WAHITIMU ST. EMMANUEL CHAMAZI TEMEKE JIJINI DAR ES SALAAM WAASWA KUZINGATIA ELIMU
HomeJamii

WAHITIMU ST. EMMANUEL CHAMAZI TEMEKE JIJINI DAR ES SALAAM WAASWA KUZINGATIA ELIMU

  Mkurugenzi Mtendaji wa Shule ya ST. Emmanuel High School, Ernest Masaka, akizungumza katika mahafali ya saba ya Kidato cha Nne ya...

SPIKA NDUGAI, KATIBU WA BUNGE, NDG. KAGAIGAI WATEMBELEA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA ARDHI, MALIASILI NA UTALII
MPANGO WA UENDESHAJI WA KIJINSIA KWA AJILI YA MWITIKIO WA UKIMWI TANZANIA BARA WATAMBULISHWA RASMI KWA MKOA WA SINGIDA
HITILAFU YA MFUMO WA KUPOKELEA GESI KINYEREZI I, TATHIMINI YAONYESHA MATENGENEZO MAKUBWA YANAHITAJIKA.







 Mkurugenzi Mtendaji wa Shule ya ST. Emmanuel High School, Ernest Masaka, akizungumza katika mahafali ya saba ya Kidato cha Nne yaliyofanyika Chamazi jijini Dar es Salaam jana. Wengine kutoka kulia ni Mkuu wa shule hiyo, Khalid Simba, Diwani wa Kata ya Chamazi, Hemedi Karata  ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye mahali hayo, Katibu wa Diwani huyo na Lucy Peter, mke wa Mkurugenzi wa shule hiyo.


 Mkuu wa shule hiyo, Khalid Simba, akizungumza katika 
mahafali hayo. Kutoka kulia ni Makamu Mkuu wa Shule, Ally Mkamba, Diwani wa Kata ya Chamazi, Hemedi Karata na Katibu wa Diwani.
 Taswira ya meza kuu kwenye mahafali hayo.
 Wahitimu wa kidato cha nne wakionesha vyeti vyao.
 Mahafali yakiendelea.
 Ndugu na Jamaa yake mhitimu Winfrida Komba wakiwa kwenye mahafali hayo.
 Walimu wa shule hiyo wakishiriki kwenye mahafali hayo.
 Wazazi na walezi wa wahitimu hao wakiwa kwenye mahafali hayo.
 Wahitimu hao wakionesha jinsi ya kujifunza somo la Sayansi.
 Wanafunzi wa shule hiyo wakipata burudani kupitia madirishani.
 Burudani zikiendelea kutolewa na wahitimu hao.
 Wageni waalikwa wakiwa kwenye sherehe hiyo.
 Katibu wa Diwani (kulia), akitoa vyeti kwa niaba ya diwani huyo.
 Mwanafunzi akikabidhiwa cheti na Katibu wa Diwani wa Kata ya Chamazi.
Katibu wa Diwani wa Kata ya Chamazi, akimkabidhi cheti mhitimu, Winfrida Komba katika mahafali hayo. Kulia ni Mkuu wa shule hiyo, Khalid Simba.




Na Dotto Mwaibale

WAHITIMU wa Kidato cha Nne mwaka 2016 katika Shule ya St. Emmanuel iliyopo Chamazi jijini Dar es Salaam wametakiwa kuzingatia elimu ili kutimiza ndoto za maisha yao badala ya kujihusisha na vitendo viovu na utoro.

Mwito huo umetolewa na Diwani wa Kata ya Chamazi, Hemedi Karata wakati akiwahutubia wanafunzi hao kwenye  mahafali ya saba ya kidato cha nne ya shule hiyo yaliyofanyika Dar es Salaam jana.

"Zingatieni masomo yenu ili mtimize ndoto za maisha yenu ya baadae, wazazi wenu wanawalipia ada ni vizuri mkawaonesha mafanikio yenu katika elimu na sio tabia mbaya," alisema Karata ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mahafali hayo.

Alisema kwa maisha ya leo bila ya kuwa na elimu kuna changamoto kubwa ya maisha hivyo aliwaasa wahitimu hao kufanya bidii ya kusoma hata watapokuwa kidato cha tano na sita na elimu ya juu.

Mkurugenzi Mtendaji wa shule hiyo, Ernest Masaka aliwaomba wazazi kushirikiana na uongozi wa shule katika kuwalea wanafunzi hao wawapo nyumbani na shuleni.

"Ushirikiano baina ya wazazi, wanafunzi na walimu ni muhimu sana katika kuwajengea wanafunzi mazingira mazuri ya kupata elimu bora hivyo nawaombeni tuendelee kushirikiana," alisema Masaka.

Mkuu wa shule hiyo, Khalid Simba alisema shule hiyo imekuwa ikifanya vizuri kutokana na ushirikiano uliopo kati ya wazazi, walimu na wanafunzi wenyewe.

Alisema licha ya shule hiyo kuwa na mafanikio, changamoto ndogo ndogo zinakuwepo lakini wanajitahidi kuzitatua kwa kushirikiana kwa pamoja na wazazi.




Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: WAHITIMU ST. EMMANUEL CHAMAZI TEMEKE JIJINI DAR ES SALAAM WAASWA KUZINGATIA ELIMU
WAHITIMU ST. EMMANUEL CHAMAZI TEMEKE JIJINI DAR ES SALAAM WAASWA KUZINGATIA ELIMU
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhRGjHuERssOwC3VggPurUj-429LayDuU2UiTW6mWqtuHAwfKXLwe5QD302Pt06LMRuOH4d7KhxWVEja6dWdUw6B6B5bDtV6WCHQic545sUR9wq1HGZsb1p3FtEo7sYfVtSDgQ0Kqqn8c_p/s640/1.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhRGjHuERssOwC3VggPurUj-429LayDuU2UiTW6mWqtuHAwfKXLwe5QD302Pt06LMRuOH4d7KhxWVEja6dWdUw6B6B5bDtV6WCHQic545sUR9wq1HGZsb1p3FtEo7sYfVtSDgQ0Kqqn8c_p/s72-c/1.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2016/10/wahitimu-st-emmanuel-chamazi-temeke.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/10/wahitimu-st-emmanuel-chamazi-temeke.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy