Wabunge wa bunge la Afrika Mashariki kutoka Tanzania, na wafanyakazi wa Clouds Media Group, akiwemo mchekeshaji maarufu Bishang...
Wabunge wa bunge la Afrika Mashariki kutoka Tanzania, na wafanyakazi wa Clouds Media Group, akiwemo mchekeshaji maarufu Bishanga Bashaija, wakiwa kwenye moja ya studio za Clouds Media Group, wakati wa kipindi maarufu cha Leo Tena, Aprili 22, 2016.
NA
K-VIS MEDIA/Khalfan Said
K-VIS MEDIA/Khalfan Said
WABUNGE wa bunge la Afrika Mashariki (EALA), kutoka Tanzania, wametembelea Clouds Media Group,Mikocheni jijini Dar es Salaam Aprili 22, 2016 ikiwa ni sehemu
ya ziara yao ya takriban siku 20 kutembelea vyombo vya habari kwa nia ya kuvishirikisha vyombo hivyo kutoa elimu kwa wananchi kuchangamkia fursa zilizopo kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki.
ya ziara yao ya takriban siku 20 kutembelea vyombo vya habari kwa nia ya kuvishirikisha vyombo hivyo kutoa elimu kwa wananchi kuchangamkia fursa zilizopo kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group, inayomiliki kituo cha radio, Clouds FM, Clouds TV, Bw. Ruge Mutahaba, amewaeleza wabunge hao walioongozwa na mwenyekiti wao Mh. Chrles Makongoro Nyerere kuwa, Tanzania inakabiliwa na tatizo kubwa la kutogeuza vipaji kuwa biashara na hivyo kujiingizia kipato.
Ruge amewahimiza wabunge hao kushawishi serikali ya Tanzania kurekebisha sera zake za kuwawezesha wananchi na kuwajengea uwezo wa kuvitumia vipaji walivyojaaliwa
na Mwenyezimungu ili kujiingizia kipato.
na Mwenyezimungu ili kujiingizia kipato.
Akielezea nia ya ziara hiyo, Mwenyekii Mh. Makongoro Nyerere alisema, wabunge kutoka nchi wanachama walipewa jukumu la kuwatembelea wananchi wa nchi watokako ili kwahimiza
kuchangamkia fursa zilizopo kwenye Jumuiya hiyo ambayo kwa sasa ina jumla ya wanachama sita, Tanzania, Kenya Uganda, Rwanda, Burundi na Sudani Kusini.
kuchangamkia fursa zilizopo kwenye Jumuiya hiyo ambayo kwa sasa ina jumla ya wanachama sita, Tanzania, Kenya Uganda, Rwanda, Burundi na Sudani Kusini.
“Jumuiya ya Afrika Mashariki ina soko la kutosha na wananchi wa Jumuiya hii wanyo fursa ya kwenda kufanya shughuli za kiuchumi bila kizuizi chochote ikiwemo biashara na kufanya kazi hivyo ni wakati wa watanzania kuacha kulalamika na kuchangamkia
fursa hiyo.” Alisema Mh. Makongoro.
fursa hiyo.” Alisema Mh. Makongoro.
Pamoja na Mh. Makongoro, wabunge wengine ni pamoja na Mh. Shy-Rose Bhanji, na Mh. Nderakindo Kessy.
Mtangazaji wa kipindi cha Leo Tena, Gea Habib.
Mwenyekiti Mh. Charles Makongozo Nyerere (kulia) akizungumza kwenye kipindi cha Leo tena.
Mh. Shy-Rose Bhanji mkutanoni
Mh. Nderakindo Kessy akiwa mkutanoni.
Mtangazaji wa kipindi cha Leo Tena Husna Abdul "DAHUU".
Mchekeshaji maarufu Bishanga Bashaija (kulia), akiwa katika kipindi cha Leo Tena aprili 22, 2016.
Dahuu.
Bi. Gea.
Mwenyekiti Mh. Charles Mkongoro Nyerere akizungumza kwenye kikao cha kubadilishana mawazo na uongozi wa Clouds Media Group.
Mh. Shy-Rose Bhanji, akizungumza kwenye kikao hicho.














COMMENTS