SAMUEL SITTA, "MZEE WA SPEED NA VIWANGO" HATUNAYE TENAI, AFARIKI DUNIA AKIWA KWENYE MATIBABU NCHINI UJERUMANI

 Spika wa bunge mstaafu, Samuel Sitta, au kama alivyojiita "Mzee wa Speed na Viwango" amefariki du...







 Spika wa bunge mstaafu, Samuel Sitta, au kama alivyojiita "Mzee wa Speed na Viwango" amefariki dunia usiku wa kuamkia leo akiwa nchini Ujerumani alikopelekwa kupatiwa matibabu. Taarifa iliyotolewa na mwanaye Benjamin Sitta, ambaye ni Meya wa Manispaa ya Kinondoni, mapema leo aimethibitisha kifo cha Mzee Sitta. Tayari Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, amemtumia salamu za rambirambi spika wa bunge Job Ndugai, kufuatia kifo cha mzee Sitta. Kwa muda mrefu Samuel Sitta ambaye aliwahi kutumikia nyadhifa mbalimbali tangu serikali ya awamu ya kwanza, alikuwa haonekani hadharani kutokana na kuugua. Ni miezi michache iliyopita Mzee Sitta alikuwa akionekana kwenye vyombo vya habari akitembeelwa na viongozi mbalimbali kumjulia hali. Mungu aiweke roho ya marehemu mahali pema peponi AMIN.







JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULUDescription: Description: Description: Description: Description: Coat of Arms
Simu: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: press@ikulu.go.tz
Tovuti : www.ikulu.go.tz               

Faksi: 255-22-2113425



OFISI YA RAIS,
     IKULU,
1 BARABARA YA BARACK OBAMA,   
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai kufuatia kifo cha Spika Mstaafu na Mbunge Mstaafu wa Jimbo la Urambo lililopo Mkoani Tabora Mhe. Samwel Sitta.
Mhe. Samuel Sitta amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika hospitali ya Technical University of Munich nchini Ujerumani alikokuwa akipatiwa matibabu tangu mwezi uliopita.
Katika salamu hizo, Rais Magufuli amesema amepokea kwa mshtuko na masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Mhe. Samwel Sitta na kwamba Taifa limempoteza mtu muhimu aliyetoa mchango mkubwa katika uongozi na maendeleo.
“Nitamkumbuka Mzee Sitta kwa uchapakazi wake, uzalendo wake na tabia yake ya kusimamia ukweli katika kipindi chote alichokuwa kiongozi katika ngazi mbalimbali za siasa na Serikali.
“Kupitia kwako Mhe. Spika naomba kutoa pole nyingi kwa Mke wa Marehemu Mhe. Magreth Sitta ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Urambo na familia nzima ya marehemu, Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wananchi wa Urambo Mkoani Tabora na watu wote walioguswa na msiba huu” amesema Rais Magufuli katika salamu hizo.
Dkt. Magufuli amesema anaungana na wafiwa wote katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo na amewaombea moyo wa uvumilivu na ustahimilivu.
“Namuomba Mwenyezi Mungu aiweke roho ya Marehemu mahali pema peponi, Ameni”

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
07 Novemba, 2016



  Samuel Sitta akiwa na mkewe, Mama Margaret Sitta wakati wa uhai wake.


 Spika Sitta, akipokea ripoti maarufu ya Richmond, kutoka kwa mwenyekiti wa kamati teule, Dkt. Harrison Mwakyembe. Ripoti hii ilimuondoa madarakani aliyekuwa Waziri Mkuu wakati wa kuingia kwa serikali ya awamu ya nne, Mh. Edward Lowassa.


 Mzee Sitta alikuwa rafiki wa kila mtu. Hapa akiwa na Mbunge Tundu Lissu kutoka CHADEMA.




 Spika Samuel Sitta, akila kiapo cha kushika uspika wa bunge, mwanzoni mwa serikali ya awamu ya nne.

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: SAMUEL SITTA, "MZEE WA SPEED NA VIWANGO" HATUNAYE TENAI, AFARIKI DUNIA AKIWA KWENYE MATIBABU NCHINI UJERUMANI
SAMUEL SITTA, "MZEE WA SPEED NA VIWANGO" HATUNAYE TENAI, AFARIKI DUNIA AKIWA KWENYE MATIBABU NCHINI UJERUMANI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg9LzeSYV8cWvyhyxp3y82-ri1gxHmJRILA0VoypO5Z0AMVTWaa9F3FaOYRr2bwyTCFqTCtOd1CYVtVXhcIQ2TnJ_lA223YxyhJiDeqjDI-kN4F9pJkrR7T-HQVNj5tpNdColFk3RzueUY/s640/bunge3.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg9LzeSYV8cWvyhyxp3y82-ri1gxHmJRILA0VoypO5Z0AMVTWaa9F3FaOYRr2bwyTCFqTCtOd1CYVtVXhcIQ2TnJ_lA223YxyhJiDeqjDI-kN4F9pJkrR7T-HQVNj5tpNdColFk3RzueUY/s72-c/bunge3.jpg
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2016/11/samwel-sitta-mzee-wa-speed-na-viwango.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/11/samwel-sitta-mzee-wa-speed-na-viwango.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy