTOBA 16, 2016
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: WAZIRI MKUU AAGIZA MAPATO YA HOSPITALI YA NACHINGWEA YAKUSANYWE KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI
WAZIRI MKUU AAGIZA MAPATO YA HOSPITALI YA NACHINGWEA YAKUSANYWE KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi3-6RCDL0OGIjicyJUh1yYZqN_-AgGBCqMj4aiwltFd9-FoZwUhrpeT0uxduFTmrK9l180bRuJ4bED5hMvPrvA7rSJmQMEEjUSjsXVdVHKC34PUv9-eYHxrUcPFCon4CXWFnlBHU1bXkA/s640/LUW1-768x512.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi3-6RCDL0OGIjicyJUh1yYZqN_-AgGBCqMj4aiwltFd9-FoZwUhrpeT0uxduFTmrK9l180bRuJ4bED5hMvPrvA7rSJmQMEEjUSjsXVdVHKC34PUv9-eYHxrUcPFCon4CXWFnlBHU1bXkA/s72-c/LUW1-768x512.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2016/10/waziri-mkuu-aagiza-mapato-ya-hospitali.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/10/waziri-mkuu-aagiza-mapato-ya-hospitali.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy