MPANGO WA GO FARMING KUBADILISHA MAISHA YA WAKULIMA WA ZABIBU NCHINI KUWA BORA

  Wakulima wakipalilia mashamba yao ya mizabibu mkoani Dodoma.     Mche wa mzabibu shambani kabla ya mavuno.   ...




 Wakulima wakipalilia mashamba yao ya mizabibu mkoani Dodoma.
 
 Mche wa mzabibu shambani kabla ya mavuno.
 
“Kwa muda mrefu wakulima wa zabibu mkoani Dodoma tumekuwa tukikabiliwa na changamoto mbalimbali kiasi kwamba licha ya kufanya kazi za kilimo hususani cha mazao ya biashara tumekuwa tukiendelea kukabiliwa na tatizo la kutopata faida na kubaki katika hali duni za kutuwezesha kupata mahitaji muhimu ya kukidhi mahitaji yetu ikiwemo kujenga nyumba bora na kusomesha watoto wetu”Anasema Yarendi Makuya, mkulima wa zabibu  kijiji cha Handala mkoani Dodoma.
 
 Anasema kuwa katika miaka ya karibuni kutokana na kuongezeka kwa wawekezaji katika sekta ya viwanda wakulima wa zabibu wameanza kupata ahueni ya maisha kutokana na wateja wanaowatembelea vijijini wakihitaji kununua zao  la zabibu wamekuwa wakiongezeka siku hadi siku hali inayotia matumaini kuwa kilimo cha zao hilo kina fursa ya kuchangia uchumi na kuinua maisha ya wakulima iwapo watawezeshwa ipasavyo.
 
Yarendi aliyekuwa akiongea kwa niaba ya wenzake alieleza kuwa hivi sasa baadhi ya makampuni yaliyowekeza kwenye viwanda  yameanza kujenga ukaribu na kushirikiana na wakulima ili yaweze kupata malighafi kwa ajili ya viwanda vyao na kuhakikisha uzalishaji wa zao hili unaongezeka.
 
 Moja ya kampuni aliyoitaja kuwa  hivi sasa imejikita katika kilimo shirikishi na wakulima wa zabibu na ushirikiano huo umeanza kuonyesha mafanikio ni kampuni ya Tanzania Distilleries Limited (TDL) maarufu kama Konyagi iliyopo chini ya TBL Group ambayo hivi sasa inashirikiana na wakulima kwa lengo la kuwawezesha  kuongeza uzalishaji wa zabibu kupitia mpango wa Go Farming na  wakati wa msimu inanunua zao hilo kwa bei nzuri na malipo kufanyika bila urasimu kama ilivyokuwa hapo awali walipokuwa wanauza zabibu kupitia vituo vya Ushirika na walanguzi wa mazao ambao kwa kiasi kikubwa walikuwa wakiwapunja  katika bei ya kuuzia.

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: MPANGO WA GO FARMING KUBADILISHA MAISHA YA WAKULIMA WA ZABIBU NCHINI KUWA BORA
MPANGO WA GO FARMING KUBADILISHA MAISHA YA WAKULIMA WA ZABIBU NCHINI KUWA BORA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi39D_zg_m9NOJ-JAUdDHrsAu4VoJYaQA-mAnFT-9XmlfAAv1-EExNrVTPJ-7jWf_ALIkKPs9wCXJGc7hx6-fNwpiU2XIz4PX25_bTjxvjPmpFfYQPXGz3X9b7m2pz56uzve6gU_JQc4Uqh/s640/ZABIBU+1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi39D_zg_m9NOJ-JAUdDHrsAu4VoJYaQA-mAnFT-9XmlfAAv1-EExNrVTPJ-7jWf_ALIkKPs9wCXJGc7hx6-fNwpiU2XIz4PX25_bTjxvjPmpFfYQPXGz3X9b7m2pz56uzve6gU_JQc4Uqh/s72-c/ZABIBU+1.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2016/08/mpango-wa-go-farming-kubadilisha-maisha.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/08/mpango-wa-go-farming-kubadilisha-maisha.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy