MAMIA WAMUAGA MWANAHABARI JOYCE MMASI JIJINI DAR ES SALAAM
HomeJamii

MAMIA WAMUAGA MWANAHABARI JOYCE MMASI JIJINI DAR ES SALAAM

  Marehemu Joyce Mmasi enzi za uhai wake.   Waombolezaji wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa mwanahabari Joyce wakati ukiwasili...

RC MAKONDA ATAJA MAMBO MAKUU MANNE KUKABILIANA NA UHALIFU JIJINI DAR ES SALAAM
MAADHIMISHO YA SIKU YA MTOTO WA AFRIKA TAARIFA YA THBUB KWA VYOMBO VYA HABARI
WADAU WA JOTOARDHI WAKUTANA JIJINI DAR ES SALAAM LEO




 Marehemu Joyce Mmasi enzi za uhai wake.
 Waombolezaji wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa mwanahabari Joyce wakati ukiwasili viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salaam leo kwa ibada ya kuuaga kabla ya kuelekea mkoani Kilimanjaro kwa mazishi.
 Waombolezaji wakiwa kwenye ibada hiyo.
 Wanahabari wakiwa kwenye ibada hiyo.
 Wadau mbalimbali wakiwa kwenye ibada hiyo.
 Mchungaji Kulwa wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, akiongoza ibada hiyo.
 Katibu Tawala wa Wilaya ya Kigamboni, Rachel Mhando akizungumza kwenye ibada hiyo.
 Mbunge wa Viti Maalumu, Suzan Lyimo akizungumza. Lyimo na marehemu Mmasi wanatoka kijiji kimoja.
 Familia ya marehemu ikiwa katika ibada hiyo. Kulia ni mtoto wa kwanza wa marehemu, Lawrence Nicky Mayella.
 Mume wa marehemu Joyce Mmasi, Andrew Kamugisha akizungumza kwenye ibada hiyo.


Rafiki wa marehemu Mashaka Mgeta, akizungumzia maisha ya Joyce na jinsi alivyomfahamu.



 Waandishi wa habari wanawake wanaounda kikundi cha Wawata wakitoa neno katika ibada hiyo.
 Mwanahabari Hellen Mwango akisaidiwa baada ya kupoteza fahamu.
 Mtoto mkubwa wa marehemu,  Lawrence Nicky Mayella, akisoma Historia ya mama yake.
 Mwenyekiti wa kamati ya mazishi, Thomson, akizungumza katika ibada hiyo.
 Waombolezaji wakiwa katika foleni ya kwenda kutoa heshima za mwisho mbele ya jeneza lenye mwili wa marehemu.
Foleni ya kwenda kutoa heshima za mwisho.

Na Dotto Mwaibale

VILIO Majonzi na simanzi vilitawala   wakati wa ibada ya kuuaga mwili wa mwanahabari nguri Joyce Mmasi iliyofanyika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo.

Katika ibada hiyo mamia ya wakazi wa Jiji la Dar es Salaam, wanahabari na wadau wengine walijitokeza katika viwanja hivyo kwa ajili ya kumuaga mpendwa wao Joyce Mmasi ambaye alikuwa akifanyia kazi katika gazeti la Mwananchi.

Mchungaji Kulwa kutoka Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), ambaye aliongoza ibada hiyo aliwaambia watu waliokuwepo kwenye ibada hiyo kuwa wanapaswa kujitayarisha wakati wote kwani hawajui ni lini wataondoka hapa duniani.

"Mwenzetu Joyce ametutangulia tulikuwa naye pamoja lakini wewe uliye hai leo hii umejiandaeje katika maisha ya kiroho?" alisema Mchungajia Kulwa.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Kigamboni, Rachel Mhando alisema kifo cha Mmasi kimemshitua kila mtu na wanahabari wamepata pigo la kumpoteza mwenzao.

Mhando alihimiza kudumisha upendo kwa watu wote pamoja na wanahabari.

Katika ibada hiyo makundi mbalimbali yalijitokeza kutoa salamu za rambirambi na kuhudhuriwa na viongozi wa dini, siasa, serikali na wadau wengine.

Mwili wa marehemu Joyce umesafirishwa kwenda mkoani Kilimanjaro nyumbani kwao kwa mazishi.

Marehemu ameacha mume na watoto watatu, Mungu ailaze mahali pema roho ya marehemu.

(Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com-simu namba 0712727062)
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: MAMIA WAMUAGA MWANAHABARI JOYCE MMASI JIJINI DAR ES SALAAM
MAMIA WAMUAGA MWANAHABARI JOYCE MMASI JIJINI DAR ES SALAAM
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhzPIL_VF1PLmANBQ5FVUkuiIU7ZdUAr2i2Ab5aWLsRGUMKkv1uiw3-b7k2LbKCcUjjuCmmnizpe7_AVqABXbk141pOAVsBRAtUStptQMiVSMeTtnPXaV0qT_flzoNEwEceyiP_LdAhxDA2/s640/11.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhzPIL_VF1PLmANBQ5FVUkuiIU7ZdUAr2i2Ab5aWLsRGUMKkv1uiw3-b7k2LbKCcUjjuCmmnizpe7_AVqABXbk141pOAVsBRAtUStptQMiVSMeTtnPXaV0qT_flzoNEwEceyiP_LdAhxDA2/s72-c/11.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/12/mamia-wamuaga-mwanahabari-joyce-mmasi.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/12/mamia-wamuaga-mwanahabari-joyce-mmasi.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy