KING MAJUTO AMFAGILIA RAIS MAGUFULI, AFARIJIKA BAADA KUTEMBELWA NAYE AKIWA HOSPITALINI
Homedijital

KING MAJUTO AMFAGILIA RAIS MAGUFULI, AFARIJIKA BAADA KUTEMBELWA NAYE AKIWA HOSPITALINI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU Simu: 255-22-2114512, 2116898 E-mail: press@ikulu.go.tz ...

MAKALA MAALUM YA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII
MAELEZO TV:WATANZANIA WATAKIWA KUACHA KUTUMIA VIPODOZI VISIVYOKUWA NA KIWANGO
BBC DIRA YA DUNIA JUMATANO 31.01.2018


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULUDescription: Description: Description: Description: Description: Coat of Arms
Simu: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: press@ikulu.go.tz
Tovuti : www.ikulu.go.tz               

Faksi: 255-22-2113425


OFISI YA RAIS,
     IKULU,
1 BARABARA YA BARACK OBAMA,   
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 31 Januari, 2018 amewajulia hali wagonjwa waliolazwa katika Hospitali ya Tumaini Jijini Dar es Salaam akiwemo muigizaji mkongwe nchini Mzee Amri Athuman, maarufu kwa jina la “King Majuto”.
Mhe. Rais Magufuli ambaye ameongozana na Mkewe Mhe. Mama Janeth Magufuli, amewajulia hali wagonjwa waliolazwa katika wodi namba 3 hadi namba 8 na baadaye akamuona King Majuto ambaye anaendelea kupata matibabu ya tezi dume.
King Majuto amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kwenda hospitali kumuona na amempongeza kwa namna anavyosimamia huduma za afya nchini, kwani tangu maradhi yalipomuanza amehudumiwa vizuri na ana matumaini ya kupona na kurejea katika majukumu yake ya kila siku.
Aidha, King Majuto amemuombea Mhe. Rais Magufuli ili aendelee kutekeleza majukumu yake ya kuongoza nchi vizuri, na amebainisha kuwa hatua zinazochukuliwa na Serikali ya Awamu ya Tano zimerejesha nidhamu, zimeongeza uchapakazi, zimesaidia kukabiliana na wizi na zimeongeza heshima ya nchi.
“Kiongozi lazima awe namna hii, sio kuleta mzahamzaha, ukisema jambo watu wanatekeleza, wezi wanakamatwa, wala rushwa wanakamatwa, wenye vyeti feki hata kama amefanya kazi miaka 20 fukuza, hii safi, sasa kuna heshima na watu wanachapa kazi, ndio maana mimi hata wakati wa kampeni niliwaambia wasanii wenzangu hapa Rais ni Magufuli” amesema King Majuto.


Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

31 Januari, 2018



Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: KING MAJUTO AMFAGILIA RAIS MAGUFULI, AFARIJIKA BAADA KUTEMBELWA NAYE AKIWA HOSPITALINI
KING MAJUTO AMFAGILIA RAIS MAGUFULI, AFARIJIKA BAADA KUTEMBELWA NAYE AKIWA HOSPITALINI
https://lh5.googleusercontent.com/HvJ5S_lcIDl5db3l2zYdiPX22_BFZmeIHD8DMmhBhaBTNs8Wa0LCxIMXlgcxIlSAi2x7Yun3Mww1QAheDefY4W6KQOjB-JXDfuYgmi9ocpCToSAWNv8AC0h6TMwomDnMTof_DCosVSjxqSvhUw
https://lh5.googleusercontent.com/HvJ5S_lcIDl5db3l2zYdiPX22_BFZmeIHD8DMmhBhaBTNs8Wa0LCxIMXlgcxIlSAi2x7Yun3Mww1QAheDefY4W6KQOjB-JXDfuYgmi9ocpCToSAWNv8AC0h6TMwomDnMTof_DCosVSjxqSvhUw=s72-c
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2018/01/king-majuto-amfagilia-rais-magufuli.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2018/01/king-majuto-amfagilia-rais-magufuli.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy