UJUMBE WA SKAUTI TANZANIA KWENDA KOREA KUSINI

Kamishina Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania, Abdulkarim Shah akizungumza katika hafla ya kukabidhi kukabidhi nyaraka za...




Kamishina Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania, Abdulkarim Shah akizungumza katika hafla ya kukabidhi kukabidhi nyaraka za kutagaza Utalii kwa ujumbe wa skauti utakaokwenda Korea Kusini.
 
Kaimu Mkurugenzi wa Masoko Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Philip Chitaunga (kushoto) akimkabidhi nyaraka za kutangaza utalii Mskauti Mkuu, Mwantumu Mahiza ambaye ataongoza ujumbe wa chama cha skauti Tanzania huko Korea ya Kusini. Kulia ni Kamishina Mkuu wa Skauti, Abdulkarim Shah.  
 Mskauti Mkuu, Mwantumu Mahiza ambaye ataongoza ujumbe wa chama cha skauti Tanzania huko Korea ya Kusini akizungumza katika hafla hiyo.
 Stakauti wakiimba nyimbo.
 Kaimu Mkurugenzi wa Masoko Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Philip Chitaunga (kushoto) akimkabidhi nyaraka za kutangaza utalii pamoja na bendera ya Taifa Mskauti Mkuu, Mwantumu Mahiza ambaye ataongoza ujumbe wa chama cha skauti cha Tanzania huko Korea ya Kusini. Kulia ni Kamishina Mkuu wa Skauti, Abdulkarim Shah.
Kaimu Mkurugenzi wa Masoko Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Philip Chitaunga (wa pili kushoto) akimkabidhi Bendera ya Taifa kutangaza utalii pamoja Skauti Mkuu, Mwantumu Mahiza. Kulia ni Kamishina Mkuu wa Skauti, Abdulkarim Shah na Kushoto ni Ofisa Mawasiliano Mkuu wa TTB, Geofrey Tengeneza.

TAARIFA FUPI YA KAMISHNA MKUU WA CHAMA CHA SKAUTI TANZANIA ILIYOTOLEWA TAREHE 27/07/2016 KWENYE HAFLA FUPI ILIYOFANYIKA KWENYE VIWANJA VYA MAKAO MAKUU YA CHAMA CHA SKAUTI TANZANIA UPANGA YA KUUKABIDHI UJUMBE WA CHAMA CHA SKAUTI TANZANIA NYARAKA ZA KUTANGAZA UTALII WATAKAPOKUWA SAFARINI HUKO KOREA YA KUSINI

Viongozi wetu wote wa juu wa  nchi hii kwa vipindi tofauti wamekuwa  wakizungumzia maisha bora kwa wananchi wake. Rais wetu wa awamu ya tano, Mhe. John Pombe Magufuli hali kadhalika anazungumzia maisha bora na yenye neema kwa raia wake. Ametuambia mara nyingi anataka kuigeuza nchi yetu kuwa ya viwanda vitakavyoongeza ajira kwa vijana na hatimae nchi yetu iweze kuwa miongoni mwa nchi wahisani. Hii ndio ndoto ya Rais wetu wa awamu ya tano.

Chama cha Skauti Tanzania kina dhima ya malezi ya watoto na vijana. Malengo makuu ya Chama hiki ni kuwaendeleza watoto na vijana kimwili, kiakili, kihisia, kijamii na kiroho na wakati huo watoto na vijana hawa wawe raia wema na wazalendo wa kweli wa nchi hii wenye manufaa kwa Taifa lao na watu wake.

Chama cha Skauti Tanzania kinatekeleza dhima yake kwa dhamira kubwa na ya kweli. Chama kinalea watoto na vijana ambao hatimae wanakua wenye afya bora, jasiri na wenye uthubutu. Vijana hawa wanaweza kuaminika katika utumishi wa umma na hata sekta binafsi. 

Wanaweza kulitumikia Taifa lao kwenye vyombo vyetu vya ulinzi na usalama kwa uzalendo wa hali ya juu, kwenye Wizara na idara za Serikali Kuu na za Mitaa, mashirika ya Umma na Sekta binafsi kwa uaminifu mkubwa. Aidha sifa moja kubwa walionayo vijana hawa ni kujituma katika shughuli za kijamii kwa njia ya kujitolea. 

Vijana wetu tuliowaandaa wana mchango mkubwa sana katika kuifikisha jamii kwenye ndoto za viongozi wetu wa nchi.  Tuwape nafasi na tuwatume na watatumika bila kinyongo na watatoa matokeo chanya tarajiwa.

Skauti ni vugu vugu la vijana la Kimataifa. Wapo Skauti kwenye nchi zipatazo 216 duniani. Vyama vya Skauti vya Nchi mbali mbali vina taratibu za kualikana kwa shughuli mbali mbali. Mwaka huu Desemba Tanzania inatarajia kuwa mwenyeji wa mashindano ya Kanda ya Afrika Mashariki na vile vile kuwa na Mkutano Mkuu wa Kanda utakaojumuisha nchi za Ethiopia, Sudani ya Kusini, Uganda, Kenya, Rwanda, Burundi na mwenyeji Tanzania. Hapa watakutana Skauti na viongozi wasiopungua 400.

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: UJUMBE WA SKAUTI TANZANIA KWENDA KOREA KUSINI
UJUMBE WA SKAUTI TANZANIA KWENDA KOREA KUSINI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhoaGRaJFtHpzCQDIDZkiumO6INtY5djgAmLVYgSz7cpLf4uuMtWvpyPwsFI4u5k8ndPBysmeMRsjSdPfLLNMToSIzzSADIOL6hHuPRIFQGmCDNcKCcUvZEtDq5J4q01sXXAcsP667YH_Y/s640/IMG_3416.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhoaGRaJFtHpzCQDIDZkiumO6INtY5djgAmLVYgSz7cpLf4uuMtWvpyPwsFI4u5k8ndPBysmeMRsjSdPfLLNMToSIzzSADIOL6hHuPRIFQGmCDNcKCcUvZEtDq5J4q01sXXAcsP667YH_Y/s72-c/IMG_3416.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2016/07/ujumbe-wa-skauti-tanzania-kwenda-korea.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/07/ujumbe-wa-skauti-tanzania-kwenda-korea.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy