MHE DKT. MWANJELWA AMNADI MGOMBEA UDIWANI KATA YA IBIGI, APOKEA WANACHAMA WAPYA 21
HomeSiasa

MHE DKT. MWANJELWA AMNADI MGOMBEA UDIWANI KATA YA IBIGI, APOKEA WANACHAMA WAPYA 21

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhe Mary Mwanjelwa (Mnec) ambaye ni Naibu Waziri wa kilimo akimnadi Mgombea Udiwani K...







Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhe Mary Mwanjelwa (Mnec) ambaye ni Naibu Waziri wa kilimo akimnadi Mgombea Udiwani Kata ya Ibigi Wilayani Rungwe Mkoa wa Mbeya Bi Suma Ikenda Fyandomo, Jana Novemba 20, 2017. Picha Zote Na Mathias Canal

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhe Mary Mwanjelwa (Mnec) ambaye ni Naibu Waziri wa kilimo akimvalisha kofia ya CCM kijana aliyehama Chadema wakati wa kampeni za Udiwani Kata ya Ibigi Wilayani Rungwe Mkoa wa Mbeya Bi Suma Ikenda Fyandomo, Jana Novemba 20, 2017.


Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhe Mary Mwanjelwa (Mnec) ambaye ni Naibu Waziri wa kilimo akifurahi na wananchama wa CCM wakati wa mkutano wa kumnadi Mgombea Udiwani Kata ya Ibigi Wilayani Rungwe Mkoa wa Mbeya Bi Suma Ikenda Fyandomo, Jana Novemba 20, 2017.

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhe Mary Mwanjelwa (Mnec) ambaye ni Naibu Waziri wa kilimo akifurahi na wananchama wa CCM wakati wa mkutano wa kumnadi Mgombea Udiwani Kata ya Ibigi Wilayani Rungwe Mkoa wa Mbeya Bi Suma Ikenda Fyandomo, Jana Novemba 20, 2017.

Na Mathias Canal, Mbeya


Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhe Mary Mwanjelwa (Mnec) ambaye ni Naibu Waziri wa Kilimo amewasihi wananchi kwa kauli moja kuchagua kiongozi makini anayetokana na CCM.


Mhe Mwanjelwa alisema kuwa kumchagua diwani wa CCM ni dalili nzuri ya kumpongeza na kuunga mkono juhudi za Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli anazozifanya kwa muktadha wa kuwaletea maendeleo watanzania wote.


Mjumbe huyo wa NEC, aliyasema hayo Leo Novemba 20, 2017 katika Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Bujinga A na B kilichopo Kata ya Ibigi, Wilayani Rungwe Mkoa wa Mbeya ambapo alimnadi mgombea Udiwani wa Kata hiyo Bi Suma Ikenda Fyandomo.


(Mnec), Mhe Mwanjelwa aliwakumbusha wananchi waliojitokeza katika mkutano huo kuwa Hawachagui ilani mpya Bali wanachagua Diwani kwa ajili ya kutekeleza ilani ya Ushindi ya CCM ya Mwaka 2015-2020 ambayo wananchi waliiamini na kuichagua Octoba 25, 2015.


Alisema kuwa nchini Tanzania hakuna chama chenye uwezo wa kuwaletea maendeleo wananchi Bali Chama Cha Mapinduzi pekee ndicho chenye uwezo na jukumu la kuwaletea maendeleo endelevu wananchi.


Katika Mkutano huo wanachama 21 walivutiwa na hotuba ya Mjumbe huyo wa Halmashauri kuu ya CCM wakati akimnadi mgombea hivyo kufanya maamuzi ya kujivua uanachama wa CHADEMA na kujiunga na CCM ambapo wameahidi kushirikiana na mgombea udiwani wa CCM ili kuhakikisha anashinda kwa kishindo.


Ushiriki wa kampeni hizo katika Kata ya Ibigi unajili wakati ambapo Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa yupo ziarani Mkoani Mbeya ambapo pamoja na mambo mengine Kesho Disemba 21, 2017 atashiriki ufunguzi wa Mkutano wa Makatibu Tawala na washauri wa kilimo wa Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini juu ya mfumo wa ununuzi wa mbolea (BPS).


Mkutano huo utafanyika katika Ukumbi wa Benjamini Mkapa Jijini Mbeya.
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: MHE DKT. MWANJELWA AMNADI MGOMBEA UDIWANI KATA YA IBIGI, APOKEA WANACHAMA WAPYA 21
MHE DKT. MWANJELWA AMNADI MGOMBEA UDIWANI KATA YA IBIGI, APOKEA WANACHAMA WAPYA 21
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEilFxhotMR3ertwD6HHVCv6c-2wqN3pL5bywKTcj_TOGmQ-OV0Dj91BN9qIHY28hAh9GfOPz11r5LqvmVMqU3dUwUobzq9V4xGeZ4Llkqgn3gYUYMEo3tSnwAFvge_0zaWOLQhvEOBEolBu/s640/IMG_2182.CR2
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEilFxhotMR3ertwD6HHVCv6c-2wqN3pL5bywKTcj_TOGmQ-OV0Dj91BN9qIHY28hAh9GfOPz11r5LqvmVMqU3dUwUobzq9V4xGeZ4Llkqgn3gYUYMEo3tSnwAFvge_0zaWOLQhvEOBEolBu/s72-c/IMG_2182.CR2
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/11/mhe-dkt-mwanjelwa-amnadi-mgombea.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/11/mhe-dkt-mwanjelwa-amnadi-mgombea.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy