Waheshimiwa Dkt. Mahiga na Dkt. Kolimba kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Wabunge wa Bunge la Nne la Afrika Mashariki. Kulia kwa Waziri Ma...
Waheshimiwa Dkt. Mahiga na Dkt. Kolimba kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Wabunge wa Bunge la Nne la Afrika Mashariki. Kulia kwa Waziri Mahiga ni Mwenyekiti wa Wabunge hao Mhe. Dkt. Abdullah Makame. Wengine waliosimama kutoka kushoto ni Mhe. Dkt. Ngwaru Maghembe, Mhe. Happiness Lugiko, Mhe. Mhandisi Mohamed Habib Mnyaa, Mhe. Pamela Maasay na Mhe. Adam Kimbisa.

Balozi Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akifungua Semina Elekezi kwa Wabunge wa Tanzania wa Bunge la Nne la Afrika Mashariki iliyofanyika kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere tarehe 19-20 Januari, 2018.

Waheshimiwa Dkt. Mahiga na Dkt. Kolimba kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Wakurugenzi na maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Waheshimiwa Wabunge wa Bunge la Nne la Afrika Mashariki kwenye Semina elekezi iliyoandaliwa na Wizara kwa lengo la kuwaongezea uzoefu Wabunge hao.

Mheshimiwa Adam Kimbisa akisalimiana na Mheshimiwa Dkt. Mahiga wakati wa Semina hiyo ya siku mbili iliyofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere tarehe 19-20 Januari, 2018.

Dkt. Suzan Kolimba, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akiwatambulisha baadhi ya Wakurugenzi wa Wizara hiyo kwa Wabunge wa Tanzania wa Bunge la Afrika Mashariki wakati wa Semina elekezi iliyoandaliwa na Wizara kwa ajili ya Wabunge hao.

Mheshimiwa Pamela Maasay akijitambulisha wakati wa Semina elekezi ya Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki.

Mheshimiwa Mhandisi Mohamed Habib Mnyaa akijitambulisha wakati wa Semina elekezi ya Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki

Mheshimiwa Dkt. Ngwaru Maghembe akijitambulisha wakati wa Semina elekezi ya Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki

Wajumbe wa Semina hiyo wakimsikiliza Mheshimiwa Dkt. Mahiga wakati wa ufunguzi wa Semina ya siku mbili ya kuwaongezea uwezo Wabunge wa Tanzania watakaowakilisha nchi kwenye Bunge la Nne la Afrika Mashariki.
COMMENTS