SERIKALI YA ISRAEL YAAHIDI KUENDELEA KUPANUA WIGO KATIKA MIRADI YAKE NCHINI IKIWEMO MIRADI YA AFYA
Waziri wa Sheria wa Israel Mhe. Aleyet Shaked akiagana na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi mara baada ya kumaliza ziara yake ya kikazi jana ya kuona ushirikiano uliopo wa matibabu ya moyo kwa watoto kati ya JKCI na Taasisi ya Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child’s Heart – SACH) ya nchini Israel. Kulia ni Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Mohammed Kambi.

HomeJamii

SERIKALI YA ISRAEL YAAHIDI KUENDELEA KUPANUA WIGO KATIKA MIRADI YAKE NCHINI IKIWEMO MIRADI YA AFYA

Na Mwandishi Maalum Serikali ya Israel imeahidi kuendelea kupanua wigo katika miradi yake mbalimbali iliyopo hapa nchini ikiwemo ...




Na Mwandishi Maalum
Serikali ya Israel imeahidi kuendelea kupanua wigo katika miradi yake mbalimbali iliyopo hapa nchini ikiwemo miradi ya afya ili  iweze kuwafikia wananchi wengi zaidi.
Ahadi hiyo imetolewa jana na  Waziri wa Sheria wa nchi hiyo Mhe. Aleyet Shaked alipotembeleaTaasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ili kuona ushirikiano uliopo kati ya Taasisi hiyo na Taasisi ya Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child’s Heart – SACH) ya nchini humo.
Mhe. Shaked alisema kuwa kwa upande wa afya katika Taasisi ya Moyo wamekuwa wakifanya matibabu ya moyo kwa watoto na katika siku za baadaye wataangalia namna ya kuongeza huduma hiyo ili iweze kuwasaidia watu wengi zaidi
“Nikirudi nyumbani nitafanya majadiliano na waziri wa Afya na kumpa  mrejesho wa miradi tunayoifanya hapa nchini, nitamuomba   kuendeleza kukuza uhusiano uliopo kwa kupanua wigo wa miradi yetu  kwenye maeneo mengine ya afya katika  sehemu zingine za nchi hii itasaidia  kuweza kufikia watu wengi zaidi.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI Prof.  Mohamed Janabi alisema  kabla ya kuanzishwa kwa Taasisi hiyo mwaka 2015 asilimia 65 ya upasuaji wa moyo kwa watoto ulikua unafanywa na madaktari wa nje kwa kushirikiana na watanzania.
 Hivi sasa  madaktari wa Taasisi hiyo wanafanya upasuaji wa moyo kwa watoto kwa asilimia 70 na asilimia 30 inafanywa  kwa ushirikiano na wageni wanaokuja katika  kambi maalum za matibabu hii ni kutokana na upasuaji mwingine kuhitaji  utaalam wa juu zaidi.
“Tangu tumeanza kufanya kazi kama Taasisi mwaka 2015 hadi sasa tumeshafanya upasuaji wa moyo kwa  watoto 400 na asilimia 70 ya hao watoto wamefanyiwa na daktari wetu bingwa wa upasuaji wa Moyo kwa watoto Godwin Sharau ambaye amesoma nchini Israel”, alisema  Prof. Janabi.


Mwaka 2015 Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete ilianza ushirikiano na SACH  kwa kusomesha madaktari na wauguzi na kufanya  kambi maalum za matibabu ya moyo kwa watoto ambapo watoto wanaokutwa na matatizo yanayohitaji matibabu ya hali ya juu wanatibiwa nchini Israel bila malipo.



Waziri wa Sheria wa Israel Mhe. Aleyet Shaked akiwa katika picha ya pamoja na viongozi  wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) mara baada ya kumaliza ziara ya kikazi jana katika Taasisi hiyo. Mhe. Shaked alitembelea Taasisi hiyo jana kwa ajili ya kuona ushirikiano ulipo wa matibabu ya moyo kwa watoto, kusomesha madaktari na wauguzi kati  ya JKCI na Taasisi ya Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child’s Heart – SACH) ya nchini Israel.


Waziri wa Sheria wa Israel Mhe. Aleyet Shaked akiangalia makala ya video inayoonyesha matibabu ya moyo kwa watoto yanayofanywa na madaktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya  Moyo Jakaya Kikwete kwa kushirikiana na wenzao wa Taasisi ya Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child’s Heart – SACH) ya nchini Israel. Tangu mwaka 2015 JKCI kwa kushirikiana na SACH ya nchini Israel wanafanya kambi maalum ya matibabu ya moyo kwa watoto ambapo watoto wanaokutwa na matatizo wanatibiwa hapa nchini na wanaokutwa na matatizo yanayohitaji matibabu ya hali ya juu wanatibiwa nchini humo bila malipo.


Waziri wa Sheria wa Israel Mhe. Aleyet Shaked akisaini kitabu cha wageni alipotembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) jana kwa ajili ya kuona ushirikiano ulipo wa matibabu ya moyo kwa watoto, kusomesha madaktari na wauguzi kati  ya JKCI na Taasisi ya Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child’s Heart – SACH) ya nchini Israel. Kushoto ni Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Mohammed Kambi na kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi.


Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akiongea na waandishi wa Habari mara baada ya kumalizika kwa ziara ya  Waziri wa Sheria wa Israel Mhe. Aleyet Shaked alipotembelea Taasisi hiyo jana kwa ajili ya  kuona ushirikiano ulipo wa matibabu ya moyo kwa watoto, kusomesha madaktari na wauguzi kati  ya JKCI na Taasisi ya Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child’s Heart – SACH) ya nchini Israel. (Picha na JKCI)


Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: SERIKALI YA ISRAEL YAAHIDI KUENDELEA KUPANUA WIGO KATIKA MIRADI YAKE NCHINI IKIWEMO MIRADI YA AFYA
SERIKALI YA ISRAEL YAAHIDI KUENDELEA KUPANUA WIGO KATIKA MIRADI YAKE NCHINI IKIWEMO MIRADI YA AFYA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiX9TLFlqgXe61woTHKt90NwLIFF8GNY3wcx1eelsRknrCIPrPqSAqpFUS6_hC7Lkw_Ej8iWezPxMXHHeM5U-xDUKC546rWElW09CMYkIFVJyx-qpgDNqL6Uvr7NmxPVjIiMzhMwe5I0ZI/s640/Picha+no.+1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiX9TLFlqgXe61woTHKt90NwLIFF8GNY3wcx1eelsRknrCIPrPqSAqpFUS6_hC7Lkw_Ej8iWezPxMXHHeM5U-xDUKC546rWElW09CMYkIFVJyx-qpgDNqL6Uvr7NmxPVjIiMzhMwe5I0ZI/s72-c/Picha+no.+1.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2018/04/serikali-ya-israel-yaahidi-kuendelea.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2018/04/serikali-ya-israel-yaahidi-kuendelea.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy