BANCABC YASHIRIKIANA NA KITENGO CHA DHARURA CHA MUHIMBILI KUTOA BIMA YA AFYA KWA WATOTO
HomeBiashara

BANCABC YASHIRIKIANA NA KITENGO CHA DHARURA CHA MUHIMBILI KUTOA BIMA YA AFYA KWA WATOTO

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Wazee Ummy Mwalimu akikabidhi moja ya kadi za bima kwa watoto zaidi ya 100 wanaoishi kw...

WANAWAKE WASHIKA NAFASI MBALIMBALI ZA UONGOZI MASOKONI JIJINI DAR ES SALAAM
ZINGATIA KUNUFAIKA NA OFA MBALIMBALI ZINAZOTANGAZWA
BENKI YA KCB TANZANIA YAZINDUA WARSHA YA BIASHARA CLUB KWA WATEJA WAKE AMBAO NI WAJASIRIAMALI WADOGO NA WAKATI



Waziri
wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Wazee Ummy Mwalimu akikabidhi
moja ya kadi za bima kwa watoto zaidi ya 100 wanaoishi kwenye mazingira
magumu jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki ikiwa na ushirikiano baina
ya Kitengo cha magonjwa ya dharura cha Hospitali ya Taifa ya Muhimbili
na BancABC Tanzania.



Baadhi wa watoto wanufaika na kadi za bima wakiwa na walezi wao
wakisikiliza hotuba ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na
Wazee Ummy Mwalimu



Baadhi ya wafanyakazi wa Kitengo cha magonjwa ya dharura kutoka
Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wakifuatilia kwa umakini hotuba ya
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Wazee Ummy Mwalimu wakati
wa hafla ya kukabidhi kadi za bima kwa watoto zaidi100 ya ambao ni
mayatima

Baadhi ya wafanyakazi BancABC Tanzania wakifuatilia kwa umakini hotuba
ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Wazee Ummy Mwalimu
wakati wa hafla ya kukabidhi kadi za bima kwa watoto zaidi100 ya ambao
ni mayatima.
Waziri
wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Wazee Ummy Mwalimu akiongea na
Mkurugenzi wa Kitego cha wateja wakubwa na wadogo wa BancABC Joyce Malai
wakati wa kukabidhi kadi za bima kwa watoto zaidi ya 100 jijini Dar es
Salaam mwishoni mwa wiki ikiwa na ushirikiano baina ya Kitengo cha
magonjwa ya dharura cha Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na BancABC
Tanzania.

Picha ya Pamoja
Waziri
wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Wazee Ummy Mwalimu aikisisita
jambo kwa Mkurugenzi wa Kitego cha wateja wakubwa na wadogo wa BancABC
Joyce Malai wakati wa kukabidhi kadi za bima kwa watoto zaidi ya 100
jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki ikiwa na ushirikiano baina ya
Kitengo cha magonjwa ya dharura cha Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na
BancABC Tanzania. 

BancABC, ambayo ni sehemu ya Atlas Mara, imeshirikiana na Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ili kutoa huduma ya bima ya afya itakayofaidisha watoto 100 ambao ni yatima na wanaoishi katika mazingira magumu kupitia mradi mpya wa afya wa Muhimbili uliozinduliwa leo.

Akizindua mpango huo wa Afya wa Muhimbili Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, aliishukuru BancABC kwa kushirikiana na Hospitali ya Muhimbili katika suala hilo la kutoa huduma ya bima ya afya kwa watoto.

Alisema mradi huo wa Muhimbili kushirikiana na BancABC unaendea sambamba kabisa na malengo ya serikali iliyojiwekea katika kuhakikisha kuwa jamii inapata huduma ya Afya kwa uhakika katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwani watoto ndio moja ya makundi ambayo huathirika sana wasipopatiwa huduma za Afya za uhakika.

“Natoa wito kwa wazazi watumie fursa hii iliyotolewa na BancABC kwa ushirikiano na Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa kuwafungulia watoto wao akaunti BancABC ili kuhakikisha watoto wao wanapata huduma kwa uhakika muda wowote bila ya ulazima wa kuwa na fedha tasilimu pale mtoto anapougua,” alisema.

Alitoa wito pia kwa watoa huduma za kifedha nchini pamoja na mashirika mengine kuhakikisha yanaiga mfano huo wa BancABC kwani wizara yake iko tayarikushirikiana na taasisi ambazo ziko tayari kuimaisha huduma katika sekta ya afya hasa upande wa utoaji huduma.

Naye Mkuu wa Mkuu wa kitengo cha wateja wadogo wadogo na wafanyabiashara wa kati, Bi Joyce Malai alisema BancABC inatambua umuhimu wa kuwa kampuni inayowajibika katika masuala ya kijamii kwa kurudisha kwa jamii sehemu ya faida na hasa katika sekta muhimu sana ya afya, dhamira hii ya BancABC kusaidia kwenye kuwezesha Afya ya watoto ni yamsingi sana kwa kuwa pia inasaidia serikali kufikia malengo yake.

Alisema baada ya kufungua akaunti hizo, wazazi wa watoto wenye akaunti hizo watakuwa wanahimizwa wakewe hela mara kwa mara kwa ajili ya bima ya watoto wao ili wapate huduma kupitia akaunti hizo za Mwangaza Junio Kids Accountambayo haina tozo ya kila mwezi.

Bi Joyce Malai aliongeza kuwa huduma hiyo ya bima haitakuwa na masharti kuhusu umri. “Wazazi wanaweza kufungua akaunti kwa mtoto zaidi ya moja na kuweka fedha kiasi chochote wanachotaka kwani itasaidia kuhakikisha watoto wao wana bima,”. 

Nae Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa, Prof. Lawrence Museru, aliishukuru BancABC kwa ushirikiano huo na kusema hatua hii haitasaidia watoto kupata tu huduma za afya kwa kupitia bima, bali itawajengea pia utamaduni wa kuweka akiba katika benki kuanzia utotoni hadi wanapokuwa watu wazima ili wapange mambo yao vizuri .

“Kwa sasa akaunti hizi zitafunguliwa na wazazi wao ila watakuwa wakitambua umuhimu wa huduma hii na wataendelea nayo hadi ukubwani,"alisema na kutoa rai kwa wazazi watumie fursa hiyo vizuri.
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: BANCABC YASHIRIKIANA NA KITENGO CHA DHARURA CHA MUHIMBILI KUTOA BIMA YA AFYA KWA WATOTO
BANCABC YASHIRIKIANA NA KITENGO CHA DHARURA CHA MUHIMBILI KUTOA BIMA YA AFYA KWA WATOTO
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhvBbSADfp_54IYCmRHyNuRXAjV8nrqzNrJArAllrWFY33-B8k3GwGBc_-VKsOTk7daXespRypjDlH3-z9mzSEVrDuYYv6IJu9UxnMPb6wTmNfKFoicK8Vjm2LmbtebOTd7WARRdEFL1KWh/s640/0D6A0435.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhvBbSADfp_54IYCmRHyNuRXAjV8nrqzNrJArAllrWFY33-B8k3GwGBc_-VKsOTk7daXespRypjDlH3-z9mzSEVrDuYYv6IJu9UxnMPb6wTmNfKFoicK8Vjm2LmbtebOTd7WARRdEFL1KWh/s72-c/0D6A0435.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/11/bancabc-yashirikiana-na-kitengo-cha.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/11/bancabc-yashirikiana-na-kitengo-cha.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy