WATANZANIA TUENDELEE KUICHANGIA TAASISI YA JKCI: DKT.TULIA
HomeJamii

WATANZANIA TUENDELEE KUICHANGIA TAASISI YA JKCI: DKT.TULIA

Na Agness Moshi na Bushiri Matenda –MAELEZO. Watanzania na wadau  mbalimbali wa sekta ya Afya nchini wameombwa kuendelea  kuisaidia Taasi...

RAIS MHE. DKT. MAGUFULI AONDOKA UGANDA MARA BAADA YA KUHUDHURIA VIKAO VYA WAKUU WA NCHI ZA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI (EAC)
OSHA YASISITIZA KADA YA USALAMA KAZINI KUTAMBULIKA RASMI
MPINA APIGA FAINI SHILINGI BILIONI 19 MELI 19 ZILIZOTOROKA BILA KUKAGULIWA
Na Agness Moshi na Bushiri Matenda –MAELEZO.
Watanzania na wadau  mbalimbali wa sekta ya Afya nchini wameombwa kuendelea  kuisaidia Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) ili iendelee kufanya kazi kwa ufanisi na kutoa huduma bora.
Hayo yamesemwa na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Mfuko wa Tulia Trust Mhe. Dkt. Tulia Akson, wakati akikabidhi msaada  runinga nne na katoni mbili za maziwa vyenye thamani ya  shilingi 1,000,000 vilivyotolewa kwa watoto waliopo kwenye Taasisi hiyo kwa ushirikiano na Dstv, TSN na Kampuni ya Twincity.
Dkt. Tulia amesema msaada  wa Luninga unatimiza ahadi waliohaidi kwa taasisi hiyo na unamaana kubwa sana kwa sababu utawasaidia watoto wanaokaa hospitalini hapo kwa muda mrefu  kujifunza ,na kuwaburudisha  kwa kipindi chote cha matibabu ya awali  kabla ya kufanyiwa upasuaji.
“Watoto hawa wanakaa muda mrefu hospitalini wakitibiwa hivyo wanashindwa kujumuika na wenzao kwa michezo jambo ambalo linawafanya wahisi upweke  kwa kuwapatia runinga kutawasaidia kuondoa hali hiyo , kuwaburudisha na kuwapa nafasi ya  kujifunza kupitia vipindi mbalimbali vinavyorushwa na king’amuzi cha DSTV”, alisema Dkt.Tulia
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI Profesa Mohammed Janabi amesema kuwa si watoto tu watakaofaidika kwani hata wazazi wao wataweza kujua mambo mbalimbali  yanayoendelea Nchini kwa kuangalia taarifa za Habari zitakazokua zinaonyeshwa kupitia chaneli mbalimbali.
“ Sio watoto wote wanaokuja hapa wanatatizo la moyo peke yake wengine wanakuja wakiwa na magonjwa mengine  ambapo inabidi  tuanze kuwatibia kwanza magonjwa hayo ambapo wakati mwingine yanachukua muda mrefu  hivyo basi kwa kipindi chote hicho runinga hizi zitakua zikiwapa burudani, elimu kwa masomo mbalimbali kama vile kiingereza, hesabu  kwa watoto wakubwa na kwa wale wadogo wataburudika kupitia katuni”,alisema Profes Janabi.
Profesa Janabi ameongeza kuwa msaada wa maziwa waliopewa utasaidia kuimarisha afya za watoto wadogo wanaotibiwa kwani wapo wengine wamekuja wakiwa na Afya duni, wengine wana magonjwa ya utapia mlo hivyo kupelekea kuchelewa kupatiwa matibabu.
Aidha, Profesa Janabi amemshukuru Dkt. Tulia kupitia Mfuko wake wa Tulia Trust kwa kuendelea kuhamasisha wadau mbalimbali kuipatia misaada Taasisi hiyo.
Kwa upande wake mtoto Mwamvita Hassani mwenye umri wa miaka 13 kutoka wilayani Kondoa kwa niaba ya watoto wanaotibiwa kwenye Taasisi hiyo ametoa shukrani zake kwa Naibu Spika na wadau waliowapa misaada hiyo.
“Ninawashukuru sana kwakutuletea Tv na Maziwa,Tumefurahi na tunawaombea watuletee Tv zingine”, alisema Mwamvita.

Profesa Janabi  amewaomba wadau mbalimbali kujitokeza kusaidia upatikanaji wa vitanda kwa ajili ya Taasisi hiyo kwani wanakabiliwa na  changamoto mbalimbali ikiwemo swala la upungufu wa vitanda kwa wagonjwa kwani wanavitanda 128 tu ambavyo havikidhi mahitaji kutokana na idadi kubwa ya wagonjwa wanaofika kwa ajili ya matibabu.




Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI Profesa Mohammed Janabi akimpatia maelezo Mwenyekiti wa Mfuko wa Tulia Trust Mhe. Dkt. Tulia Akson alipotembelea watoto wagonjwa wanaotibiwa kwenye Taasisi hiyo jijini Dar es Salaam leo.


 Mwenyekiti wa Mfuko wa Tulia Trust Mhe. Dkt. Tulia Ackson akiwa katika picha ya pamoja na watoto wanaotibiwa kwenye Taasisi hiyo jijini Dar es Salaam leo. Pamoja nao ni walezi na wauguzi wa Taasisi.

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: WATANZANIA TUENDELEE KUICHANGIA TAASISI YA JKCI: DKT.TULIA
WATANZANIA TUENDELEE KUICHANGIA TAASISI YA JKCI: DKT.TULIA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhQVtIMdr-HWfA-XC0FoZnR2jBgFPhDB4nM2MBIyZbSQddPDTFb7RpZftuZH0B3fk3Sl8rDM_o0r49yjIVIVCta1EpltW-Za878kImv-ynaLYL5a5KtRK2hQNF8mS1O1OjiVxu_MzpgwrA/s640/PIX1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhQVtIMdr-HWfA-XC0FoZnR2jBgFPhDB4nM2MBIyZbSQddPDTFb7RpZftuZH0B3fk3Sl8rDM_o0r49yjIVIVCta1EpltW-Za878kImv-ynaLYL5a5KtRK2hQNF8mS1O1OjiVxu_MzpgwrA/s72-c/PIX1.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/08/watanzania-tuendelee-kuichangia-taasisi.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/08/watanzania-tuendelee-kuichangia-taasisi.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy