SINGIDA INAZALISHA NUSU YA ASALI YOTE INAYOZALISHWA NCHINI; WAZIRI MKUU MSTAAFU PINDA AELEZA
HomeJamii

SINGIDA INAZALISHA NUSU YA ASALI YOTE INAYOZALISHWA NCHINI; WAZIRI MKUU MSTAAFU PINDA AELEZA

   Waziri Mkuu Mstaafu Mheshimiwa Mizengo Peter Pinda akizindua kikundi cha wazalishaji nyuki cha Kisaki katika manispaa ya ...

CHAMA CHA WAKUNGA TAWI LA HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI (MNH) CHATOWA HUDUM BURE KWA WANANCHI
WAZIRI SIMBACHAWENE ATOA MAAGIZO KWA WAKUU WA MIKOA
MHANDISI LWENGE: HAKUNA MUDA UTAKAO ONGEZWA MSIPOKAMILISHA MRADI KWA WAKATI


 
 Waziri Mkuu Mstaafu Mheshimiwa Mizengo Peter Pinda akizindua kikundi cha wazalishaji nyuki cha Kisaki katika manispaa ya Singida. 


Waziri Mkuu Mstaafu Mheshimiwa Mizengo Peter Pinda akiwa anatazama asali inayozalishwa na kikundi cha wazalishaji nyuki Kisaki, Kulia kwake ni Mkurugenzi wa kikundi hicho Philemon Kiemi. 

Waziri Mkuu Mstaafu Mheshimiwa Mizengo Peter Pinda akimpongeza Jacob Edward Mashimba kwa kuhitimu mafunzo ya ufugaji nyuki kibiashara kabla ya kumtunuku cheti cha mafunzo hayo.
Eneo la kikundi cha wafugaji nyuki kibiashara likiwa na mizinga ya nyuki ya kutosha katika kijiji cha Kisaki, Manispaa ya Singida. Waziri Mkuu Mstaafu Mheshimiwa Mizengo Peter Pinda akipata maelezo ya ukamuaji na upakiaji wa asali kisasa kutoka kwa Mkurugenzi wa kikundi cha uzalishaji nyuki Philemon Kiemi.

……………………………………………………………………………….

Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda Mkoa wa Singida kwa kuzalisha nusu ya asali yote inayopatikana nchini Tanzania.

Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda ametoa pongezi hizo wakati akifunga mafunzo ya ufugaji nyuki kibiashara wa kikundi cha wafugaji nyuki wa kijiji cha Kisaki Manispaa ya Singida ambapo aliwatunuku vijana 23 vyeti vya mafunzo hayo.

Amesema Singida imekuwa ikizalisha tani elfu 17 kwa mwaka huku uzalishaji kwa nchi nzima ukiwa ni tani elfu 34 kwa mwaka hivyo basi wananchi watumie fursa ya hiyo kuzalisha asali bora ili ipate soko la kimataifa.

Mheshimiwa Pinda amesema asali ina faida kubwa kwakuwa imekuwa ikitumika kama chakulana pia dawa huku akiongeza kuwa baadhi ya wazalishaji wameweza kutumia nta kuzalisha mshumaa na gundi ijapokuwa bado si kwa kiwango cha kutoshelesha hata soko la ndani.

Ameongeza kuwa kuwa wananchi watumie fursa ya nchi ya Tanzania kuwa na misitu hekta milioni 35 kufuga nyuki kwa wingi ili misitu hiyo iwezwe kutunzwa huku ikiwafaidisha kwa kuvuna asali na mazao yake.

Mheshimiwa Pinda amewaasa vijana waliohitimu mafunzo ya ufugaji nyuki kibiashara kuhakikisha wanaisambaza elimu waliyoipata kwa wenzao pamoja na wao kuwa wagujai nyuki wa mfano katika maeneo yao.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Singda Elias Tarimo amesema Manispaa ya Singida ina vikundi 16 vya uufugaji nyuki na wafugaji nyuki wengi wakiwa katika kata za Uhamaka, Mungumaji, Mtamaa, Mwankonko na Kisaki.

Tarimo amesema wataendelea kuhamasisha vijana na wakazi wengi kufuga nyuki kisasa na kusisitiza ufugaji nyuki kibiashara ndio wenye tija na manufaa kwa mfugaji.

Mmoja wa wahitimu Jacob Edward Mashimba amesema mafunzo ni mazuri na yatawasaidia katika kutunza mazingira kutokana na jamii imekuwa ikikata miti kwa wingi.

Mashimba amesema katika jamii anayotoka ya kihadzabe ambayo bado inategemea asali kama chakula kikuu elimu ya ufugaji nyuki kibiashara itasaidia licha ya upungufu wa baadhi ya vifaa vya kisasa vya ufugaji nyuki.
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: SINGIDA INAZALISHA NUSU YA ASALI YOTE INAYOZALISHWA NCHINI; WAZIRI MKUU MSTAAFU PINDA AELEZA
SINGIDA INAZALISHA NUSU YA ASALI YOTE INAYOZALISHWA NCHINI; WAZIRI MKUU MSTAAFU PINDA AELEZA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg9PXsJtk-J2-m2COQyvR6ni7ENDZ9cz_fUuqA2Qm1PZh8HZXgOyh7JCm2AsDce25VsMEIaKaLXOqro5XDpXPJSYHBKt9YnClYIsPse5_w-gjFDz_nmiczqYcCpzFu1bWO103FR7hzV9LQ/s640/DA2-2.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg9PXsJtk-J2-m2COQyvR6ni7ENDZ9cz_fUuqA2Qm1PZh8HZXgOyh7JCm2AsDce25VsMEIaKaLXOqro5XDpXPJSYHBKt9YnClYIsPse5_w-gjFDz_nmiczqYcCpzFu1bWO103FR7hzV9LQ/s72-c/DA2-2.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/05/singida-inazalisha-nusu-ya-asali-yote.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/05/singida-inazalisha-nusu-ya-asali-yote.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy